Mtanzania wa kwanza kupanda mt evarest - Wilfred Moshi

@ WatoaPovu
Wabongo mara nyingi linapofika swala la kuambiwa ukweli wanakua mbogo,sijajua tatizo ni nini? Ukweli kwamba hizo ni sifa za kijinga au mnataka kuturudisha ukoloni kwamba wazungu ndio watu wa kwanza kuona mlima kilimanjaro and then what? Amepata nini kwa kupanda huo mlima?
 
wilfred ni rafiki yangu na ni kweli amefika kilele cha mlima everest,anaishi moshi na ni tour Guide wa siku nyingi pale moshi mjini pia ni IT expert wa siku nyingi sana na aliwahi kufanya kazi internrt cafe maarufu ya moshi mjini easycom....haikua rahisi kwake kupanda mlima huo ila alikua na determination siku nyingi sana na piaa aliomba michango na akatangaza kwenye runinga watu wengi walimkashifu na pia walimpuuza lakini nwishowe ameweza...

record kama hz wenzetu huwa wanazitumia vizuri sana,namjua jamaa mwingine wa moshi pia ambae angeweza kuupanda huo mlima mwaka 2004 ila alinyimwa leseni kimizengwe sana anakaa maeneo ya kiboroloni na yeye pia ni guide maarufu....la kujiuliza ni kuwa tutautumiaje uzoefu wa wilfred au fred kama tunavyomuita kujitangaza kiutalii? je wizara yetu ya utalii ina taarifa na huyu bwana? haya kama kuna mtanzania anahitaji no ya wilfred au wizara anipm ataipata namba yake na kufanya nae mawasiliano kama kawaida...
 
Back
Top Bottom