Netanyahu
Senior Member
- Oct 2, 2008
- 147
- 22
Na Festo Polea
10/16/2009
ASHISH Thakkar anatarajia kuwa Mtanzania wa kwanza kwenda mwezini wakati atakapofanya safari hiyo mwakani.
Mtanzania huyo, ambaye ni chotara wa Kiingereza alienda Ikulu jijini Dar es salaam jana kumueleza Rais Jakaya Kikwete kuhusu safari yake na kumuaga.
Thakkar, ambaye mama yake ni mzaliwa wa Mwanza na baba Uingereza, alimwambia rais kuwa anajisikia vizuri kuwa mwakilishi wa Afrika, na hasa Tanzania kwenye safari hiyo ya angani.
"Najisikia vizuri kuwa mwakilishi wa Afrika hasa Tanzania ambako mama yangu alizaliwa, na hii itakuwa nafasi muhimu kwetu kujitangaza duniani kote na kuieleza dunia kuwa Afrika tunaweza na tuna maliasili za pekee,"alisema Takkar alipokuwa akizungumza na Rais Kikwete.
Rais alimweleza Mtanzania huyo anatakiwa apige picha nyingi atakapokwenda mwezini kwa ajili ya kujitangaza zaidi na kuinadi sekta ya utalii kwa juhudi zake zote.
Rais Kikwete alimkabidhi mwanaanga huyo bendera ya Tanzania na kusema watu wenye damu ya Tanzania wapo wengi duniani kote, lakini hawajitokezi kuitangaza nchi kama anavyofanya Thakkar.
"Ni nafasi nzuri kujitangaza kwa kuwa hauwezi kufanikiwa katika utalii bila kujitangaza na tunataraji kupitia Thakkar tutatangaza vyema utalii wetu popote atakapokuwa mwanaanga huyu angani na ardhini,"alisema Rais Kikwete.
SOURCE: MWANANCHI NEWSPAPER .
MY COMMENTS
Ingekuwa nchi nyingine habari hii ingekuwa breaking news vyombo vyote vya habari vya nchi husika lakini Tanzania mhhhhhh hatujui kupigia kelele na parapanda tunapofanya vizuri medani za kimataifa kwa vitu kama hivi yaani taarifa hii haikupewa hata robo saa kwenye vipindi vya vyombo vyetu vya habari wako tayari kuweka nusu saa vipindi vya kuigiza vya BONGO DAR ES SALAAM NA VILE VYA ZE COMEDY VYA AKINA MASANJA LAKINI HABARI KAMA HII NZITO HAINA NAFASI.NDIO MAANA WATANZANIA WENGI NI MABWEGE.
Hongera Takkar na hongera Kikwete kumtambua na hongera Gazeti la Mwananchi kuweka habari hii.
10/16/2009
ASHISH Thakkar anatarajia kuwa Mtanzania wa kwanza kwenda mwezini wakati atakapofanya safari hiyo mwakani.
Mtanzania huyo, ambaye ni chotara wa Kiingereza alienda Ikulu jijini Dar es salaam jana kumueleza Rais Jakaya Kikwete kuhusu safari yake na kumuaga.
Thakkar, ambaye mama yake ni mzaliwa wa Mwanza na baba Uingereza, alimwambia rais kuwa anajisikia vizuri kuwa mwakilishi wa Afrika, na hasa Tanzania kwenye safari hiyo ya angani.
"Najisikia vizuri kuwa mwakilishi wa Afrika hasa Tanzania ambako mama yangu alizaliwa, na hii itakuwa nafasi muhimu kwetu kujitangaza duniani kote na kuieleza dunia kuwa Afrika tunaweza na tuna maliasili za pekee,"alisema Takkar alipokuwa akizungumza na Rais Kikwete.
Rais alimweleza Mtanzania huyo anatakiwa apige picha nyingi atakapokwenda mwezini kwa ajili ya kujitangaza zaidi na kuinadi sekta ya utalii kwa juhudi zake zote.
Rais Kikwete alimkabidhi mwanaanga huyo bendera ya Tanzania na kusema watu wenye damu ya Tanzania wapo wengi duniani kote, lakini hawajitokezi kuitangaza nchi kama anavyofanya Thakkar.
"Ni nafasi nzuri kujitangaza kwa kuwa hauwezi kufanikiwa katika utalii bila kujitangaza na tunataraji kupitia Thakkar tutatangaza vyema utalii wetu popote atakapokuwa mwanaanga huyu angani na ardhini,"alisema Rais Kikwete.
SOURCE: MWANANCHI NEWSPAPER .
MY COMMENTS
Ingekuwa nchi nyingine habari hii ingekuwa breaking news vyombo vyote vya habari vya nchi husika lakini Tanzania mhhhhhh hatujui kupigia kelele na parapanda tunapofanya vizuri medani za kimataifa kwa vitu kama hivi yaani taarifa hii haikupewa hata robo saa kwenye vipindi vya vyombo vyetu vya habari wako tayari kuweka nusu saa vipindi vya kuigiza vya BONGO DAR ES SALAAM NA VILE VYA ZE COMEDY VYA AKINA MASANJA LAKINI HABARI KAMA HII NZITO HAINA NAFASI.NDIO MAANA WATANZANIA WENGI NI MABWEGE.
Hongera Takkar na hongera Kikwete kumtambua na hongera Gazeti la Mwananchi kuweka habari hii.