Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 98,023
- 142,774
ukatili hauna kabila,dini wala rangi.
Bahati mbaya wapo watu wanaoamini hivyo, kwamba ukatili unahusiana na rangi, dini, kabila, na kadhalika ilhali uhalisia wa mambo uko tofauti na hizo imani zao.
Kwangu mimi huo ni ujinga. Nasema ujinga kwa sababu kama kweli mtu anajua (tukifuata fasili ya neno ujinga) basi hawezi kufikia hitimisho la kijinga namna hiyo kwa sababu haya matukio ya ukatili hutokea kila mahali.
Hata Tanzania yapo na ni mengi tu. Watu huua watoto wao, wenza wao, ndugu zao, jamaa zao, n.k.
Sasa mtu anadiriki kusema makabila ya Kinyamwezi na Kisukuma hayana ukatili kiasi kama alichofanya huyo bwana.
Huo ni ujinga. Ni ujinga kwa sababu kama angekuwa anajua basi ni asingesema hivyo hata kidogo.
Huko Usukumani kila siku watu wanauana. Kurasa za mwanzo mwanzo kwenye hii mada nimebandika picha ya katoto kalikocharangwa mapanga na baba'ake mzazi huko Shinyanga.
Nina ndugu wa karibu aliyeuliwa kwa kuchinjwa na kichwa chake kikatupwa kwenye majaruba ya mpunga. Na mimi ni Msukuma 100% na huyo ndugu yangu marehemu naye ni Msukuma 100% na waliomuua ni Wasukuma 100%.
Sasa huyu mtu anayedai Wasukuma na Wanyamwezi hawana ukatili kiasi hicho sijui anatumia vigezo katika kupima ukatili!
Yaani watu wa humu kwa kupenda kurundika rundika kijumla jumla tu hawajambo kwa kweli. Utadhani wanaishi dunia ingine tofauti kabisa na tuishiyo wengine.