Mtanzania aaga dunia huko Rwanda

Mtanzania aaga dunia huko Rwanda

inna lillahi wa inna ilaihi rajiun.
Poleni sana mungu amuweke mahala pema peponi.
Vingenevyo:
Humu watu wakianza kuandika au kutoa taarifa za vilio, nafasi ya kubadilishana hoja itakuwa haipo kabisa.
Labda kwa kuwa huyu mtanzania ni mchaga nini ndo maana taarifa yake inatolewa.?
mbona mkuu mkatili hivi mkeo bado uko nae nyumba moj

samahan kuuliza hvii ukijibu ntafafanua
 
Hahahha ..kaka sio sababu ya uchagga..ni mazingira tu..lengo ni ubalozi pale kigali ushtuke kidogo..maana una tabia ya kulalalala..kumbuka huyu ni konda tu..na maiti yabidi isafirshwe..so msaada wa ubalozi unahitajika

Kwanini msimwambie kagame kama mmeshindwa kusafilisha hiyo maiti? kwa mzee pk ni faster sana,ni kuwapatia ndege mpaka dar au mnasemaje? msisubiri ubalozi kula kona.
 
Polen wafiwa embu badaya taarifa jichangishen hata mkirud mkiwambia mnakadhaa wanajuawamalizaje

mungu awafariji
 
poleni sana je ubalozi umetoa ushirikiano unaotakiwa ??
 
Ndugu wanajukwaa..naleta habari za masikitiko za kifo cha Mtanzania mwenzetu aliyefariki kwa ajali ya maji hapa Rwanda.Kifo kimemkuta leo mida ya saa nne katika ziwa Kivu- mjini Gisenyi/Rubavu karibu na mpaka wa Goma/Kongo.

Kijana huyo aliyejulikana kwa jina Nasib Athuman(23),Mkazi wa Kinondoni(mchaga);alikuwa katika safari ya masafa marefu kutoka DSM kuelekea Goma-Kongo.Leo asubuhi walifika Gisenyi.Huku taratibu za kuvuka mipaka zikiendelea kijana huyo alikuwa na watanzania wenzake akiwemo kaka yake waliyekuwa pamoja katika roli hilo la mizigo; baada ya kuchezacheza mpira kijana huyo aliamua kwenda kuogelea ziwani(lipo eneo hilo).
Hivyo kijana alielekea eneo moja karibu na hotel ya serena..alijirusha majini(diving)..basi alivyo-dive hakuweza kutokea tena hadi vijana walipoamua kufuatilia na kumkuta chini kabisa akiwa ameshakata roho.Maiti ya kijana huyo imehifadhiwa katika hospitali ya serikali-Gisenyi.Tunasubiri kesho(siku ya kazi) ili kwa kushirikiana na mamlaka husika tutoe taarifa ubalozi wa Tanzania-Kigali kuona taratibu za kusafirisha mwili hapo kesho..Bwana alitoa na bwana ametwaa jina lake libarikiwe.Amina

CHANZO CHA HABARI: mimi mwenyewe nipo eneo la tukio

Poleni sana,Ina maana madereva wote waliokua hapo ni wageni wa safari za Goma?,Si tulishakatazwa wageni wasioge kwenye hilo ziwa,mbona waTanzania hatuelewi na kutii miiko ya nchi za watu?!.WAAMBIENI WOTE WLIOPO HAPO,WAGENI HAWARUHUSIWI KUOGA KWENYE HILO ZIWA WALA KUCHEZEA MAJI YA ZIWA KIVU.
 
poleni sana ila isije ikawa kuna hujuma zimefanywa na huyo dikteta maana mpaka sasa hatupo kwenye uhusiano mzuri

Ndugu sio Hujuma,hao itakua wameenda na vijana wageni kwa safari za Goma,kwa kawaida tulishakatazwa na wenyeji tuaioge kwenye hilo ziwa,mgeni akiingia tu kwenye hayo maji akitoka ni maiti
 
Ndugu wanajukwaa..naleta habari za masikitiko za kifo cha Mtanzania mwenzetu aliyefariki kwa ajali ya maji hapa Rwanda.Kifo kimemkuta leo mida ya saa nne katika ziwa Kivu- mjini Gisenyi/Rubavu karibu na mpaka wa Goma/Kongo.

Kijana huyo aliyejulikana kwa jina Nasib Athuman(23),Mkazi wa Kinondoni(mchaga);alikuwa katika safari ya masafa marefu kutoka DSM kuelekea Goma-Kongo.Leo asubuhi walifika Gisenyi.Huku taratibu za kuvuka mipaka zikiendelea kijana huyo alikuwa na watanzania wenzake akiwemo kaka yake waliyekuwa pamoja katika roli hilo la mizigo; baada ya kuchezacheza mpira kijana huyo aliamua kwenda kuogelea ziwani(lipo eneo hilo).
Hivyo kijana alielekea eneo moja karibu na hotel ya serena..alijirusha majini(diving)..basi alivyo-dive hakuweza kutokea tena hadi vijana walipoamua kufuatilia na kumkuta chini kabisa akiwa ameshakata roho.Maiti ya kijana huyo imehifadhiwa katika hospitali ya serikali-Gisenyi.Tunasubiri kesho(siku ya kazi) ili kwa kushirikiana na mamlaka husika tutoe taarifa ubalozi wa Tanzania-Kigali kuona taratibu za kusafirisha mwili hapo kesho..Bwana alitoa na bwana ametwaa jina lake libarikiwe.Amina

CHANZO CHA HABARI: mimi mwenyewe nipo eneo la tukio

Ningekuwa mwalimu wa kiswahili ningekuchapa bakora, huwezi kusema source ni wewe ulieko eneo la tukio wakati heading inasema huko(ukimaanisha haupo eneo la tukio). Pili sikuona umuhimu wa kuonesha kabila la victim ikiwa umeshatanguliza utaifa...
 
huyo kijana mama yake alishakufa siku nyingi,baba yake hana uwezo nae ni wa kuungaunga. Kijana alilelewa na bibi yake kwa miaka mingi. Alianzia ajira za utotoni kwa kuendesha bodaboda akiwa na umri mdogo mpaka juzijuzi kaka yake kindugu akamsaidia asafiri nae kama turnboy,walikua wakiogelea na wenzake ndipo maji yakawashinda nguvu,wengine naskia walilazwa hospital sijui kama wametoka,maskini ya Mungu na ndio mauti yamemkuta akiwa anasonga kutafuta maisha!.source:mtu anayemjua marehemu.Rip!
 
Ndugu sio Hujuma,hao itakua wameenda na vijana wageni kwa safari za Goma,kwa kawaida tulishakatazwa na wenyeji tuaioge kwenye hilo ziwa,mgeni akiingia tu kwenye hayo maji akitoka ni maiti

Kwanini wageni wanakufa? Je wenyeji wakiingia hawafi?
 
Back
Top Bottom