Mr Hassan Ngoma ni nani?Mawazo ya kuwadhihaki Watu huwa siyo mawazo ya Tija na acha kutetea Upumbavu. Huwezi kutumia platform kubwa kama ya kuwa katika Kipindi kinachoheshimiwa cha 360 Clouds tv halafu ukatokwa na comment ya Kifedhuli kabisa kama aliyoisema huyo Mtangazaji Hassan Ngoma. Na kibaya zaidi basi bora angekuwa kasema hayo maneno Kiutani tungemwelewa ila kayasema akimaanisha kabisa na kuonyesha kuwa alidhamiria kutuonyesha dharau na nyodo zake aliyarudia tena mara mbili tatu na kusisitiza kuwa Wasomi Wadaiwa sugu wote wa HESLB wafanye hima watembeze madeli ya Ice Cream wauze ili wapate Mamilioni ya Bodi ya Mikopo.
Hii ni dharau isiyovumilika na tunamtaka huyu Mtangazaji Hassan Ngoma wa Clouds tv upesi na haraka sana awaombe radhi hao wote aliowadhihaki. Kuna Watu hadi sasa wana maumivu makubwa ya kukosa Ajira huku wengine wakiwa wameshaathirika Kisaikolojia baada ya kujua wanadaiwa na HESLB na kimsingi tulidhani Mtu kama yeye mwenye Heshima yake Kijamii angekuwa na kauli nzuri na za kuwatia matumaini Wadaiwa na badala yake sasa anawadhihaki na kuwadharau.
Amenisikitisha mno.