Mtangazaji wa Clouds tv 360 awataka Wasomi wadaiwa HESLB wakauze Ice Cream walipe deni

Wewe unaona anaropoka wenzako wanatumia ushauri wake wanasonga mbele...Mtaani kwangu kuna mtu ni msomi wa degree ya medicine lakini anauza mkaa na ana store yake kubwa tu ya mkaa,magunia yanaondoka na anapiga pesa mbaya,mwingine ana masters ya education na anauza pumba kwa ajili ya chakula cha kuku nyie mnashangaa kuuza icecream?!
Tatizo la wasomi wa Tanzania mnataka kiyoyozi na kwenda mabega juu,mtaani fursa kibao nyie mnasubiri ofisi huku mnakufa njaa,kaulizeni mabilionea wa leo kina bakhresa,Mengi nk walianzaje kama hamjabaki midomo wazi.
Hakuna sehemu yeyote iliyoandikwa kwamba msomi hatakiwi kuuza Icecream,kama nyie mnaona aibu endeleeni na ubishoo wenu,vaeni tai sana,pigeni polish viatu ving'ae zaidi na muendelee kutafuta kazi za viyoyozi huku mkiendelea kudaiwa na HESLB na wakati mwingine utakuta huyo anayejidai msomi na hataki kuuza ice cream anakwenda kukopa hela ya kula kwa muuza icecream.
UKITAKA KUTAFUTA PESA USIONE AIBU,ukiuza nyanya,ukiuza mchicha,ukiuza mkaa,ukiuza pumba,ukiuza icecream utapata pesa.
Kabla haujaniquote na kuandika gazeti angalau hata ungeelewa, tatizo sio kuuza icecream hata kidogo. Tatizo ni uropokaji wake,na sio katika hili tu ni mropokaji mzuri tu.
Uliangalia kipindi au umeandika gazeti tu!! The way alivyoongea ndio tatizo, hakuongea kama ushauri, hapa suala sio kudharau kazi,anauza ice cream hadi maandazi Bakhresa itakuwa msomi!!!
 
Sijaona baya alilozungumza huyo hassan ngoma kwani ice CREAM sio biashara mbona kuna watu wanaishi kwa kuuza hizo ice CREAM au hao sio binadamu. Hayo no mawazo tu ambayo kayatoa mtangazaji sasa kama hakuna kazi ufanyeje kwa mfano ! Ukae tu nyumbani si bora ujishughulishe na biashara yoyote ikiwemo kuuza hizo ramba ramba maisha yaendelee mbona tunao wasomi wengi tu na bado wanafanya biashara za machinga kariakoo..... Tuache mawazo mgando na kuuza ice CREAM sio tusi wala sio dharau usisubiri kukaa ofisini hata maji wewe tembeze tu
 
kama unaakili,jiulize serikali haitoi ajira , mikopo hamna , kilimo hakilipi, bora aiskrim ili serikal waone wapi wamekosea,yuko sahihi
 
Kabla haujaniquote na kuandika gazeti angalau hata ungeelewa, tatizo sio kuuza icecream hata kidogo. Tatizo ni uropokaji wake,na sio katika hili tu ni mropokaji mzuri tu.
Uliangalia kipindi au umeandika gazeti tu!! The way alivyoongea ndio tatizo, hakuongea kama ushauri, hapa suala sio kudharau kazi,anauza ice cream hadi maandazi Bakhresa itakuwa msomi!!!
Ni kweli mkuu sikumsikia,possibly ningemsikia ningekuja na kitu tofauti,niwie radhi na gazeti langu.
 
-->>hata hivyo kulipa fedha hizi kwa heslb ni suala lisilokwepeka kwa binafsi naona ni lazima zilipwe /ILI WENGINE NAO PIA WAWEZE KUSOMA.
•NI LAZIME KUWE NA BALANCES YA UTOAJI WA FEDHA HIZI NA MAREJESHO YA FEDHA HIZI.
•PIA NADHANI MFUMO WA UKOPESHWAJI UREKEBISHWE KWA MAANA YA KWAMBA "MKOPESHWAJI ATALIPA FEDHA HIZI BILA YA KIGEZO CHA KUWA AMEPATA AJIRA AU LA"
•HILI LITAMJENGA MWANAFUNZI NA FAMILIA YAKE KISAIKOLOJIA MAPEMA....(kwamba kuna deni)
hii imekaa vizuri no way out kulipa kuko palepale!!!!!!
 
Mimi hilo deni sitakuja nilipe ase, yani nipige kazi zangu binafsi halafu nije niwalipe tu kirahisi *****
 
Sasa kama unatafuta ajira haipatikani ni bora ukae pasipo kazi au ufanye chochote kitacho kusaidia kuendesha maisha wapo walio fanya biashara ya juisi naleo hii ni matajiri wa kutolewa mfano.
 
Kwan elimu za watangazaji wengi sizinafahamika?? Wao wanasema wanajali kipaji cha kuongea wala siyo elimu. Simshangai
 
Siku hizi watangazaji wenye akili zao ni wachache sana.saivi ukijua kuongea saaaana basi waweza kuwa mtangazaji!!
Yule jamaa kawaida yake kuongea kuongea tu ili asitoke kwenye kipindi bila kuongea.
 
MIE NIKAJUA NI MTU MWENYE AKILI ZAKE KUMBE ANA AKILI MGANDO SANA ALIDHANI ALIVYOKOPESHWA MKOPO NANI AMLIPIE,NILIDHANI ATALETA MBINU MPYA KWA WANACHUO WENZIE NAMNA YA KUREJESHA MKOPO BADALA YAKE ANAANDIKA MIPASHO
We mwenyewe unabwabwaja mipasho humu na unadhani upo kijiweni wanakufahamu, unakera na utoto wako eboooo.....
 
Shukhrani ya Punda mateke.
Mtangazaji ustaadh Hassan nakupa 100,deni lilipwe,mlipewa mkasema msipangiwe matumizi,kulipa nako msipangiwe?ebo?
Tena nasema,kuanzia mwakani kama hujaanza kulipa hakuna kuoa!
Utalipa wewe, wengine hatulipi na keki inatafunwa taratibuu bila kero... Aseee
 
Je, sidhani kama ni sahihi kuanza kunikata mkopo kwa asilimia 15 wakati Mimi na wao tuliingia mkataba wa kukatwa asilimia 8. Hii haivumiliki, kwa kweli. Sheria hii ya 15% ilitakiwa itumike wakati gani? Nadhani hapa kuna changamoto, tunaomba wanasheria mtusaidie
Kweli mkuu na muda wa kulipa I think ni miaka 10, kuna haja ya wanasheria kwenda mahakamani kuhoji hiki kitu.
 
Na mwisho wa siku hawatapigiwa simu za pongezi wala kadi za sikukuu. Kimsingi hachombezi kwenye hoja fikirishi na jenzi. Jana alikuwepo prof Mkumbo akipresent yanayoitesa nchi, badala ya kuuliza maswali ya hoja tangulizi yeye anajamtoa kwenye hoja ya msingi. Nilichoka kabisa.
Namsihi akamuone mtaalamu wa saikolojia.. Huyo kijana anayo matatizo makubwa sana ya kisaikolojia
 
Back
Top Bottom