Mtangazaji 'Diva The Bawse' aaga rasmi Wasafi Media

Mtangazaji 'Diva The Bawse' aaga rasmi Wasafi Media

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,397
Reaction score
14,505
Mtangazaji maarufu na kipenzi cha mashabiki, Diva Gissele Malinzi almaarufu Diva The Bawse, ametangaza rasmi kuachana na kituo cha Wasafi Media, akieleza kuwa amefikia hatua ya kuanza ukurasa mpya katika maisha yake ya kazi.

1752649653319.png
Kupitia ujumbe uliojaa hisia, shukrani na upendo mkubwa kwa familia ya Lavidavi na timu nzima ya Wasafi, Diva amesema amewasilisha barua yake ya kuondoka mapema leo asubuhi, ameeleza kuwa kipindi cha Lavidavi kilikuwa moja ya sura nzuri zaidi katika taaluma yake, na kwamba kila usiku, kila sauti ya msikilizaji na kila ujumbe vilikuwa sehemu ya moyo wake.

"Tumejenga nyumba ya hadithi halisi za mapenzi, uponyaji, vicheko, ujasiri na mazungumzo ya kweli. Mmenilea, mmenisukuma, na mmenifanya kuwa bora zaidi," ameandika Diva.

Akiwaaga kwa heshima timu nzima ya Wasafi, kuanzia kwa watayarishaji, timu ya kidijitali, wahandisi wa sauti hadi uongozi, Diva amesema anaanza msimu mpya wa maisha, lakini akasisitiza kuwa huu si mwisho wa safari, bali ni pumziko la heshima.

"Popote nitakapokwenda, roho ya Lavidavi itaendelea kuishi. Endeleeni kupenda, kupona, na kuamini katika mapenzi."

Kwa miaka kadhaa, Diva The Bawse amekuwa sauti ya kipekee usiku katika redio ya Wasafi, akitoa nafasi kwa simulizi za mapenzi, mafanikio na changamoto za maisha, huku akibaki kuwa miongoni mwa watangazaji wenye ushawishi mkubwa Tanzania.

Screenshot 2025-07-16 100550.png
 
Mtangazaji maarufu na kipenzi cha mashabiki, Diva Gissele Malinzi almaarufu Diva The Bawse, ametangaza rasmi kuachana na kituo cha Wasafi Media, akieleza kuwa amefikia hatua ya kuanza ukurasa mpya katika maisha yake ya kazi.

Kupitia ujumbe uliojaa hisia, shukrani na upendo mkubwa kwa familia ya Lavidavi na timu nzima ya Wasafi, Diva amesema amewasilisha barua yake ya kuondoka mapema leo asubuhi, ameeleza kuwa kipindi cha Lavidavi kilikuwa moja ya sura nzuri zaidi katika taaluma yake, na kwamba kila usiku, kila sauti ya msikilizaji na kila ujumbe vilikuwa sehemu ya moyo wake.

“Tumejenga nyumba ya hadithi halisi za mapenzi, uponyaji, vicheko, ujasiri na mazungumzo ya kweli. Mmenilea, mmenisukuma, na mmenifanya kuwa bora zaidi,” ameandika Diva.

Akiwaaga kwa heshima timu nzima ya Wasafi, kuanzia kwa watayarishaji, timu ya kidijitali, wahandisi wa sauti hadi uongozi, Diva amesema anaanza msimu mpya wa maisha, lakini akasisitiza kuwa huu si mwisho wa safari, bali ni pumziko la heshima.

“Popote nitakapokwenda, roho ya Lavidavi itaendelea kuishi. Endeleeni kupenda, kupona, na kuamini katika mapenzi.”

Kwa miaka kadhaa, Diva The Bawse amekuwa sauti ya kipekee usiku katika redio ya Wasafi, akitoa nafasi kwa simulizi za mapenzi, mafanikio na changamoto za maisha, huku akibaki kuwa miongoni mwa watangazaji wenye ushawishi mkubwa Tanzania.
At her age 37 yrs hana Nyumba ,hana ndoa hana mtoto anabidi kujitafakari Sana akumbuke Malinzi sio Baba yake hivyo anaweza asimpe urithi.
 
Mtangazaji maarufu na kipenzi cha mashabiki, Diva Gissele Malinzi almaarufu Diva The Bawse, ametangaza rasmi kuachana na kituo cha Wasafi Media, akieleza kuwa amefikia hatua ya kuanza ukurasa mpya katika maisha yake ya kazi.

Kupitia ujumbe uliojaa hisia, shukrani na upendo mkubwa kwa familia ya Lavidavi na timu nzima ya Wasafi, Diva amesema amewasilisha barua yake ya kuondoka mapema leo asubuhi, ameeleza kuwa kipindi cha Lavidavi kilikuwa moja ya sura nzuri zaidi katika taaluma yake, na kwamba kila usiku, kila sauti ya msikilizaji na kila ujumbe vilikuwa sehemu ya moyo wake.

"Tumejenga nyumba ya hadithi halisi za mapenzi, uponyaji, vicheko, ujasiri na mazungumzo ya kweli. Mmenilea, mmenisukuma, na mmenifanya kuwa bora zaidi," ameandika Diva.

Akiwaaga kwa heshima timu nzima ya Wasafi, kuanzia kwa watayarishaji, timu ya kidijitali, wahandisi wa sauti hadi uongozi, Diva amesema anaanza msimu mpya wa maisha, lakini akasisitiza kuwa huu si mwisho wa safari, bali ni pumziko la heshima.

"Popote nitakapokwenda, roho ya Lavidavi itaendelea kuishi. Endeleeni kupenda, kupona, na kuamini katika mapenzi."

Kwa miaka kadhaa, Diva The Bawse amekuwa sauti ya kipekee usiku katika redio ya Wasafi, akitoa nafasi kwa simulizi za mapenzi, mafanikio na changamoto za maisha, huku akibaki kuwa miongoni mwa watangazaji wenye ushawishi mkubwa Tanzania.

Nilishapita hapo
 
Mtangazaji maarufu na kipenzi cha mashabiki, Diva Gissele Malinzi almaarufu Diva The Bawse, ametangaza rasmi kuachana na kituo cha Wasafi Media, akieleza kuwa amefikia hatua ya kuanza ukurasa mpya katika maisha yake ya kazi.

Kupitia ujumbe uliojaa hisia, shukrani na upendo mkubwa kwa familia ya Lavidavi na timu nzima ya Wasafi, Diva amesema amewasilisha barua yake ya kuondoka mapema leo asubuhi, ameeleza kuwa kipindi cha Lavidavi kilikuwa moja ya sura nzuri zaidi katika taaluma yake, na kwamba kila usiku, kila sauti ya msikilizaji na kila ujumbe vilikuwa sehemu ya moyo wake.

"Tumejenga nyumba ya hadithi halisi za mapenzi, uponyaji, vicheko, ujasiri na mazungumzo ya kweli. Mmenilea, mmenisukuma, na mmenifanya kuwa bora zaidi," ameandika Diva.

Akiwaaga kwa heshima timu nzima ya Wasafi, kuanzia kwa watayarishaji, timu ya kidijitali, wahandisi wa sauti hadi uongozi, Diva amesema anaanza msimu mpya wa maisha, lakini akasisitiza kuwa huu si mwisho wa safari, bali ni pumziko la heshima.

"Popote nitakapokwenda, roho ya Lavidavi itaendelea kuishi. Endeleeni kupenda, kupona, na kuamini katika mapenzi."

Kwa miaka kadhaa, Diva The Bawse amekuwa sauti ya kipekee usiku katika redio ya Wasafi, akitoa nafasi kwa simulizi za mapenzi, mafanikio na changamoto za maisha, huku akibaki kuwa miongoni mwa watangazaji wenye ushawishi mkubwa Tanzania.

Aseme ukweli hana vigezo vya kuwa mwandishi kwa mujibu wa wizara ya habari
 
Back
Top Bottom