Avatar Myg
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 675
- 118
Kijana wa Kihaya aishiye huko Marekani alimpigia simu mama yake. Maongezi yao yalikuwa kama ifuatavyo: Kijana: Mama, nina virusi vya UKIMWI! Mama: Mwanangu, ninakusihi, ninakusihi, ninakusihi sana, usirudi nyumbani kabisa. Kijana: Kwa nini mama? Mama: Endapo utarudi nyumbani, mkeo pia ataathirika. Mkeo akiathirika atamwathiri pia mdogo wako. Mdogo wako akishaathirika atamwathiri pia msichana wetu wa kazi. Ujuwe mwanangu, msichana wetu wa kazi naye atamwathiri pia baba yako. Baba yako naye atamwathiri mdogo wangu, mdogo wangu atamwathiri mumewe ambaye naye ataniathiri mimi pia. Mimi nikishaathirika nitamwathiri mtunza bustani wetu. Mtunza bustani wetu akishaukwaa atamwambukiza pia mdogo wako wa kike. Mdogo wako akishaupata tu, ujuwe kijiji kizima kimeupata! Mwanangu, kwa jina la Mungu, tafadhali, tafadhali kiokoe kijiji chetu. Ninakusihi tena mwanangu, USIRUDI TENA NYUMBANI!