Msomi ni nani

Msomi ni nani

Mwakyembe kasoma shule ila HAJAELIKA. maaana yake nini ?

Maana yake ni hana AKILI, unaeza ukwa umesoma shule ila huna akili, UKITAKA MAELEZP ZAID, REPLY NTAKUPATIA MDADAVUO WA MAMBO YA SHULE, kuelimika na kuwa na akili,
 
Msomi
Ni mtu aliyepata Maarifa flani ambayo kwayo yanakuwa na manufaa kwa jamii yake.
Baadhi ya matokeo ya Msomi.
1. Abuni kitu au Jambo linaloinufaisha jamii Kama yule mgunduzi wa Umeme au Kijiko Cha kulia msosi.
2. Anayeweza zalisha ajira yoyote halali.
3. Anayeweza toa suluhisho flani la tatizo kama huduma muhimu au ya kawaida.
NK.
Ukiona mtu ana PHD halafu anategemea kuajiriwa na hazalishi chochote na huko ofisini kwake Hana Cha zaidi ya kujisalinisha posho na kuwanyima maslahi walio chini yake huyo ni Zero IQ.
Sio Msomi.
 
Ndugu yangu kujua kiingereza siyo kuwa msomi ile no lugha tu kama lugha zingine
ukishajua kuhesbu,kusoma na kuandika halafu ujue kuongea na kiingereza vizuri
[/QUOTE]
 
Habari wakuu.

Ningependa kufahamu ni kiwango gani cha elimu mtu akifikia anastahili kuitwa msomi?

Je, akijua kusoma na kuandika anastahili kuitwa msomi? Au akimaliza elimu ya msingi anafaa kuitwa msomi? Au kuitwa msomi kunaanzia ngazi ya elimu ya sekondari (O-level & A-level)? Au ni ngazi ya Astashahada, Stashahada, Shahada, Uzamili, Uzamivu hadi Uprofessa?

~Gai da seboga
Sisi wote watanzania tuna PhD.Rais kasema.
 
Msomi
Ni mtu aliyepata Maarifa flani ambayo kwayo yanakuwa na manufaa kwa jamii yake.
Baadhi ya matokeo ya Msomi.
1. Abuni kitu au Jambo linaloinufaisha jamii Kama yule mgunduzi wa Umeme au Kijiko Cha kulia msosi.
2. Anayeweza zalisha ajira yoyote halali.
3. Anayeweza toa suluhisho flani la tatizo kama huduma muhimu au ya kawaida.
NK.
Ukiona mtu ana PHD halafu anategemea kuajiriwa na hazalishi chochote na huko ofisini kwake Hana Cha zaidi ya kujisalinisha posho na kuwanyima maslahi walio chini yake huyo ni Zero IQ.
Sio Msomi.
Nakupata nakupataaa... Ongeza saut kidogo
 
Habari wakuu.

Ningependa kufahamu ni kiwango gani cha elimu mtu akifikia anastahili kuitwa msomi?

Je, akijua kusoma na kuandika anastahili kuitwa msomi? Au akimaliza elimu ya msingi anafaa kuitwa msomi? Au kuitwa msomi kunaanzia ngazi ya elimu ya sekondari (O-level & A-level)? Au ni ngazi ya Astashahada, Stashahada, Shahada, Uzamili, Uzamivu hadi Uprofessa?

~Gai da seboga
Kuanzia uzamili na kuendelea.
 
Wakati fulani hapa JF watu husema kusoma si kuelimika, hivi tofauti ya Elimu na usomi ni nini. Unawezaje kutofautisha msomi ambaye hajaelimika na mtu aliyeelimika lakini ambaye si msomi?
 
Msomi ni mtu aliyejifunza kitu katika fani fulani lakini hana uelewa wa fani zingine.

Elimu ni mchanganyiko wa fani nyingi mtu mwenye elimu anaweza kuwa aliishia darasa la saba

Lakini ana uwezo wa kutengeneza gari la mtu mwenye degree nne so elimu ni pana kuliko usomi.

Ndio maana unakuta doctor hana ujuzi wa kuendesha gari ila kijana mwenye elimu ya darasa la saba anaendesha gari kwa ustadi mkubwa.

Elimu inaunganisha vipaji vingi na mtu anayejua mambo mengi ila msomi ni matokeo ya kufundishwa kitu kimoja.

Kiufupi elimu ni kujifunza ila usomi ni kufundishwa.

Wajuzi watanirekebisha zaidi.
 
Asilimia 90 ya waliosoma Tanzania huwa hawaelimiki nililigundua hili nilipo enda TRA

Kodi yangu ya mwaka mzima ni tshs 150000 lakini mimi biashara nimeanza mwezi wa 9 nikaambiwa nilipe kodi yote ya mwaka haijalishi biashara nimeanza lini

Kanuni za kodi duniani kote inatakiwa mtu afanye biashara na apate faida ndio alipe kodi

Sasa wao walipo niambia nilipe kodi hadi ya miezi ambayo biashara haikuwepo yani mwezi January -- August wao mambo haya wameyasoma wapi

Nikaona kabisa hawa jamaa wamesoma lakini hawajaelimika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
technically umetoa maelezo yenye kufikirisha sana. Ila sijaelewa tofauti ya kujifunza na kufundishwa. Ina maana mtu anayefundishwa hawezi kujifunza kama yule anayejifunza mwenyewe bila ya kufundishwa?

live on mfano wako nimeupenda sana. Lakini hao wasomi wameshindwaje kujua kwamba haitakiwi mtu kulipa kodi kwa biashara ambayo hajaifanya? Walipokuwa vyuoni wakisomea mambo ya kodi hilo hawakujifunza?
 
Back
Top Bottom