Msomi ni nani

Msomi ni nani

Ahsante sana umedadavua kiasi kama nakuelewa,,,lakini vipi hii imekaaje,,Hata madiwani nao wanasema wasomi hawana kitu.
Au niseme labda msomi ni mtu yeyeote mwenye hekima na busara,,na si veti vya shule,,hebu nisaidie hapo
Naomba kuchangia tena.
Nadhani kuna tofauti ya maana ya kitu na namna kitu hicho kinavyopaswa kuwa.Daktari wa SUA aliebukua na kupata udaktari ni msomi.Jamii ipende isipende,ili kuwa na ujuzi alofikia muungwana huyo lazima hatua flani zipitiwe,ikiwa ni pamoja na kuingia darasani,kutoa mihadhara,nk.Hizo ni taratibu za kuingia daraja la usomi.Usomi wa Msomi usipoweza kuisaidia jamii,au kutokuwa na manufaa kwa jamii,inapelekea kushuka thamani kwa usomi huo,lakini hakuondoi usomi.Kitakachotengua usomi wa mhusika ni kukiuka kanuni na taratibu za fani husika,na sio flani anapenda au flani hapendi.Ikumbukwe,walomwingiza katika daraja hilo sio jamii bali WASOMI wenzie.Wanaweza kuwa mabwanyenye wanaofikiria maslahi yao binafsi,lakini huo ndio ukweli mchungu wa maisha.Kwa mfano,Tuna viongozi wabovu,lakini kwa vile wamechaguliwa (wakati mwingine kwa kununua kura) wanaendelea kuitwa viongozi.Je wabunge wasiowakilisha VEMA wananchi wao hatuendelei kuwaita WABUNGE?

Nadhani kisifa (adjective) USOMI inatokana na kitenzi (verb) SOMA au KUSOMA.Kwa mantiki hiyo,USOMI unahusiana na KUSOMA,na nomino MSOMI ni MTU ALIESOMA.Wakati mwingine maneno ya kiswahili yanaleta maana flani yanapoelekwa kwenye lugha nyingine.Kwenye Swahili-english dictionary,ukisaka maana ya neno MSOMI kwa Kiingereza inakupa majibu yafuatayo:

msomi , pl wasomi { English: intellectual }
noun

msomi , pl wasomi { English: learned person , pl learned people }
noun

msomi , pl wasomi { English: lecturer , pl lecturers } [derived: soma V]
noun

msomi , pl wasomi { English: reader } [derived: soma V]
noun ,

msomi , pl wasomi { English: scholar , pl scholars } [derived: Swahili -soma]
noun

5 distinct results returned (chanzo:THE KAMUSI PROJECT)

Kwa mtizamo wangu unaoweza kuwa sio sahihi,nadhani kuna umuhimu wa kutofautisha MATARAJIO YA JAMII KWA "WASOMI" na MAANA YA NENO "MSOMI".

Bwaya anahoji iwapo Profesa anayepika tafiti zake kwa manufaa ya mafisadi, je naye ni msomi?Yes,ni MSOMI,lakini ANAYEKIUKA KANUNI,TARATIBU NA SHERIA ZINAZOONGOZA FANI YAKE.

Kuna baadhi ya sifa ambazo mtu akishafanikiwa kuzipata hubaki nazo kwa muda mrefu kama sio milele.Ni mithili ya ualimu,jina linaendelea kubaki MWALIMU hata pale mtu anapostaafu au kufukuzwa kazi.

Naomba kunukuu hoja nzito ya Bwaya kwamba "....Ninawafahamu wanasayansi wengi waliokimbia umande, ama kushindwa mitihani, ambao maarifa yao yanaheshimika mpaka leo. Je, hawa si wasomi hata kama hawana vyeti? Hawakuwahi kuitwa madokta wala maprofesa, lakini waliweza kuyatumia maarifa yao wenyewe ambayo wasomi wa enzi hizo hawakuwa nayo!" Binafsi,nadhani mwanzoni mwa mjadala niligusia juu ya umuhimu wa vyeti KAMA KITAMBULISHO lakini haimaanishi kwamba kutokuwa na cheti kunamuondolea mtu umahiri wake katika fani husika.Pia ili mtu aitwe msomi si lazima awe dokta au profesa LAKINI LAZIMA ASOME,iwe nyumbani,darasani au kwa njia ya posta au kujielimisha kwa elimu vitendo.HUWEZI KUWA MSOMI PASIPO KUSOMA.Utawezaje kuwa mwanasayansi kama hujasoma sayansi?

Mwisho,wakati JAMII INATARAJIA wasomi wafanye vitu kwa manufaa kwa jamii,kutakuwa na wasomi watakaotimiza matarajio hayo,na kuna wengine ambao hawatatimiza.Wote wataendelea kuitwa wasomi.Kitakachozidi au kupungua ni heshima yao kwa jamii na wanafani wenzao.Kinyume cha matarajio ya jamii kuhusu kinachotarajiwa kutoka kwa anayeitwa MSOMI hakibadili maana ya neno MSOMI...just like UONGOZI MBOVU usivyoweza kuondoa maana ya neno UONGOZI (bali kuathiri TASWIRA ya uongozi).
Swali,je kuna neno MBADALA kwa mtu aliyesoma sana lakini kusoma huko hakuinufaishi jamii?
 
Kwani msomi ni nani? Wabobezi nifafanulieni
Msomi ni mtu aliyesoma.
Mtaalamu ni mtu aliye elimika.
Kuelimika kunatokana na kusoma na kusoma kunatokana na kujifunza na kujifunza ndiyo utaratibu wa kupata maarifa na maarifa huleta ujuzi na ujuzi ndiyo unaoweza kukurahisishia maisha yako na kuweza kuyamudu kwa usalama na urahisi.
 
Naomba kuchangia tena.
Nadhani kuna tofauti ya maana ya kitu na namna kitu hicho kinavyopaswa kuwa.Daktari wa SUA aliebukua na kupata udaktari ni msomi.Jamii ipende isipende,ili kuwa na ujuzi alofikia muungwana huyo lazima hatua flani zipitiwe,ikiwa ni pamoja na kuingia darasani,kutoa mihadhara,nk.Hizo ni taratibu za kuingia daraja la usomi.Usomi wa Msomi usipoweza kuisaidia jamii,au kutokuwa na manufaa kwa jamii,inapelekea kushuka thamani kwa usomi huo,lakini hakuondoi usomi.Kitakachotengua usomi wa mhusika ni kukiuka kanuni na taratibu za fani husika,na sio flani anapenda au flani hapendi.Ikumbukwe,walomwingiza katika daraja hilo sio jamii bali WASOMI wenzie.Wanaweza kuwa mabwanyenye wanaofikiria maslahi yao binafsi,lakini huo ndio ukweli mchungu wa maisha.Kwa mfano,Tuna viongozi wabovu,lakini kwa vile wamechaguliwa (wakati mwingine kwa kununua kura) wanaendelea kuitwa viongozi.Je wabunge wasiowakilisha VEMA wananchi wao hatuendelei kuwaita WABUNGE?

Nadhani kisifa (adjective) USOMI inatokana na kitenzi (verb) SOMA au KUSOMA.Kwa mantiki hiyo,USOMI unahusiana na KUSOMA,na nomino MSOMI ni MTU ALIESOMA.Wakati mwingine maneno ya kiswahili yanaleta maana flani yanapoelekwa kwenye lugha nyingine.Kwenye Swahili-english dictionary,ukisaka maana ya neno MSOMI kwa Kiingereza inakupa majibu yafuatayo:

msomi , pl wasomi { English: intellectual }
noun

msomi , pl wasomi { English: learned person , pl learned people }
noun

msomi , pl wasomi { English: lecturer , pl lecturers } [derived: soma V]
noun

msomi , pl wasomi { English: reader } [derived: soma V]
noun ,

msomi , pl wasomi { English: scholar , pl scholars } [derived: Swahili -soma]
noun

5 distinct results returned (chanzo:THE KAMUSI PROJECT)

Kwa mtizamo wangu unaoweza kuwa sio sahihi,nadhani kuna umuhimu wa kutofautisha MATARAJIO YA JAMII KWA "WASOMI" na MAANA YA NENO "MSOMI".

Bwaya anahoji iwapo Profesa anayepika tafiti zake kwa manufaa ya mafisadi, je naye ni msomi?Yes,ni MSOMI,lakini ANAYEKIUKA KANUNI,TARATIBU NA SHERIA ZINAZOONGOZA FANI YAKE.

Kuna baadhi ya sifa ambazo mtu akishafanikiwa kuzipata hubaki nazo kwa muda mrefu kama sio milele.Ni mithili ya ualimu,jina linaendelea kubaki MWALIMU hata pale mtu anapostaafu au kufukuzwa kazi.

Naomba kunukuu hoja nzito ya Bwaya kwamba "....Ninawafahamu wanasayansi wengi waliokimbia umande, ama kushindwa mitihani, ambao maarifa yao yanaheshimika mpaka leo. Je, hawa si wasomi hata kama hawana vyeti? Hawakuwahi kuitwa madokta wala maprofesa, lakini waliweza kuyatumia maarifa yao wenyewe ambayo wasomi wa enzi hizo hawakuwa nayo!" Binafsi,nadhani mwanzoni mwa mjadala niligusia juu ya umuhimu wa vyeti KAMA KITAMBULISHO lakini haimaanishi kwamba kutokuwa na cheti kunamuondolea mtu umahiri wake katika fani husika.Pia ili mtu aitwe msomi si lazima awe dokta au profesa LAKINI LAZIMA ASOME,iwe nyumbani,darasani au kwa njia ya posta au kujielimisha kwa elimu vitendo.HUWEZI KUWA MSOMI PASIPO KUSOMA.Utawezaje kuwa mwanasayansi kama hujasoma sayansi?

Mwisho,wakati JAMII INATARAJIA wasomi wafanye vitu kwa manufaa kwa jamii,kutakuwa na wasomi watakaotimiza matarajio hayo,na kuna wengine ambao hawatatimiza.Wote wataendelea kuitwa wasomi.Kitakachozidi au kupungua ni heshima yao kwa jamii na wanafani wenzao.Kinyume cha matarajio ya jamii kuhusu kinachotarajiwa kutoka kwa anayeitwa MSOMI hakibadili maana ya neno MSOMI...just like UONGOZI MBOVU usivyoweza kuondoa maana ya neno UONGOZI (bali kuathiri TASWIRA ya uongozi).
Swali,je kuna neno MBADALA kwa mtu aliyesoma sana lakini kusoma huko hakuinufaishi jamii?
kaka nimekuelewa,,umedadavua hakika nimekuelewa vizuri,,ila kwa hili limeakaaje kama msomi ni yeyote aliyeenda shule,,kwamantiki hiyo basi hata aliyeishia darasa la saba na hakufaulu ni msome,,ila mwalimu wa SUA ni msomi wa taaluma...hapa ikoje,,
 
Msomi/Mwanachuoni ni mjuzi katika fani fulani kimaana na kimatendo na aliyekusanya misingi kumi ya fani husika.

Swali utamjuaje fulani ni msomi ? Hizi ni baadhi ya sifa za msomi yaani mwanachuoni.

1. Msomi hajiiti yeye ni msomi.
2. Msomi lazima awe ameidhinishwa na wasomi ya kuwa fulani ni msomi basi kachukueni elimu toka kwake. Kiistilahi kitendo hiki huitwa "Ijaza/Tazkiya".
3. Msomi lazima awe ameandika vitabu juu ya fani husika.
4. Msomi lazima elimu yake aifundishe yaani awe na wanafunzi, kwani husemwa ya kuwa "ukitaka kumjua msomi basi waangalie wanafunzi wake"
5. Msomi lazima awe amedumu katika fani husika kwa miaka mingi yenye kukidhi haja na kutajika.

Hizi ni baadhi ya sifa za msomi. Salamu hizi ziwafikie wale wajinga wajiitao "Wakili msomi" kisha wamehitimu miaka yao mitano na gamba lao kibindoni kisha akapiga mwaka ule mmoja.

Zingatia : Elimu ni ile unayotembea nayo kifuani mwako na elimu au usomi si wingi wa vyeti kabatini.
 
Msomi/Mwanachuoni ni mjuzi katika fani fulani kimaana na kimatendo na aliyekusanya misingi kumi ya fani husika.

Swali utamjuaje fulani ni msomi ? Hizi ni baadhi ya sifa za msomi yaani mwanachuoni.

1. Msomi hajiiti yeye ni msomi.
2. Msomi lazima awe ameidhinishwa na wasomi ya kuwa fulani ni msomi basi kachukueni elimu toka kwake. Kiistilahi kitendo hiki huitwa "Ijaza/Tazkiya".
3. Msomi lazima awe ameandika vitabu juu ya fani husika.
4. Msomi lazima elimu yake aifundishe yaani awe na wanafunzi, kwani husemwa ya kuwa "ukitaka kumjua msomi basi waangalie wanafunzi wake"
5. Msomi lazima awe amedumu katika fani husika kwa miaka mingi yenye kukidhi haja na kutajika.

Hizi ni baadhi ya sifa za msomi. Salamu hizi ziwafikie wale wajinga wajiitao "Wakili msomi" kisha wamehitimu miaka yao mitano na gamba lao kibindoni kisha akapiga mwaka ule mmoja.

Zingatia : Elimu ni ile unayotembea nayo kifuani mwako na elimu au usomi si wingi wa vyeti kabatini.
Kwahiyo aliye ishia darasa la saba sio msomi
 
Kwahiyo aliye ishia darasa la saba sio msomi
Atakuwa msomi endapo atakuwa na ujuzi wa fani fulani, haijalishi ana cheti au hana.

Usomi una nasibishwa na fani fulani, usomi siyo kujua kusoma tu na kuandika, la hasha ingekuwa hivyo sote sisi tungekuwa wasomi, bali usomi ni kwa fani fulani. Endapo mtu huyo wa darasa la saba akawa amejifunza fani fulani na wasomi wakampitisha kwamba mti huyo ni mjuzi basi tunasema na sisi huyo ni msomi.
 
kaka nimekuelewa,,umedadavua hakika nimekuelewa vizuri,,ila kwa hili limeakaaje kama msomi ni yeyote aliyeenda shule,,kwamantiki hiyo basi hata aliyeishia darasa la saba na hakufaulu ni msome,,ila mwalimu wa SUA ni msomi wa taaluma...hapa ikoje,,
Ngoja niendelee labda utaelewa

Mwenye elimu ni yeyote asiyemjinga katika eneo flani [yaani uelewa/ufahamu juu ya matumizi n.k ya kitu ama jambo flani] elimu si lazima itolewe darasani ndiyo maana kuna kitu kinaitwa elimu dunia,hivyo mtu akikuita mjinga kabla hujakasirika furahia ila umuulize mimi mjinga eneo gani?​

Kwa kuwa nimekwambia mtu kuwa mjinga ni hali ya kutokuwa na uelewa/ufahamu wa jambo ama kitu flani.2 MSOMI NI MTU MWENYE UJUZI/TAALUMA FLAN I juu ya jambo flani,kwa maana nyingine huwezi kuitwa msomi kama hujabobea katika tasnia husika,inaweza ikawa katika mambo ya siasa,uhandisi,kilimo,sayansi,dini n.k,ndiyo maana makazini watu huajiliwa kwa utalamu wao[yaani taaluma zao]​

Ngoja niseme hivi ili uelewe zaidi,wasomi wako kwa ajiri ya kutatua matatizo kwa kuwa wamebobea katika maeneo husika mfano madaktari..ndiyo maana wakati flani unaweza kusikia tuna uhaba wa wataalamu,wenye elimu ni wengi kuliko wataalamu,NAOMBA NIMALIZE HIVI,MTU ANAWEZA KUWA NA UELEWA WA SHERIA LAKINI ASIITWE MWANASHERIA...​

UMENIELEWA MPENDWA? Haya nikupe na huu mfano wa mwisho,kama ukiwa hujui kutumia kompyuta kwa lugha nyepesi niseme wewe ni mjinga katika eneo hilo la matumizi ya kompyuta,lakini ukipata maelekezo ya matumizi yake hautaitwa tena mjinga ila utaitwa una una ufahamu yaani elimu ya kompyuta lakini kamwe hauwezi kuitwa MTALAAMU WA KOMPYUTA.​

Namaliza kwa mnyumbuisho wa maneno yafuatayo. 1.ELIMU-elimika-elimisha-elimishwa. 2.SOMO-soma- someka- someshwa-somea- USOMI- MSOMI. 3.TAALAMU-taluma-mtalam.​

 
Atakuwa msomi endapo atakuwa na ujuzi wa fani fulani, haijalishi ana cheti au hana.

Usomi una nasibishwa na fani fulani, usomi siyo kujua kusoma tu na kuandika, la hasha ingekuwa hivyo sote sisi tungekuwa wasomi, bali usomi ni kwa fani fulani. Endapo mtu huyo wa darasa la saba akawa amejifunza fani fulani na wasomi wakampitisha kwamba mti huyo ni mjuzi basi tunasema na sisi huyo ni msomi.
kama sdijakuelewa vile,,,kwani kamusi inasemaje.....na mnukuu mchangia hapo juuu alitoa viashiria vya neno msomi,,,,,
msomi , pl wasomi { English: intellectual }
noun

msomi , pl wasomi { English: learned person , pl learned people }
noun

msomi , pl wasomi { English: lecturer , pl lecturers } [derived: soma V]
noun

msomi , pl wasomi { English: reader } [derived: soma V]
noun ,

msomi , pl wasomi { English: scholar , pl scholars } [derived: Swahili -soma]
noun

5 distinct results returned (chanzo:THE KAMUSI PROJECT)
 
Ngoja niendelee labda utaelewa

Mwenye elimu ni yeyote asiyemjinga katika eneo flani [yaani uelewa/ufahamu juu ya matumizi n.k ya kitu ama jambo flani] elimu si lazima itolewe darasani ndiyo maana kuna kitu kinaitwa elimu dunia,hivyo mtu akikuita mjinga kabla hujakasirika furahia ila umuulize mimi mjinga eneo gani?​

Kwa kuwa nimekwambia mtu kuwa mjinga ni hali ya kutokuwa na uelewa/ufahamu wa jambo ama kitu flani.2 MSOMI NI MTU MWENYE UJUZI/TAALUMA FLAN I juu ya jambo flani,kwa maana nyingine huwezi kuitwa msomi kama hujabobea katika tasnia husika,inaweza ikawa katika mambo ya siasa,uhandisi,kilimo,sayansi,dini n.k,ndiyo maana makazini watu huajiliwa kwa utalamu wao[yaani taaluma zao]​

Ngoja niseme hivi ili uelewe zaidi,wasomi wako kwa ajiri ya kutatua matatizo kwa kuwa wamebobea katika maeneo husika mfano madaktari..ndiyo maana wakati flani unaweza kusikia tuna uhaba wa wataalamu,wenye elimu ni wengi kuliko wataalamu,NAOMBA NIMALIZE HIVI,MTU ANAWEZA KUWA NA UELEWA WA SHERIA LAKINI ASIITWE MWANASHERIA...​

UMENIELEWA MPENDWA? Haya nikupe na huu mfano wa mwisho,kama ukiwa hujui kutumia kompyuta kwa lugha nyepesi niseme wewe ni mjinga katika eneo hilo la matumizi ya kompyuta,lakini ukipata maelekezo ya matumizi yake hautaitwa tena mjinga ila utaitwa una una ufahamu yaani elimu ya kompyuta lakini kamwe hauwezi kuitwa MTALAAMU WA KOMPYUTA.​

Namaliza kwa mnyumbuisho wa maneno yafuatayo. 1.ELIMU-elimika-elimisha-elimishwa. 2.SOMO-soma- someka- someshwa-somea- USOMI- MSOMI. 3.TAALAMU-taluma-mKwahiyo​


Ngoja niendelee labda utaelewa

Mwenye elimu ni yeyote asiyemjinga katika eneo flani [yaani uelewa/ufahamu juu ya matumizi n.k ya kitu ama jambo flani] elimu si lazima itolewe darasani ndiyo maana kuna kitu kinaitwa elimu dunia,hivyo mtu akikuita mjinga kabla hujakasirika furahia ila umuulize mimi mjinga eneo gani?​

Kwa kuwa nimekwambia mtu kuwa mjinga ni hali ya kutokuwa na uelewa/ufahamu wa jambo ama kitu flani.2 MSOMI NI MTU MWENYE UJUZI/TAALUMA FLAN I juu ya jambo flani,kwa maana nyingine huwezi kuitwa msomi kama hujabobea katika tasnia husika,inaweza ikawa katika mambo ya siasa,uhandisi,kilimo,sayansi,dini n.k,ndiyo maana makazini watu huajiliwa kwa utalamu wao[yaani taaluma zao]​

Ngoja niseme hivi ili uelewe zaidi,wasomi wako kwa ajiri ya kutatua matatizo kwa kuwa wamebobea katika maeneo husika mfano madaktari..ndiyo maana wakati flani unaweza kusikia tuna uhaba wa wataalamu,wenye elimu ni wengi kuliko wataalamu,NAOMBA NIMALIZE HIVI,MTU ANAWEZA KUWA NA UELEWA WA SHERIA LAKINI ASIITWE MWANASHERIA...​

UMENIELEWA MPENDWA? Haya nikupe na huu mfano wa mwisho,kama ukiwa hujui kutumia kompyuta kwa lugha nyepesi niseme wewe ni mjinga katika eneo hilo la matumizi ya kompyuta,lakini ukipata maelekezo ya matumizi yake hautaitwa tena mjinga ila utaitwa una una ufahamu yaani elimu ya kompyuta lakini kamwe hauwezi kuitwa MTALAAMU WA KOMPYUTA.​

Namaliza kwa mnyumbuisho wa maneno yafuatayo. 1.ELIMU-elimika-elimisha-elimishwa. 2.SOMO-soma- someka- someshwa-somea- USOMI- MSOMI. 3.TAALAMU-taluma-mtalam.​

Kwahiyo kama utaenda darasani ukawa hukupata taaluma wewe sio msomi.
 
kama sdijakuelewa vile,,,kwani kamusi inasemaje.....na mnukuu mchangia hapo juuu alitoa viashiria vya neno msomi,,,,,
msomi , pl wasomi { English: intellectual }
noun

msomi , pl wasomi { English: learned person , pl learned people }
noun

msomi , pl wasomi { English: lecturer , pl lecturers } [derived: soma V]
noun

msomi , pl wasomi { English: reader } [derived: soma V]
noun ,

msomi , pl wasomi { English: scholar , pl scholars } [derived: Swahili -soma]
noun

5 distinct results returned (chanzo:THE KAMUSI PROJECT)
Ulichoandika hapa umeonyesha udhaifu wa kamusi katika kutoa maana. Huwezi kumjua msomi kama hujamnasibisha na fani fulani, aidha fundi, mwalimu, mwanashera au mfano wake. Kwai fundi gereji hasomi ? Lazima afundishwe ndiyo kazi aijue huenda akafundishwa darasani au sehemu ya kazi husika (site).

Au unafikiri kusoma mpaka ukae darasani kwenye madawati na mfungiwe Projector,au uvae joho na mfano wake ? Kuwaza kwa mtindo huu ni kuwaza kitoto mno. Kwa sababu historia inatunukulia wasomi na wanao rejewa katika fani mbali mbali hawakuwa na shahada, wala stashahada, wala shahada ya uzamili wala uzamivu. Mfano wa harakaharaka ni Shabaani Robert nakumbuka kama sijakosea aliishia darasa la nne (Mtanisahihisha hapa), lakini tunaambiwa yeye ndiyo baba wa Fasihi ya Kiswahili, na hawa wako wengi sana mpaka kwenye Sayansi,Falsafa na fani nyingine.
 
Ulichoandika hapa umeonyesha udhaifu wa kamusi katika kutoa maana. Huwezi kumjua msomi kama hujamnasibisha na fani fulani, aidha fundi, mwalimu, mwanashera au mfano wake. Kwai fundi gereji hasomi ? Lazima afundishwe ndiyo kazi aijue huenda akafundishwa darasani au sehemu ya kazi husika (site).

Au unafikiri kusoma mpaka ukae darasani kwenye madawati na mfungiwe Projector,au uvae joho na mfano wake ? Kuwaza kwa mtindo huu ni kuwaza kitoto mno. Kwa sababu historia inatunukulia wasomi na wanao rejewa katika fani mbali mbali hawakuwa na shahada, wala stashahada, wala shahada ya uzamili wala uzamivu. Mfano wa harakaharaka ni Shabaani Robert nakumbuka kama sijakosea aliishia darasa la nne (Mtanisahihisha hapa), lakini tunaambiwa yeye ndiyo baba wa Fasihi ya Kiswahili, na hawa wako wengi sana mpaka kwenye Sayansi,Falsafa na fani nyingine.
Enyi wasomi mlioko juu kama nyota, nani anayeingia mikataba ya kilaghai inayohatarisha rasilimali za nchi yetu kama siyo nyie?
 
Back
Top Bottom