Msambichaka Mkinga
JF-Expert Member
- Oct 22, 2015
- 1,646
- 2,911
Wewe ni big O, unasoma lakini huelewi unachosoma. Marekebisho ya katiba ya Zanzibar yamejenga takwa la kikatiba kuwa kwaajili ya utengamano wa watu wa Zanzibar, chama chochote kinachoshinda kitaunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa.Huyu mwanasheria anayedai matokeo hayajakidhi matakwa ya kikatiba hivyo unapaswa kurejewa ni jipu lililooza inabidi atumbuliwe mapema! Ni aibu kwa mwanasheria kudai hivyo!
Ukweli ni kwamba matokeo hayajakidhi kuundwa kwa serikali ya UMOJA wa kitaifa! Kwa hiyo itaundwa serikali ya chama kimoja!
Mantiki ya serikali ya UMOJA wa kitaifa ni matokeo ya uchaguzi kutokutofautiana kwa kiasi kikubwa. Lakini kwa matokeo ambayo mgombea mmoja amezoa zaidi ya asilimia 90 katiba iliona hakuna mantiki ya kuunda serikali ya UMOJA wa kitaifa! Ndiyo maana katiba haisemi katika mazingira hayo serikali ya UMOJA wa kitaifa itaundwaje, maana haipaswi kuundwa katika mazingira hayo!
Ndiyo maana Hamad Rashid ameangukia pua!
Kama Shein akichagua Makamu wa kwanza wa rais katika mazingira haya, atakuwa amevunja katiba na baraza la wawakilishi wanaweza kumwajibisha!
Kisha katiba hiyo ikatengeneza scenario ya uundwaji wa serikali hiyo. Moja ni pale kuna mgombea wa Urais zaidi ya mmoja, na ya pili ni pale ambapo kuna mgombea mmoja tu.
Takwa hili la kikatiba ndiyo lililoilazimisha CCM kutokukubali kuwaondoa wagombea wote ambao walisema wamejitoa. Na pia wakaweka tahadhari nyingine ambayo ilikuwa ni kuwabembeleza wanasiasa tumbo kutangaza kuwa wao watashiriki.
Vyovyote watakavyofanya, CCM imeitia aibu kubwa Tanzania, Zanzibar na watu wote wa Taifa hili. Dr. Shein mtu aliyeonekana muungwana ameingia kwenye rekodi mbaya ya tamaa ya madaraka. To hell CCM.