Msiwalaumu na kuwadhihaki wanaoondoka CHADEMA

Msiwalaumu na kuwadhihaki wanaoondoka CHADEMA

Smile Digital Stationery

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2024
Posts
202
Reaction score
317
Mimi sio mtu wa siasa, sina chama chochote ispokuwa mimi ni mfuatiliaji wa hoja zote, pale napoona anayeongea na kufanya mazuri namfurahia na kumwombea afanye zaidi, na anayefanya mabaya namchukia na kumwombea abadilike awe mwema.

Kwa muda mrefu nimeona na kusoma malumbano ya hoja mbali mbali za wanasiasa, kiukweli mimi yeyote anayeitwa Mwanasiasa simchukulii kama Suluhisho, bali namchukulia kama mtafutaji na kachagua hiyo ndio njia yake ya riziki na haijalishi ni wa chama gani.

Kwa siku za hivi karibuni nimewaona wanasiasa wa Chama cha Chadema wakifarakana na yote hyo ilianzia pale kwenye kubadilisha Kiongozi wao Mkuu (Mwenyekiti) wa chama, kiukweli mimi haya yanayotokea nilishajua kuwa yatatokea, maana ulikuwa ni uchaguzi ambao wagombea walitumia silaha kali za kutoleana na kukosoana bila kuangaliana usoni, kiuhalisia wakati mshindi anapatikana kwa mwenye jicho la saikolojia ya kumsoma mtu, yule kiongozi wa mwanzo baada ya matokeo walikumbatiana ila yule aliyeshindwa hakuwa ni mwenye kukubali 100% na matokeo yake ndio kama haya yanayoonekana, kwamba wale walikuwa wanamsaport kuondoka kwenye chama baada ya Uongozi wa sasa kuja na agenda yao ya "No reform No Election".

Mnadhani kuwa KUBWA LA MAADUI NI NANI?, Unaweza kujiuliza, ni kwanini hawakuondoka awali na badala yake wamesubiri hadi Baadhi ya Viongozi kuwa kwenye matatizo?

Jibu linabaki palepale kwenye mawazo yangu kuwa, "Wanasiasa sio watetezi wetu wenye kutatua changamoto zetu bali ni watafutaji wa riziki". Wale walioondoka wameondoka maana wameona huku hakuna ulaji tena, hawawez kukaa sehemu ambayo haina ulaji, hvyo wameenda wanapokwenda kwa lengo la kuja kugombea na kuja kuwadanganyeni kwenye kampeni muwape ulaji.

Na kubwa zaidi turudi kwa nyie wananchi na wanachama wa chadema, wale watu wanaoondoka kwenye chama miongoni mwao wana majeraha, na historia ya kuteseka wakidai waliteseka kwaajili yenu, (ijapokuwa ni kwaajili yao pia), Ila je, Mliwasaport kwa kiasi gani kipindi walipokuwa wanaumia kwaajili yenu?,

Walipokuwa wanaitisha maandamano ili kuishurutisha Serikali kuwasikiliza na kufanyia kazi malalamiko yao, mlikuwa mnawaonyesha kwenye social medias kuwa mpo nao pamoja, ila siku husika za maandamano MBONA MLIWAACHA WAO WENYEWE WAPIGWE NA KUUMIZWA?.

Namalizia kwa kusema, MSIWADHIHAKI WANAOONDOKA MAANA HAMKUWASAPORT PINDI WALIPOKUWEPO.
 
Kama Kuna MTU Kahama, alafu akahama na Wafuasi, ajitokeze mbele !!.


CHADEMA Kwa nyomi lake hili, bado Kuna MTU anawawazia G 55??.



Mabadiliko ya Sasa ni ya Wananchi wenyewe, hamna MTU anayeweza badilisha Hilo.
 
Leo nimemskia Lema kwenye moja ya mikutano anasema yupo kwenye siasa kuwasaidia watanzania wanyonge.

Aliendelea kusema kama angeacha siasa akaingia kwenye biashara ndani ya miaka 10 atakuwa na pesa kumzidi MO.

I told my self wow!! Nampa hongera saana kama ayasemayo yanatoka moyoni mwake.
 
Mbona
Mimi sio mtu wa siasa, sina chama chochote ispokuwa mimi ni mfuatiliaji wa hoja zote, pale napoona anayeongea na kufanya mazuri namfurahia na kumwombea afanye zaidi, na anayefanya mabaya namchukia na kumwombea abadilike awe mwema.

Kwa muda mrefu nimeona na kusoma malumbano ya hoja mbali mbali za wanasiasa, kiukweli mimi yeyote anayeitwa Mwanasiasa simchukulii kama Suluhisho, bali namchukulia kama mtafutaji na kachagua hiyo ndio njia yake ya riziki na haijalishi ni wa chama gani.

Kwa siku za hivi karibuni nimewaona wanasiasa wa Chama cha Chadema wakifarakana na yote hyo ilianzia pale kwenye kubadilisha Kiongozi wao Mkuu (Mwenyekiti) wa chama, kiukweli mimi haya yanayotokea nilishajua kuwa yatatokea, maana ulikuwa ni uchaguzi ambao wagombea walitumia silaha kali za kutoleana na kukosoana bila kuangaliana usoni, kiuhalisia wakati mshindi anapatikana kwa mwenye jicho la saikolojia ya kumsoma mtu, yule kiongozi wa mwanzo baada ya matokeo walikumbatiana ila yule aliyeshindwa hakuwa ni mwenye kukubali 100% na matokeo yake ndio kama haya yanayoonekana, kwamba wale walikuwa wanamsaport kuondoka kwenye chama baada ya Uongozi wa sasa kuja na agenda yao ya "No reform No Election".
Mnadhani kuwa KUBWA LA MAADUI NI NANI?, Unaweza kujiuliza, ni kwanini hawakuondoka awali na badala yake wamesubiri hadi Baadhi ya Viongozi kuwa kwenye matatizo?
Jibu linabaki palepale kwenye mawazo yangu kuwa, "Wanasiasa sio watetezi wetu wenye kutatua changamoto zetu bali ni watafutaji wa riziki". Wale walioondoka wameondoka maana wameona huku hakuna ulaji tena, hawawez kukaa sehemu ambayo haina ulaji, hvyo wameenda wanapokwenda kwa lengo la kuja kugombea na kuja kuwadanganyeni kwenye kampeni muwape ulaji.

Na kubwa zaidi turudi kwa nyie wananchi na wanachama wa chadema, wale watu wanaoondoka kwenye chama miongoni mwao wana majeraha, na historia ya kuteseka wakidai waliteseka kwaajili yenu, (ijapokuwa ni kwaajili yao pia), Ila je, Mliwasaport kwa kiasi gani kipindi walipokuwa wanaumia kwaajili yenu?, walipokuwa wanaitisha maandamano ili kuishurutisha Serikali kuwasikiliza na kufanyia kazi malalamiko yao, mlikuwa mnawaonyesha kwenye social medias kuwa mpo nao pamoja, ila siku husika za maandamano MBONA MLIWAACHA WAO WENYEWE WAPIGWE NA KUUMIZWA?.
Namalizia kwa kusema, MSIWADHIHAKI WANAOONDOKA MAANA HAMKUWASAPORT PINDI WALIPOKUWEPO.
lowassa aliondoka na kundi au mafuriko kwend CCM lakini Chadema bado ipi. Kwangu mimi hali hii inakiimarisha chama chini ya mikono ya wananchi.
 
Mbona

lowassa aliondoka na kundi au mafuriko kwend CCM lakini Chadema bado ipi. Kwangu mimi hali hii inakiimarisha chama chini ya mikono ya wananchi.
Hao wananchi wenyewe ni wanafiki mno, isingekuwa kwamba wale wanaowapambania nao wanapata pesa kupitia maumivu hayo, wasingeendelea kuteseka kwaajili ya watu wasiowathamini.
 
Leo nimemskia Lema kwenye moja ya mikutano anasema yupo kwenye siasa kuwasaidia watanzania wanyonge.

Aliendelea kusema kama angeacha siasa akaingia kwenye biashara ndani ya miaka 10 atakuwa na pesa kumzidi MO.

I told my self wow!! Nampa hongera saana kama ayasemayo yanatoka moyoni mwake.
Sidhani kwamba kuna ukweli kwa asilimia mia moja, huezi kuteseka, kuumizwa, kufungwa, kutishiwa hadi uhai kwa kitu ambacho unaowapambania wao wanawacheka pindi mnapoteseka na kubaki ku comment tuu kwenye mitandao ila wakiwaambia watoke front hawaonekani.
 
Mbona

lowassa aliondoka na kundi au mafuriko kwend CCM lakini Chadema bado ipi. Kwangu mimi hali hii inakiimarisha chama chini ya mikono ya wananchi.
Na walioondoka na Lowasa ni walewale alokuja nao. Kama waliongezeka ni kidogo. Kwa ufupi Wanasiasa ni wachumia tumbo, siku zote wanakaa kule ambapo wanapata maslahi
 
Kama Kuna MTU Kahama, alafu akahama na Wafuasi, ajitokeze mbele !!.


CHADEMA Kwa nyomi lake hili, bado Kuna MTU anawawazia G 55??.



Mabadiliko ya Sasa ni ya Wananchi wenyewe, hamna MTU anayeweza badilisha Hilo.
Sidhani kama watakuwa wameondoka na wafuasi, na huenda hata kama mtaambiwa kuna wafuasi wa chadema sehemu fulani wamehama chama utakuwa ni wafuasi wa ccm ndo wamakusanywa na kuambiwa watengeneze propaganda. Ila swali linabaki kwamba, wakiondoka hao G55 wote na wakabaki hao mnaowaita Wazalendo wa chama, je mtawasaport ktk agenda zao na watakapowaita kwenda kupaza sauti (maandamano) mtaenda???
 
Sidhani kwamba kuna ukweli kwa asilimia mia moja, huezi kuteseka, kuumizwa, kufungwa, kutishiwa hadi uhai kwa kitu ambacho unaowapambania wao wanawacheka pindi mnapoteseka na kubaki ku comment tuu kwenye mitandao ila wakiwaambia watoke front hawaonekani.
Hiyo ndio kazi wanayopewaga Manabii ya kupitia mateso Nabii Lema yuko kwenye njia hiyo ya kuwakomboa Watu wasiokuwa na sauti.
 
Leo nimemskia Lema kwenye moja ya mikutano anasema yupo kwenye siasa kuwasaidia watanzania wanyonge.

Aliendelea kusema kama angeacha siasa akaingia kwenye biashara ndani ya miaka 10 atakuwa na pesa kumzidi MO.

I told my self wow!! Nampa hongera saana kama ayasemayo yanatoka moyoni mwake.
Porojo tu hizo.
Hao wanyonge aliowasaidia wako wapi?
Kwenye biashara amewahi kuwamo, alikuwa mwizi wa magari, mbona hakupata hiyo pesa ya kumzidi Mo?
 
Back
Top Bottom