Msimu wa korosho umewadia, mizani na mawe feki katika vyama vya msingi kwa ajili ya kuwaibia wakulima bado ni tatizo kubwa

Nascoba

JF-Expert Member
Mar 16, 2012
310
160
Naomba sana ujumbe huu uwafikie wahusika.

Miongoni mwa njia wanazotumia viongozi wa vyama vya msingi kujitajirisha kwa kuwaibia wakulima ni kuwa na mawe ya mzani yanayoiba.

Tatizo hili ni kubwa kuliko inavyodhaniwa lakini halijaguswa wala kuzungumzwa. Na mwaka huu hali imekuwa mbaya zaidi.
Mfano katika kijiji cha Chitowe kilichopo Nanyumbu, Masasi kati ya kilo 1200 ambazo nilishazipima, kiasi cha kilo 70 zimepungua na hali hiyo ni kwa kila mtu anayekwenda kupima anakutana nayo.

Ajabu ni kwamba, jambo hili linafahamika miaka nenda rudi lakini hakuna hatua zozote stahiki zinazochukuliwa. Au labda ni mpango wa upigaji unaofadhiliwa na wakubwa?

Hebu Waziri na Naibu Waziri fanyeni jambo kunusuru hali hii wakulima wanaumia sana.
 
Hapo chini malizia "wakulima tunaumia sana". Pia hao wanaojiita wadau wa korosho waharakishe minada ya korosho ianze haraka sana. Mpaka sasa haieleweki minada hiyo itaanza lini na wakulima tumeshavuna korosho zetu na tayari tumeshazipeleka magulioni huko tunasubiri ziuzwe tu. Halafu isitoshe msumu wa mavuno unaenda ukingoni sasa.
 
Hapo chini malizia "wakulima tunaumia sana". Pia hao wanaojiita wadau wa korosho waharakishe minada ya korosho ianze haraka sana. Mpaka sasa haieleweki minada hiyo itaanza lini na wakulima tumeshavuna korosho zetu na tayari tumeshazipeleka magulioni huko tunasubiri ziuzwe tu. Halafu isitoshe msumu wa mavuno unaenda ukingoni sasa.

Kweli kabisa kaka mkubwa
 
Bora huko kwenu mmeshapeleka maghalani, huku kwetu Ruangwa sehem nyingi maghala bado hayajafunguliwa, korosho zipo ndani tu, Na waliko fungua vitendea kazi Ni vichache kama magunio na vitabu.
Hapo chini malizia "wakulima tunaumia sana". Pia hao wanaojiita wadau wa korosho waharakishe minada ya korosho ianze haraka sana. Mpaka sasa haieleweki minada hiyo itaanza lini na wakulima tumeshavuna korosho zetu na tayari tumeshazipeleka magulioni huko tunasubiri ziuzwe tu. Halafu isitoshe msumu wa mavuno unaenda ukingoni sasa.
 
Naomba sana ujumbe huu uwafikie wahusika.

Miongoni mwa njia wanazotumia viongozi wa vyama vya msingi kujitajirisha kwa kuwaibia wakulima ni kuwa na mawe ya mzani yanayoiba.

Tatizo hili ni kubwa kuliko inavyodhaniwa lakini halijaguswa wala kuzungumzwa. Na mwaka huu hali imekuwa mbaya zaidi.
Mfano katika kijiji cha Chitowe kilichopo Nanyumbu, Masasi kati ya kilo 1200 ambazo nilishazipima, kiasi cha kilo 70 zimepungua na hali hiyo ni kwa kila mtu anayekwenda kupima anakutana nayo.

Ajabu ni kwamba, jambo hili linafahamika miaka nenda rudi lakini hakuna hatua zozote stahiki zinazochukuliwa. Au labda ni mpango wa upigaji unaofadhiliwa na wakubwa?

Hebu Waziri na Naibu Waziri fanyeni jambo kunusuru hali hii wakulima wanaumia sana.

Toa taarifa idara ya mizani kuhusu wizi huo, ofisi zao ziko Mtwara mjini nyuma ya bank ya NBC.
 
Back
Top Bottom