Msimamo wa Zitto Kabwe kuhusu Katiba mpya

Msimamo wa Zitto Kabwe kuhusu Katiba mpya

na mtaumwa sana ugonjwa uitwao Zittophobiasis. Ukweli ni kwamba Zitto yuko very smart. ndo maana kila siku mko bize humu kumtaja mara kumi kumi kuliko mnavyowataja waume zenu au wake.
Hoja ya Zitto iko very clear hapo ni kwamba anataka katiba ya Warioba ndo ijadiliwe ndo maana anabainisha wazi kuwa hataingia bungeni kama katiba ya lumumba itaendelea kujadiliwa. na mtahangaika sana mataahita nyie.


Msimamo upi sasa hapo kwamba Zitto ni Popo maana yuko kote kote ......Zitto ni historia

Mara anasema yeye sio UKAWA mara ataingia na na UKAWA kutohudhuria Bunge , aeleweke vipi huyu Popo ?

Ngoja msukule wake mwl.kaijage uje

anaposema anapenda ijadiliwe rasimu ya warioba maana yake naye ni UKAWA. Aache kuendeleza siasa zake za KINAFIKI na KINDUMILA KUWILI.Anatamani kula kote kote.Is opportunistic

huyu jamaa anakuwaga na kauli mbilimbili haswa anaporopoka jambo, akiona upepo unamwendea vibaya anarudi na kauli nyingine

Ni aibu sana kwa kijana kama ZZK kushiriki ktk harakati za kuangamiza Vyama Vya Upinzani Tanzania kwa lengo LA kukibakisha CCM madarakani iendelee kutawala kiimla ktk nchi yetu

Huyu jamaa anaizihilishia jamii ya kitanzania kwamba yeye ni msaliti mkubwa ana upande na anaonekana ana ajenda ya siri na Ccm na hii ina onyesha kwamba wapinzani jamani wanacho pigania kwa wananchi wa TZ ni haki Zitto mwenyewe ana kubali lakini asemi duuuh wana JF mnajua ni aibu Kubwa sana kwa huyu kija ameonyesha dhahili shahili kwamba ana njaa yakufamtu eee Mwenyezi Mungu humuremu madhambi yake Amen!!!!

ZZK ni kigeugeu
 
Kimsingi anakubaliana na Madai ya UKAWA.
Hiki ndio cha msingi ambacho Mpaka huyu mnafik anakubaliana nacho...
Exactly. anakubaliana na ukawa na wazo la kutorudi bungeni kama rasimu ya Warioba haitojadiliwa lakini amekiri kuwa yeye sio Ukawa.
Kuwa na wazo linalofanana na Ukawa haimaanishi kuwa wewe ni ukawa.
 
MSIMAMO WA NDUGU ZITTO KABWE KUHUSU MCHAKATO WA KUANDIKA KATIBA MPYA

Jana tarehe 29 Julai, 2014 nimefanya mahojiano katika kipindi cha PowerBreakFast kinachorushwa na Clouds FM. Baadhi ya vyombo vya habari vimeandika mahojiano yale. Napenda nitoe ufafanuzi kidogo kuhusu msimamo wangu kuhusu mchakato wa Katiba.

Kwanza, Mimi sijawahi kuwa UKAWA wala kundi lolote lile katika Bunge Maalumu la Katiba isipokuwa kundi linalotaka maridhiano. Msimamo wangu kuhusu Muungano ni Serikali Tatu Zilizoboreshwa (S3z) ili kuwa na Muungano imara usio tegemezi wala egemezi kwa Washirika wake.

Pili, Mimi niliunga mkono ‘protest’ ya baadhi ya Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kupinga lugha za matusi na lugha za kibaguzi zilizokuwa zinaendelea ndani ya mkutano ule. Vilevile niliunga mkono kwamba Rasimu inayopaswa kujadiliwa ni Rasimu iliyotokana na Tume ya Marekebisho ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Sinde Warioba. Nasisitiza umuhimu wa kupata Katiba BORA itakayoimarisha DOLA ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Tatu, kwa hali ya sasa kuna mkwamo katika kupatikana kwa Katiba Bora. Mkwamo unaotokana na kutokuwepo kwa nia ya dhati ya kupata maridhiano ya pande zinazopingana. UKAWA hawataki mazungumzo na Viongozi wa Bunge la Katiba badala ya kujenga maridhiano kila siku wanawabeza UKAWA jambo ambalo kamwe haliwezi kujenga mwafaka. Ushauri wangu ni kuahirisha mchakato mzima wa kuandika Katiba mpaka mwaka 2016 baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015. Katiba ya sasa ifanyiwe marekebisho machache kama ifuatavyo;

i) Tume ya Uchaguzi ili iwe huru na ionekane kuwa huru, ikiwemo kuwaondoa watumishi wa Halmashauri za Wilaya, Miji na Majiji katika kusimamia uchaguzi

ii) Kuruhusu mgombea binafsi

iii) Kuondoa Mafuta na Gesi kama Jambo la Muungano ili Zanzibar ianze mara moja kusimamia kwa uhuru utafutaji wa Mafuta katika vitalu vilivyopo upande huo wa Muungano

Mkutano wa Bunge Maalumu utakaofanyika bila kuwepo kwa maridhiano utakuwa hauna maana yeyote na itakuwa ni sawa na kupoteza muda na fedha za walipa kodi ambazo zingeweza kununua madawa vijijini. Mimi binafsi sitahudhuria mkutano wa Bunge Maalumu kama makundi hasimu hayatakuwa yamefikia maridhiano.

Kabwe Zitto, MB/MBMK
Tangu lini mbunge wa mahakama akawa na upande.Mahakama haina upande
 
wakuu kuna wengi humu wana ugonjwa uitwao Zittophobiasis. Ukweli ni kwamba Zitto yuko very smart. ndo maana kila siku wako bize humu kumtaja mara kumi kumi kuliko wanavyowataja waume zao au wake.
Hoja ya Zitto iko very clear hapo ni kwamba anataka katiba ya Warioba ndo ijadiliwe ndo maana anabainisha wazi kuwa hataingia bungeni kama katiba ya lumumba itaendelea kujadiliwa. na watahangaika sana mataahita haya. wala msipoteze muda nayo.


Hapana jamani. Deus Kibamba na yeye amependekeza ijadiliwe rasimu ya Warioba inamaana na yeye Deus ni UKAWA?

Mbona tunakuwa biased jamani!!

ndibalema unapomchukia mtu unamchukia na.lolote lile

alichokionyesha hapo huyo HAKISAWA ni aina ya raia tulio nao, gullible,stupid etc

kwa kauli ya zitto i would think yy ni Ukawa na hayuko against nao

analalamika ukawa kusemwa vibaya

anashauri bunge livunjwe


SIJAONA TATIZO LA KAULI YA ZITTO Hapo

Ndibalema ndio tulipofika hapa na hawa watanzania wenzetu....

sijui tuombe
 
Sio kila aliyebakia ndani anaunga Mkono serikali mbili. Kuna wazanzibari wengi pia watatoka tu baada ya bunge kuanza. Wapo kimya Vila wanamisimamo yao....
 
ndibalema unapomchukia mtu unamchukia na.lolote lile

alichokionyesha hapo huyo HAKISAWA ni aina ya raia tulio nao, gullible,stupid etc

kwa kauli ya zitto i would think yy ni Ukawa na hayuko against nao

analalamika ukawa kusemwa vibaya

anashauri bunge livunjwe


SIJAONA TATIZO LA KAULI YA ZITTO Hapo

Ndibalema ndio tulipofika hapa na hawa watanzania wenzetu....

sijui tuombe

..mbona naona kama Zitto yuko kivyake-vyake?

..hata anapotaja Ukawa anawataja kama "wale" na siyo "sisi."

..kwa mfano anasema "viongozi wa Bunge la Katiba wanawabeza Ukawa..." badala ya kusema "viongozi wa Bunge la Katiba wanatubeza sisi tulioko Ukawa..."

..sasa hii inatoka kwenye written statement ya Zitto ambapo alikuwa na muda wa kutafakari maana ya kile alichoandika.

..pia Ukawa wamefanya mikutano kadhaa mikoani na sidhani kama Zitto amewahi kushiriki mkutano wowote ule.

cc Ndibalema, Haki sawa
 
Last edited by a moderator:
Hayo ni maoni yake na familia yake.
Msukule mkubwa huyu,ukawa inamhusu nini,akomae na act mtt wa ccm
 
Zitto Ni vigumu kuamini kwamba hafahamu kuwa kinachojadiliwa bungeni ni kitu mchepuko badala ya rasimu ya katiba iliyoratibiwa kitaalamu.

Siamini haoni kwamba bunge hilo linalengo la kupitisha katiba ya ccm kwa kigezo cha wingi wao.

Inashangaza hatoi tamko kuhusu mwenendo wa bunge hilo kwamba hakuna democrasia wala ustaarabu wa kawaida.

Inaonekana ajabu haja comment uharabu wa kikwete alioufanya wa kuasisi uharamia katika matengenezo ya katiba mpya ya wananchi.

Ni mtu wa ajabu asiyeona unyanyasaji na hila zinazofanywa na ccm katika bunge hilo.

La ajabu, anaongea unafiki bila kugusia hoja za ukawa as if hafahamu kwamba wanahitaji kujadili rasimu ya tume na si ya ccm. Mbona hilo halisemi?

Wanafiki na wenye hile mwisho wao ni fedheha.
 
Zitto, alikuwa zamani huyu wa leo ni kama chui wa karatasi tu...........hana madhara hata kidogo....


Haki sawa nadhani hiyo ingekuwa news kama angesema ana imani na UKAWA lakini kwamba hana imani nayo... hiyo siyo news kutoka kwa yeye msaliti namba 1.
 
kumbe ndo zito alivyoishiwa hivi, kweli siasa na unafiki ni noma!
 
MNYONGE Mnyongeni Haki Yake Mpeni Binafsi Kunasehemu Nyingi Simuelewagi Zzk Lakn Kwa Hapa Sijaona Kosa Lake
Nawaombeni Wanajamvi Tusiangalie Maneno Yametoka Kwa Nani Bali YanasemaJE?
 
Zito hana uwezo wa kupambana na mafisadi, yeye ni sawa na mbwa asiye na meno. Ajiendee zake tu huko kwa wafuasi wenzake act kisha waendelee kupokea rushwa toka ccm.
 
..mbona naona kama Zitto yuko kivyake-vyake?

..hata anapotaja Ukawa anawataja kama "wale" na siyo "sisi."

..kwa mfano anasema "viongozi wa Bunge la Katiba wanawabeza Ukawa..." badala ya kusema "viongozi wa Bunge la Katiba wanatubeza sisi tulioko Ukawa..."

..sasa hii inatoka kwenye written statement ya Zitto ambapo alikuwa na muda wa kutafakari maana ya kile alichoandika.

..pia Ukawa wamefanya mikutano kadhaa mikoani na sidhani kama Zitto amewahi kushiriki mkutano wowote ule.

cc Ndibalema, Haki sawa
Mkuu naona kama hujaelewa.
Ni kwamba Zitto ameshaweka wazi kuwa yeye hajawahi na hatokuwa Ukawa so usishangae akiji'exclude kwenye ukawa.
Ndio maana kauli zake unaona zipo kinyume na ukawa.
 
Zitto hana jipya na hii ni political game wanataka wapite uchaguzi kilain na zitto analiongelea kana kwamba halengi uchaguzi huu mkuu but anajua UKAWA ni kikwazo
 
Back
Top Bottom