We acha tu, kasababisha nichelewe kunywa chai, uchumi wa nchi anaujua vizuri, juzi nilimsikiliza Mbatia yaani alikuwa anaongea pumba hadi roho ikaniuma eti waziri kivuli wa fedha hovyo kabisa. Zitto amekomaa kiuchumi, kuna mambo amenifungua macho, kuwa sasa uchumi wetu unategemea watalii mgodi wa Geita na mauzo ya viti vya plastic, ndo kilimo kifuate, hii ni habari mbaya kabisa kusikia.
Kushuka kwa kilimo cha pamba kwa 40% hii ni habari ya kushitua sana, wakati mjerumani alisema pamba ni white gold sie imegeuka laana. Japo mvua zinanyesha mashamba yote hayajalimwa, yale majembe ya kukokotwa na ng'ombe hayapo tena.
Pia amegusia kuwa upumbavu wa hawa jamaa kusema nchi hatatawalika kunaleta hofu kwa watu wenye mitaji yao.