Acheni kudanganya watu nyinyi bavicha, binafsi nilifika kwenye ule mkutano wa jana pale kwenye viwanja vya mwembetogwa na Msigwa hajaongea lolote la maana zaidi ya kumkashifu Rais Kikwete kwa kumuita profesa wa kichina na pia kubeza juhudi za serikali katika ujenzi wa miundo mbinu mbalimbali ikiwemo barabara akidai eti hiyo ni miradi tu (projects) ambazo hazimsaidii raia wa kawaida.
Msigwa jana kaongea yafuatayo kwa ufupi:-
1: magufuli sio suluhisho sababu haikuwa plan yeye apeperushe bendera ya ccm kwenye urais. (upuuzi mtupu)
2: pia amenukuu baadhi ya misemo ya wachina kama ifuatavyo...!
A. Ukiwa na plan ya mwaka 1 panda mpunga maana utavuna ndani ya kipindi hicho.
B. Ukiwa na plan ya miaka 25 panda miti maana utaweza kuivuna ndani ya muda huo.
C. Ukiwa na plan ya miaka 100 jenga fikra za watu kutambua haki zao.
NB: kwa maana hiyo Msigwa jana ame-declare kuwa ana plan ya miaka 100 kwahiyo yupo bize kutoa elimu ya uraia ndo maana masuala kama huduma za kijamii kama vile maji,barabara,elimu,afya na mengineyo sio VIPAUMBELE vyake na hata vishughurikia.
3: alipotakiwa aeleze ameifanyia nini iringa alidai eti MUDA hautoshi kuelezea sababu ni wakati wa msanii Frola Mbasha na wenzake kama mike T mnyalu,Izzo bizness na Roma mkatoliki KUTUMBUIZA.
4: pia anajivunia kwa kipindi cha miaka 5 ya ubunge wake watu wa iringa sasa wanatambua haki zao,pia ni MAJASIRI wa kupigana na polisi maana hawawaogopi tena polisi.
5: pia anajivunia kulala selo ingawa ana kitanda kizuri na mke mzuri nyumbani. ( mke wa msigwa ni meneja wa crdb tawi la iringa anaitwa mama Kisa)
6: pia anajisifu jinsi spika Anna Makinda anavyomuogopa pindi akiona jina lake kwenye orodha ya wachangiaji.
Mwisho.
Msigwa kama mbunge hajafanya lolote hapa iringa hata jambo la kipuuzi hajafanya achilia mbali jambo la maana.
Kuthibitisha nisemayo namnukuu "wana iringa mnahitaji mtambue haki zenu na sio madaraja maana mvua ikija yatabomoka" mwisho wa kunukuu.
Kiukweli wana iringa tunahitaji tumpate mbunge baada ya kuishi miaka 5 bila ya mbunge maana huyu anaemaliza muda wake hajafanya lolote lile liwe dogo au kubwa na mwenyewe amethibitisha hilo jana.