Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,741
- 218,332
Bado sijafahamu sababu hasa za Wanasiasa kujazana kwenye Msiba wa Bibi yule, ambaye yeye mwenyewe hakuwa Mwanasiasa.
Bali nadhani uwepo wa Mtoto wake, mpigania haki Emmaus Bandekile Mwamakula yaweza kuwa chanzo cha kujazana kwa wanasiasa kwenye msiba huo wa mkulima mdogo wa Kijiji cha Itunge.
Sijui kama walialikwa ama la , Lakini ccm ndio waliokuwa wa kwanza kutoa salamu zao kwenye msiba huo, wakiongozwa na Diwani wa eneo hilo pamoja na Mwakilishi wa Mbunge, kama kawaida ya ccm wakaleta porojo zao za ujenzi wa barabara kutoka Community center hadi Itunge, jambo ambalo lilizua zogo msibani hapo, hii ni baada ya Waombolezaji kutokuwa na imani na CCM, wanadai porojo hizo ni za kila mwaka.
Kazi ikaanza baada ya Wawakilishi wa Chadema, ambao ni Mwenyekiti wa Mkoa wa Mbeya, China wa China na Twaha Mwaipaya kutoka Bavicha Taifa, baada ya hawa kupewa kipaza sauti Msiba ukageuka kuwa Shangwe, walipangua uongo wote wa CCM, hakika Chadema Kyela ina watu.
Bali nadhani uwepo wa Mtoto wake, mpigania haki Emmaus Bandekile Mwamakula yaweza kuwa chanzo cha kujazana kwa wanasiasa kwenye msiba huo wa mkulima mdogo wa Kijiji cha Itunge.
Sijui kama walialikwa ama la , Lakini ccm ndio waliokuwa wa kwanza kutoa salamu zao kwenye msiba huo, wakiongozwa na Diwani wa eneo hilo pamoja na Mwakilishi wa Mbunge, kama kawaida ya ccm wakaleta porojo zao za ujenzi wa barabara kutoka Community center hadi Itunge, jambo ambalo lilizua zogo msibani hapo, hii ni baada ya Waombolezaji kutokuwa na imani na CCM, wanadai porojo hizo ni za kila mwaka.
Kazi ikaanza baada ya Wawakilishi wa Chadema, ambao ni Mwenyekiti wa Mkoa wa Mbeya, China wa China na Twaha Mwaipaya kutoka Bavicha Taifa, baada ya hawa kupewa kipaza sauti Msiba ukageuka kuwa Shangwe, walipangua uongo wote wa CCM, hakika Chadema Kyela ina watu.