Haya mambo ya hivi yanaleta giza sana. Hivi kweli mtu anayekabiliwa na kesi kubwa ya wizi wa ufisadi eti anajiua halafu tunaambiwa kirahisi rahisi hivi bila kuwa na uthibitisho usio na shaka. Hivi hakuna wenye hekima kushauri namna ya kudeal na mambo tata kama haya sawa na lile kifo cha Balali kweli?
Sikiliza. Ombudsman mimi nasema hapa tunautaka msululu wa watu wenye dhamana wathibitishe kifo hiki pasi na shaka kuwa aliyekufa ndiye na pia hatua gani zinachukuliwa kutoka katika mali zake maana bado anahitajika kufilisiwa kulipa fedha zetu.
Hakuna mchezo hapa katika mambo kama haya ambayo kila mwananchi ana hitaji kujua kwa uwazi, unatakiwa kuwashirikisha washiriki wengi wenye dhamana na waseme wazi mbele ya press conference na picha na video kututhibitishia ukweli huu uonekane: Hawa ni kama vile:
Mkemia Mkuu wa Serikali akishiriana na Chief Pathologist, Mkurugezi wa mashitaka ya makosa ya jinai, Jaji Mkuu, Mbunge wa eneo analokaa marehemu, Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wake, Diwani wake, kiongozi wa chama cha waandishi wa habari, Usalama wa Taifa, na mashuhuda wananchi wa kawaida wakiwemo viongozi wa dini ili siku moja ikionekana kuwa kuna uzushi au kuwa tulidanganywa basi wote hao wanahusika wanawajibishwa!
Kwa nini tunapenda kurahisisha mambo sana na usiri katika kesi nyeti za namna hii?