Mshahara wa July 2019 vipi?

Mshahara wa July 2019 vipi?

Mkuu hata wenye vyanzo vingine nao wamekwama kwa kuwa wanategemeana.
Watu hawaendi saluni, hadi mshahara utoke.
Wenye nyumba hawajalipwa kodi hadi mshahara utoke
Watu hawanywi vinywaji vya burudani hadi mshahara utoke
Watu hawanunui vitu vingine ambavyo sio basic needs hadi mshahara utoke
KUCHELEWA KWA MSHAHARA KUNAKWAMISHA HATA WENYE SHUGHULI ZINGINE
Nakuelewa na mie pia ni m/kazi. Watu wanakwama mpk wanakopa kwa kuchelewa kwa wiki tu, ukiwa na vyanzo vingine huwezi kukosa sh mbili tatu za ku-survive.
 
Ngoja ni wahi kwa yule mwenye kadi yangu ya benki
🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️
Maikinii weee.....

😂😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Kufulia hakuna mwenyewe.
Miezi mingi imepita, kila mshahara unapotoka mfukoni nina fedha nilizozipata kwa kupiga madili. Kuna mtu kashituka aliposikia neno kupiga dili. Si kila dili ni haramu, madili mengine ni shughuli halali.
Mwezi huu, nimebanwa hadi nashangaa. Mfukoni nina 4 tu mpaka sasa, kama salary haijatoka mpaka jioni naingia road napiga bodaboda.
Magu shikamoo.
hiyo inaitwa ''kuelekea 2020'''
 
Mkuu hata wenye vyanzo vingine nao wamekwama kwa kuwa wanategemeana.
Watu hawaendi saluni, hadi mshahara utoke.
Wenye nyumba hawajalipwa kodi hadi mshahara utoke
Watu hawanywi vinywaji vya burudani hadi mshahara utoke
Watu hawanunui vitu vingine ambavyo sio basic needs hadi mshahara utoke
KUCHELEWA KWA MSHAHARA KUNAKWAMISHA HATA WENYE SHUGHULI ZINGINE
Sure
 
Mshahara umetoka na kuna badiliko kwa waliopandishwa madaraja, Aidha kuna madeni yamelipwa kwa waliokuwa wanadai malimbikizo ya mishahara, fedha za likizo, matibabu, uhamisho n.k. Aidha kundi jengne linataraji kubadilishiwa vyeo mwishoni mwa mwezi huu. Fupisha habari hii kwa maneno 30
 
Mshahara umetoka na kuna badiliko kwa waliopandishwa madaraja, Aidha kuna madeni yamelipwa kwa waliokuwa wanadai malimbikizo ya mishahara, fedha za likizo, matibabu, uhamisho n.k. Aidha kundi jengne linataraji kubadilishiwa vyeo mwishoni mwa mwezi huu. Fupisha habari hii kwa maneno 30
Dah utanisababishia ban aiseee nusu nitukane nilipofika huo mstari WA mwisho, ila huendi
 
Demiss data
Mshahara tayari, ila naona wanaanza kuwekea watu wa NMB benki zingine muendelee kuwa wavumilivu.
UZI WETU UNAKWENDA KUISHIA KABURINI. RIP HUU UZI. nahisi hii comment yangu itakuwa ni ya mwisho.
 
Hakuna nyongeza hata sh. 100
😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡😡
 
Mshahara umetoka na kuna badiliko kwa waliopandishwa madaraja, Aidha kuna madeni yamelipwa kwa waliokuwa wanadai malimbikizo ya mishahara, fedha za likizo, matibabu, uhamisho n.k. Aidha kundi jengne linataraji kubadilishiwa vyeo mwishoni mwa mwezi huu. Fupisha habari hii kwa maneno 30
wewe ni lazima utakuwa ni mteja wa Milembe. Sio bure Boss.
 
Back
Top Bottom