Hiyo msg hata mimi niliipata. Vodacom wanadisclose namba zetu kwa watu wasiohusika
Msg inasema"we have an important msg for you to know it call this number 004238770736 free. Shida yangu nahitaji kujua hizo namba za nchi gani? Na vodacom nao wana share na hao?
Mimi pia nimeipata sms kama hiyo jana wakati ninatoka kanisani. Nilifikiri maombi yangu yamekubaliwa na Mola na hivyo naweza kuuweka umasikini kwenye historia!
Kwa kadri nijuavyo mimi Voda lazima wahusike kwahili
Kama kweli ukipiga wanakomba salio lako lote je wataenda wapi ku claim hizo credit kama sio Vodacom?
Mfano ninapokuwa na mchezo wangu napeleka voda na kuomba watakao shiriki wakatwe let say sh 200, basi hapo ujuwe voda watakata hela yao ya msg kama ni sh 40 na commission yao labda sh 30 na kinacho bakia mimi mwenye mchezo itabidi niende Vodacom ku claim kilicho baki katika 200 baada ya Voda kukata yao, na hapa lazima niende Voda kwasababu wao tayari walisha uza vocha na wanayo in terms of money
Sasa hawa jamaa wakikomba credit zako wata claim wapi kupata hizo pesa kama sio Voda
I stand to be corrected