KipimaPembe
JF-Expert Member
- Aug 5, 2007
- 1,285
- 699
Nchi yoyote inayofuata utawala wa sheria huongozwa kwa kufuata misingi na taratibu za kisheria ambazo zimetungwa na kuhalalishwa ndani ya bunge halali (legislature). Nchi haiongozwi wala kutawaliwa kutumia sera wala ilani za uchaguzi za vyama vya siasa. Ilani hizo na sera za vyama vya siasa inatakiwa zitumiwe kutoa mwelekeo wa utungaji wa sheria! Kwa mfano ni sheria zipi zitungwe, sheria hizo zikazie nini, vipaumbele katika utendaji viwekwe wapi, n.k.
Ni jambo la hatari sana na ni upotovu mkubwa kuingiza siasa katika utendaji wa serikali (ndo hayo yanayoendelea) na jambo hili limeshehenezwa sana na muundo wa CCM ambao hautoi mgawanyo wa kiutendaji kati ya serikali na chama. Tunajua wote jinsi jambo hilo lilivyougharimu uchumi wa Tanzania enzi za chama kushika hatamu. Wanasiasa (wawakilishi wa vyama) kwenye mashirika ya umma ni mojawapo ya vyanzo vya migogoro na matitizo ya kimenejimenti yaliyoua mashirika mengi ya umma.
Ni kweli kuwa baada ya kubadili mfumo, bado nchi inaendeshwa kimazoea. Watendaji wa serikali na hata Mawaziri (ambao ni wanasiasa) inatakiwa watekeleze sheria za nchi. Na sheria za nchi ni zile zilizotungwa na bunge!! Ni kweli kuwa sera na ilani za vyama vinaathiri utungwaji huo wa sheria, lakini sheria zikishasimama haziwi za vyama tena. Zinakuwa sheria za nchi na zinawahusu watu wote.
Haya ya kukaa na kusema hapa tunatekeleza ilani ya uchaguzi wa chama tawala ni upotovu na unaipeleka nchi pabaya mahali ambapo kila kitu kina-siasishwa na kufanya sehemu ya siasa. Manake utasema hata mahakama zinaamua kwa kufuata ilani ya vyama vilivyoko madarakani kwa sababu vyama hivyo ndo vimetoa sera inayoongoza sheria!! Tumepotoka mno na kupoteza mwelekeo! Hakika huu ugonjwa hautapona haraka mpaka kiingie chama kingine madarakani; hata hapo kuna hatari chama kingine kikiingia madarakani, kuendeleza mfumo huo.
Watendaji wote pamoja na rais mwenyewe wanaongoza nchi kwa kufuata sheria za nchi na si ilani wala sera za vyama vyao. Sera na ilani za vyama vya siasa zinatumika kuweka mwongozo tu wa sheria zitungweje! Ndo maana sheria zinajadiliwa na kupitishwa bungeni.
Hii inasababishwa mambo mengi kupenyezwa; mambo ambayo hayakupita bungeni yanapenyezwa kwa visingizio vya ilani na sera za vyama. Hatari hapa ni kubwa sana!!
Ni jambo la hatari sana na ni upotovu mkubwa kuingiza siasa katika utendaji wa serikali (ndo hayo yanayoendelea) na jambo hili limeshehenezwa sana na muundo wa CCM ambao hautoi mgawanyo wa kiutendaji kati ya serikali na chama. Tunajua wote jinsi jambo hilo lilivyougharimu uchumi wa Tanzania enzi za chama kushika hatamu. Wanasiasa (wawakilishi wa vyama) kwenye mashirika ya umma ni mojawapo ya vyanzo vya migogoro na matitizo ya kimenejimenti yaliyoua mashirika mengi ya umma.
Ni kweli kuwa baada ya kubadili mfumo, bado nchi inaendeshwa kimazoea. Watendaji wa serikali na hata Mawaziri (ambao ni wanasiasa) inatakiwa watekeleze sheria za nchi. Na sheria za nchi ni zile zilizotungwa na bunge!! Ni kweli kuwa sera na ilani za vyama vinaathiri utungwaji huo wa sheria, lakini sheria zikishasimama haziwi za vyama tena. Zinakuwa sheria za nchi na zinawahusu watu wote.
Haya ya kukaa na kusema hapa tunatekeleza ilani ya uchaguzi wa chama tawala ni upotovu na unaipeleka nchi pabaya mahali ambapo kila kitu kina-siasishwa na kufanya sehemu ya siasa. Manake utasema hata mahakama zinaamua kwa kufuata ilani ya vyama vilivyoko madarakani kwa sababu vyama hivyo ndo vimetoa sera inayoongoza sheria!! Tumepotoka mno na kupoteza mwelekeo! Hakika huu ugonjwa hautapona haraka mpaka kiingie chama kingine madarakani; hata hapo kuna hatari chama kingine kikiingia madarakani, kuendeleza mfumo huo.
Watendaji wote pamoja na rais mwenyewe wanaongoza nchi kwa kufuata sheria za nchi na si ilani wala sera za vyama vyao. Sera na ilani za vyama vya siasa zinatumika kuweka mwongozo tu wa sheria zitungweje! Ndo maana sheria zinajadiliwa na kupitishwa bungeni.
Hii inasababishwa mambo mengi kupenyezwa; mambo ambayo hayakupita bungeni yanapenyezwa kwa visingizio vya ilani na sera za vyama. Hatari hapa ni kubwa sana!!