Msanii Snura afungiwa kujihusisha na sanaa, TCRA waagizwa kuifuta video ya Chura mtandaoni

Wakuu binafsi nashindwa kuwaelewa baadhi ya wasanii wetu kwa nyimbo na video zao kuwa nje ya maadili ya kitanzania, msanii anatoa wimbo umejaa maneno ya udhalilishaji mtupu na video watu wako uchi wanacheza hovyo picha za kichefuchefu, mpaka unajiuliza hivi huyu msanii anayo familia kweli? Ana mtoto, mume, wazazi kweli? Halafu wakifungiwa na vyombo husika kama BASATA, wanaanza kujilizaliza eti wanaonewa! Nani anakuonea? Acha mfungiwe tu mpaka mkipata akili, MFUNGIWE TU
 
Ni sawa basata wana wafungia ila wanafungia kwa muda 2 ila baada ya mwenzi ana endelea na kazi kimya kimya basata nawo ni majipu mbona wimbo wa anakonda una pigwa radio adi tv hapa bongo tena kweupe amna kiongozi yoyote aliye ongea kama siyo siasa nini? uwo uonevu 2.
 
Ni sawa basata wana wafungia ila wanafungia kwa muda 2 ila baada ya mwenzi ana endelea na kazi kimya kimya basata nawo ni majipu mbona wimbo wa anakonda una pigwa radio adi tv hapa bongo tena kweupe amna kiongozi yoyote aliye ongea kama siyo siasa nini? uwo uonevu 2.
 
Mambo ya digitali hayo mzee,tunaenda Na yo mdogo mdogo, watu wanashangaa wimbo waache kushangaa miili inauzwa haaa haaa haaa
 
Wewee wazeee nini? We huna baba au babu? Unawadharau? Hutazeeka? Dont be stupid is a matter of time
 
Malezi Na makuzi ndio umfanyaa mtu awe alivyo.tena kwa watu ambao ni public figure msingi wa maisha yao yanaonekana mapema.
 
wakuu binafsi nashindwa kuwaelewa baadhi ya wasanii wetu kwa nyimbo na video zao kuwa nje ya maadili ya kitanzania, msanii anatoa wimbo umejaa maneno ya udhalilishaji mtupu na video watu wako uchi wanacheza hovyo picha za kichefuchefu, mpaka unajiuliza hv huyu msanii anayofamilia kweli? ana mtoto,mume, wazazi kweli? halafu wakifungiwa na vyombo husika kama basata, wanaanza kujilizaliza eti wanaonewa! nani anakuonea? acha mfungiwe tu mpaka mkipata akili, MFUNGIWE TU
Nilitamani ataekwa na ndani kabisa na hao wendawazimu wenziee
 
View attachment 344659
Katikati ni mkuu wa Kitengo cha mawasiliano wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Zawadi Msalla akiwa na maafisa wengine wakizungumza na waandishi wa habari.


Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo leo imetangaza kumfungia Snura kujihusisha na masuala ya sanaa.

Pia imeufungia wimbo wake Chura pamoja na video yake kutochezwa kwenye redio na TV nchini.

Taarifa hiyo imetolewa na wizara hiyo kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wake wa mikutano wizarani hapo jijini Dar.

Akiongea na waandishi wa habari, Mkuu wa Kitengo cha mawasiliano wa wizara hiyo, Zawadi Msalla, amewaonya watu kutousambaza wimbo huo kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo WhatsApp.

Amedai kuwa wale watakaokiuka agizo hilo watashtakiwa kwa kutumia sheria ya makosa ya mtandao.

Dance yenyewe ruksa?
 
kuna nyimbo nyingii sanaaa, tenaa maandili yake ni mabovu kuliko hiyo ya Chura, toeni tamkoo kwa zotee, kwan hata hizo nyingne zipo youtube na tv zetu wanazionyesha kama kawaida
 
HIII NYIMBO INA TOFAUTI GANI NA NYIMBO YA DIAMOND YA NASEMA NAYE ? HEBU ANGALIENI PARTY YA MWISHO WANA WAKE WANAVOMWAGA RADHI ..NI UCHAFU MTUPU NA UJINGA.
HII NI DOUBLE STANDARD TU.


Sawa hata hii. Naona Kama chura imepitiliza
 
Ni kweli kabisa. Imefikia kipindi sasa kule Basata wale wazee wasepe wawaachie vijana. Kwa sbb unapofungia ktk Radio station and TV. Unakuwa unataka kumkomoa mtu. Siku zote wazee wanaaaribu sana. Wanadai maadili lakini wao ndio waaribufu wa maadili wakubwa. Wafute basi na picha za ngono zote ktk Tanzania ili tujue kwamba hii nchi ya maadili. Kwa sbb Kuna mapicha ya ngono mengi yapo Tanzania. Wameshindwa kuzuia

Hawa wazee wanakera kwakweli afu kwenye hii sheria ya mtandao ndo WAMEVURUNDA KABISAAA!! Bora waseme moja tu kua ni marufuku kutumia INTERNET tanzania tujue moja sio kutunyanyasa kizee zee na generation hii bana. Mtu smartphone yako ila unaitumia kwauoooga dah

#SheriazaKizeesasaBasi
 
Back
Top Bottom