Msanii Snura afungiwa kujihusisha na sanaa, TCRA waagizwa kuifuta video ya Chura mtandaoni

Nimejaribu kila njia ya kiungwana kama kwenda kumuomba apunguze sauti ya mziki wake mara kadhaa lakini jirani huyu asikii.
Nimeenda hadi kwa balozi wa nyumba kumi lakini still bado huyu dada asikii.
Mbaya zaidi tokea wimbo wa msanii Snura wa Chura ufungiwe , yeye ndio amekuwa akiucheza kuanzia asubuhi mpaka usiku tena kwa sauti ya juu. Ukiisha tu anaurudia kuupiga.
Imefikia hatua hata nikiwa nimepumzika mida ya mchana huwa naota naangalia vyura wa kwenye huo wimbo wakinesa nesa na kuruka kichura chura.
Naombeni msaada wenu wana JF nifanyeje, kwa maana chura imekuwa kero kwangu, kwani nahisi kuchanganyikiwa.
Wewe Ni mwanamke?
 
Salaam jf

Nimeshangazwa na style iliyotumika kufungia nyimbo ya Snura inayofahamika kama snail(video na audio), ambapo kabla ya kufungiwa kwake nyimbo hiyo ilikuwa sio maarufu sana katika mitandao na hata katika jamii lakini baada ya kufungiwa kwake na mamlaka husika nchini, sasa nyimbo hiyo imekuwa maarufu na inafuatiliwa na watu wengi kuliko ufuatiliaji wa vitu vingene. Utafiti mdogo nilioufanya katika jamii inaonyesha kuwa watu wengi wenye simu za mikononi zenye uwezo wa kucheza mafaili ya video, basi lazima utakuta faili la video la msanii huyo limo hii uhusisha wanafunzi wa vyuo vikuu, walimu, wanajeshi, maaskari, waingiza nyimbo katika simu, wanafunzi wa sekondari hasa shule za kata, huku ikiwaacha watu wa dini kunusurika na swala hilo. Na haya yote ushaidi upo. Licha ya serikali kutoa onyo kali dhidi ya mtu atakaekiuka maagizo yaliyotolewa na serikali kuhusu uchezwaji wa nyimbo hiyo.

kulikuwa hakuna sababu kwa serikali kuliweka katika jamii kwa mtindo wa media badala yake kufikisha kwa watu husika na kuliwacha na mwishowe kupotea lenyewe kulingana na mazingira. Lakini mambo yamekuwa ni kinyume yaani sasa hivi Nyimbo hii inaimbwa darasani laivu na imekuwa ni ajenda iliyobebwa na wanafunzi wote wa shule za sekondari za kata na wanafunzi kukata mauno. Natarajia haya hayatakiwi kutokea tena katika idara husika iliyohusika kutoa tamko la kuzuiwa kwa nyimbo sampuli hizi.
 
Ninachojua soon video hiyo itawachosha watazamaji wake na wao wataiacha kuiangalia.

Kizuri ni kuwa Snura mwenyewe kasema kweli hajaonewa, na kakubali kosa kuwa video haikuwa safi.

Na nzuri zaidi kasema hatatoa nyimbo kama ile, so ni hatua nzuri sana kwa serikali
 
Ninachojua soon video hiyo itawachosha watazamaji wake na wao wataiacha kuiangalia.

Kizuri ni kuwa Snura mwenyewe kasema kweli hajaonewa, na kakubali kosa kuwa video haikuwa safi.

Na nzuri zaidi kasema hatatoa nyimbo kama ile, so ni hatua nzuri sana kwa serikali
But ilishaleta athari katika jamii, mfano skendo ya mamvi si unaiona katika jamii ilivyo na athari.
 
But ilishaleta athari katika jamii, mfano skendo ya mamvi si unaiona katika jamii ilivyo na athari.
Ni kweli mkuu, lakini bora nusu shari kuliko shari kamili.

Watanzania wanaomiliki video ya chura kwenye simu zao wengi ni wapenzi wa "makitu", kwa hiyo ka video kama hako kwao si ukakasi sana, kibaya ni watoto wadogo wanaokesha kutwa kuangalia kwenye TV miziki ya bongofleva.
 
Ni kweli mkuu, lakini bora nusu shari kuliko shari kamili.

Watanzania wanaomiliki video ya chura kwenye simu zao wengi ni wapenzi wa "makitu", kwa hiyo ka video kama hako kwao si ukakasi sana, kibaya ni watoto wadogo wanaokesha kutwa kuangalia kwenye TV miziki ya bongofleva.
Hapo upo sawa mkuu.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom