M-bongotz
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 1,734
- 405
MSANII ‘sidanganyiki' wa filamu nchini, Elizabert Michael ‘Lulu' ameamua kukiri maovu yake yote ambayo amekuwa akiyatenda huku akijua kwamba yeye ni kioo cha jamii.
Akiongea na Amani juzi, Lulu alisema kuwa amekaa chini na kutafakari yote yaliyokuwa yakiandikwa magazetini kuhusu yeye na kubaini kwamba amefanya makosa hivyo kuwaomba Watanzania wamsamehe.
Alisema kuwa, anaamini hakuna binadamu aliyekamilika na kwamba anakiri udhaifu wake huo na kuahidi kubadilika.
"Nimetenda dhambi nyingi sana hivyo nawaomba Watanzania wajue kuwa hakuna binadamu aliye mkamilifu chini ya jua.
"Wakati mwingine skendo zinazoelekezwa kwangu hazina ukweli ila kwakuwa nimebaini wapi nakosea, naahidi kujirekebisha, namuomba Mungu awe nami katika dhamira yangu hii,"alisema Lulu.
Katika siku za hivi karibuni binti huyu mwenye umri mdogo amekuwa akiandamwa na skendo za mapenzi, kuvaa kihasara na ulevi kiasi cha kuwafanya watu kumhurumia hasa kutokana na ukweli kuwa umri wake na mambo anayofanya ni tofauti kabisa.
Source: www.globalpublishers.info
MY TAKE:
Namwombea kwa Mungu ili awe anamaanisha kweli hayo maneno yake, bado ni binti mdogo sana asiyestahili kupoteza dira ya maisha katika umri alionao.
Jikumbushe vimbwanga vya kabinti haka kwa kubofya hapa.
Akiongea na Amani juzi, Lulu alisema kuwa amekaa chini na kutafakari yote yaliyokuwa yakiandikwa magazetini kuhusu yeye na kubaini kwamba amefanya makosa hivyo kuwaomba Watanzania wamsamehe.
Alisema kuwa, anaamini hakuna binadamu aliyekamilika na kwamba anakiri udhaifu wake huo na kuahidi kubadilika.
"Nimetenda dhambi nyingi sana hivyo nawaomba Watanzania wajue kuwa hakuna binadamu aliye mkamilifu chini ya jua.
"Wakati mwingine skendo zinazoelekezwa kwangu hazina ukweli ila kwakuwa nimebaini wapi nakosea, naahidi kujirekebisha, namuomba Mungu awe nami katika dhamira yangu hii,"alisema Lulu.
Katika siku za hivi karibuni binti huyu mwenye umri mdogo amekuwa akiandamwa na skendo za mapenzi, kuvaa kihasara na ulevi kiasi cha kuwafanya watu kumhurumia hasa kutokana na ukweli kuwa umri wake na mambo anayofanya ni tofauti kabisa.
Source: www.globalpublishers.info
MY TAKE:
Namwombea kwa Mungu ili awe anamaanisha kweli hayo maneno yake, bado ni binti mdogo sana asiyestahili kupoteza dira ya maisha katika umri alionao.
Jikumbushe vimbwanga vya kabinti haka kwa kubofya hapa.