TANMO
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 11,514
- 11,277
Wakuu hii nimeikuta kwenye Blog moja ya Kitanzania Afade Sele akionesha hisia zake juu ya ujanja ujanja wa Mheshimiwa Rais wetu JK. Kwa maelezo yake anaona kuwa JK anakusudia kuleta tofauti miongoni mwa watu wa kada mbali mbali:
Msanii huyu anasema hivi:
Msanii huyu anasema hivi:
"Ah, huyu JK kwa tamko lake hili kuhusu studio aliyowapa THT na Ruge anaonyesha jinsi gani asivyo kiongozi makini na kwa mtazamo halisi anaonyesha ni jinsi gani hakustahili kuwa mkuu wa nchi. Anajenga makundi ya chuki na uhasama katika kila sekta kuanzia kwenye chama chake, serikali yake na sasa kwenye sanaa na haswa mziki wetu ambao ndio amekuwa akijinadi kuusaidia kumbe katika hii awamu yake ndio mziki umepotea mwelekeo. Sasa kama anasema studio aliwapa waliomuomba mbona mimi na watu wengine wenye misimamo tulikuwepo siku ile alipoahidi studio hatujui lolote na hatujaonyeshwa hiyo studio?"