Mimi ni mmoja wa watu wanaodharau wanamuziki wa bongofleva hasa pale wanapomkatikia kiuno Mkwere hasa kwenye matukio ya uchaguzi. Naona mambo yanaanza kubadilika. Alianza Sugu na Mkoloni. Safari hii Selemani Msindi, narudia tena SULEMAN amenukuliwa akisema yafuatayo dhidi ya Kikwete:
Chanzo: k-massive-music
"Ah, huyu JK kwa tamko lake hili kuhusu studio aliyowapa THT na Ruge anaonyesha jinsi gani asivyo kiongozi makini na kwa mtazamo halisi anaonyesha ni jinsi gani hakustahili kuwa mkuu wa nchi.
Anajenga makundi ya chuki na uhasama katika kila sekta kuanzia kwenye chama chake, serikali yake na sasa kwenye sanaa na haswa mziki wetu ambao ndio amekuwa akijinadi kuusaidia kumbe katika hii awamu yake ndio mziki umepotea mwelekeo.
Sasa kama anasema studio aliwapa waliomuomba mbona mimi na watu wengine wenye misimamo tulikuwepo siku ile alipoahidi studio hatujui lolote na hatujaonyeshwa hiyo studio?"
Chanzo: k-massive-music