Msamaha na Kisasi

Msamaha na Kisasi

Kusamehe Kwa dhati, imekuwa Ngumu sana Kwa Binadamu, Maana ukisamehe mtu akakukosea Tena, Huwa tunarudia na kusema hii ni mara ya pili unanikosea, Mwanzo ulinikosea!
kusamehe unasamehe lakini haina maana et ubongo unafuta kila kitu
ukikosewa tena lazima ubongo utakukumbusha kua huyu mtu sio mara yake ya kwanza ni tabia yake
Na Visasi tunavyovingi hata Kama mtu hakukukosea, Mfano mtu unamkopa Hela, ukiwa unaamini atakukopesha, kumbe hana, Sasa Kwa Kukosa kukukopesha,siku akija na shida ya kukopa,unamnyima wakati unazo, unakumbuka Yeye hakukukopesha, kumbe alikuwa hana!
Hapa tatizo ni matarajio ndiyo hua sababu ya makasiriko
Wewe saidia kwa moyo mambo ya kulipwa fadhila usiyaweke kicwani
 
Msamaha ni kwa ajili yangu, si kwa ajili ya aliyenikosea ukifikiri kuwa hata mimi huwa nawakosea wengine, hivyo huachilia, maana kisasi kina hasara kubwa.

Fikiria kama mtu amekuchukulia mke wako halafu na wewe unaenda kulipiza kisasi labda kwa mke wake, au vyovyote ukakutana na magonjwa majuto anakuwa mjukuu
Msamaha ni kwa ajili ya anaesamehe upo sahihi

Kisasi kinaweza kuleta majuto ya maisha
 
Back
Top Bottom