Serikali ya Magufuli imeendelea kuwashughulikia wafuasi wa UKAWA na Lowassa kwa kutumia nguvu nyingi za Dola tangu walipokamata vijana wa tallying centres wa Chadema na kuwasingzia kuwa walikuwa wanafanya human trafficking, na sasa wanasema vijana wale waliingilia mitandao ya Tume ya Uchaguzi ili kuanza kupata matokeo, pamoja na kesi inayoendelea ya vijana hao mahakamani.
Sasa wameanza kukamata watu wote waliokuwa wakiwasiliana na vijana hao, na leo usiku huu alitekwa mkurugenzi wa zamani wa Stanbic; Bashir Awale; katika mazingira ya kutatanisha, lakini kwa tuhuma hizo hizo.
Hii njia ya kupunguza ari na joto la wananchi mamailioni ambao hawajaridhika na Uchaguzi wa mwaka huu. Inasikitisha sana kuona demokrasia inaporwa na vyombo vyetu vya Dola vikitumika vibaya.