Msaidizi wa Kampeni wa Edward Lowassa mbaroni

Msaidizi wa Kampeni wa Edward Lowassa mbaroni

Hakuna bias katika reporting ya Nipashe. Isipokuwa tu hawakusema lile gari lilipotelekezwa what happened next.
 
Usitujumlishe sisi wetu lowasa atumjui uyo mropoka ovyo

unaweza ukamwambia hivyo moja kwa moja kiwa ni mropokaji? au unaweza kumtumie ujumbe moja kwa moja aupate? kama unaweza poa ila kama huwezi nakishauri tu chuna maneno yako kwa mkuu wa nchi. wengine sisi tutukane tu hatuna shida. sio J.K yule wa kutukanwa na kuchekacheka. nakushauri ndugu yangu. fuata sheria. kosoa toa maoni lakini usimtukane
 
Labda Wananchi wa Kishumundu na Kibosho lkn WatanZania waliobakia wana Imani na Magufuli kwanza hata wale waliompigia kura fisadi Lowasa wameanza kujutia kura zao baada ya kuona kasi ya Raisi JPM!

Kua na hifadhi kidogo ya maneno,kuendesha nchi si sawa na kuendesha familia yako.
 
ccm mbona povu linawatoka sana? Hivi nchi hii wakukamatwa ni wapinzani tuu, mnatoa povu hadi kwa gazeti linalohabarisha eti wangesubiri, nchi inakoelekea siko asee

I can predict something bad...yaan kuna raia wanaombea watu mabaya tu wakidhani wao wako salama.yaan kuna watu wakiambia beba silaha uue wanaua kabisa bila huruma kwa hapa tulipofikia..in nachokijua ili uwe kiongozi mzuri lazima kwanza uwe na busara na hekima.halafu kiongozi hatakiwi kuwa na vinyongo,hatakiwi kuwa biased...sasa sielewi Hawa wanaomsemea Mheshimiwa,mara jeshi LA polisi sijui wanayatoa wapi...inasikitisha sana kama Tupo kwa ajili ya kukomoana.maana siasa ni mchezo wenye ushindani na ndani yake kina udhalilishaji,nitaona Hawa watu wakiwa wa ajabu endapo wataanza kuwa biased na kuanza kuonea watu...na nitashauri wapate kozi za uongozi kama kweli haya mambo ni kweli.watu tuache uchochezi tutapelekana kubaya kwa midomo yetu
 
Asante Mungu kutuepusha na lile fisadi, asante sana JK kuhakikisha fisadi lile halipiti kuanzia kwenye kamati ya maadili, wala kamati kuu, mbona tungekoma!
chupuchupu gasi yetu
 
Rashid-11Nov2015.png

Bashir Awale

Mwanamkakati wa aliyekuwa mgombea wa urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bashir Awale, amekamatwa na kuwekwa ndani katika Kituo cha Polisi cha Kati.

Habari zilizopatikana jana kutoka ndani ya timu ya kampeni ya mgombea wa CHADEMA, Edward Lowassa, zinasema kuwa Awale alikamatwa juzi jioni kwenye maeneo ya Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Taarifa zaidi zinasema kuwa Awale alisimamamishwa na askari, ambao walimchukua kwenye gari lao huku wakilitelekeza gari lake kwenye maeneo hayo.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, aliliambia Nipashe atalizungumzia suala hilo leo pamoja na mambo mengine.

Nimewaagiza vijana wangu waniandalie taarifa juu ya suala hilo. Nitalizungumzia jambo hilo kesho (leo) pamoja na mambo na mengine, alieleza Kamishna Kova, ambaye hakutaka kuingia kwa undani wakati alipohojiwa na gazeti hili kuhusiana na suala hilo.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili unaonyesha kwamba kukamatwa kwa Awale kunahusishwa na masuala ya Uchaguzi Mkuu uliomalizika hivi karibuni kutokana na ukaribu wake na Lowassa.

Lowassa alishindwa kwenye uchaguzi wa urais baada ya kushika nafasi ya pili kwa kupata kura 6,072, 848 sawa na asilimia 39.97 wakati mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli aliibuka mshindi kwa kupata kura 8,882,935 sawa na asilimia 58.46.

Awale alikuwa miongoni mwa viongozi waandamizi kwenye timu ya kampeni ya Lowassa tangu wakati alipokuwa mwanachama wa CCM.

Lowassa alipoachana na CCM na kujiunga na CHADEMA, Julai 28 mwaka huu, Awale alikuwa miongoni mwa watu waliofuatana naye.

Awale alikuwa miongoni mwa watu waliofuatana Lowassa siku anatambulishwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, baada ya kujiunga rasmi na chama hicho.

Kabla ya kuingia kwenye masuala ya siasa, Awale alikuwa Ofisa Mkuu Mtendaji wa Benki ya Stanbic nchini Tanzania kabla ya kuachia ngazi mwaka 2013.

Aliiongoza benki ya Stanbic kuanzia mwaka 2006, lakini kabla ya hapo alikuwa akifanya kazi katika Benki ya Citibank.

Tangu alipoachana na Stanbic, Awale alikuwa miongoni mwa wanamkakati waandamizi wa Lowassa tangu alipokuwa akiwania kugombea urais kwa tiketi ya CCM.

Lowassa alipokatwa jina lake CCM na kujiunga na CHADEMA, Awale alikuwamo kwenye timu ya kampeni akiwa miongoni mwa viongozi waandamizi.

Pamoja na kuwemo kwenye timu ya kampeni, pia ni anachukuliwa kama miongoni mwa wasaidizi na washauri muhimu wa Lowassa.

Kukamatwa kwa Awale kunakuja baada ya hivi karibuni vijana wanane waliokuwa wakisaidia kazi ya kujumlisha kura za Lowassa kwenye kituo cha vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kujumlisha matokeo ya kura za urais katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka huu.

Chanzo:
Nipashe

Hili gazeti naona bado halijaamini kama uchaguzi umekwisha.
 
Eti uchunguzi uliofanywa na gazeti. Tusubiri uchunguzi wa polisi. Nadhani wale ma IT 191 wanabanwa nyeti zao huko jela watakua wanalopoka sana. Ngoja tuone movie inaendelea

Mengi anatakiwa ajue kwamba uchaguzi umekwisha na Rais kaishaapishwa, aache kuleta siasa kwenye mambo ya kiuchunguzi yanayohusu vyombo vya usalama. Muda mwingine ndio maana anazomewa.
 
Rashid-11Nov2015.png

Bashir Awale

Mwanamkakati wa aliyekuwa mgombea wa urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bashir Awale, amekamatwa na kuwekwa ndani katika Kituo cha Polisi cha Kati.

Habari zilizopatikana jana kutoka ndani ya timu ya kampeni ya mgombea wa CHADEMA, Edward Lowassa, zinasema kuwa Awale alikamatwa juzi jioni kwenye maeneo ya Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Taarifa zaidi zinasema kuwa Awale alisimamamishwa na askari, ambao walimchukua kwenye gari lao huku wakilitelekeza gari lake kwenye maeneo hayo.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, aliliambia Nipashe atalizungumzia suala hilo leo pamoja na mambo mengine.

Nimewaagiza vijana wangu waniandalie taarifa juu ya suala hilo. Nitalizungumzia jambo hilo kesho (leo) pamoja na mambo na mengine, alieleza Kamishna Kova, ambaye hakutaka kuingia kwa undani wakati alipohojiwa na gazeti hili kuhusiana na suala hilo.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili unaonyesha kwamba kukamatwa kwa Awale kunahusishwa na masuala ya Uchaguzi Mkuu uliomalizika hivi karibuni kutokana na ukaribu wake na Lowassa.

Lowassa alishindwa kwenye uchaguzi wa urais baada ya kushika nafasi ya pili kwa kupata kura 6,072, 848 sawa na asilimia 39.97 wakati mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli aliibuka mshindi kwa kupata kura 8,882,935 sawa na asilimia 58.46.

Awale alikuwa miongoni mwa viongozi waandamizi kwenye timu ya kampeni ya Lowassa tangu wakati alipokuwa mwanachama wa CCM.

Lowassa alipoachana na CCM na kujiunga na CHADEMA, Julai 28 mwaka huu, Awale alikuwa miongoni mwa watu waliofuatana naye.

Awale alikuwa miongoni mwa watu waliofuatana Lowassa siku anatambulishwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, baada ya kujiunga rasmi na chama hicho.

Kabla ya kuingia kwenye masuala ya siasa, Awale alikuwa Ofisa Mkuu Mtendaji wa Benki ya Stanbic nchini Tanzania kabla ya kuachia ngazi mwaka 2013.

Aliiongoza benki ya Stanbic kuanzia mwaka 2006, lakini kabla ya hapo alikuwa akifanya kazi katika Benki ya Citibank.

Tangu alipoachana na Stanbic, Awale alikuwa miongoni mwa wanamkakati waandamizi wa Lowassa tangu alipokuwa akiwania kugombea urais kwa tiketi ya CCM.

Lowassa alipokatwa jina lake CCM na kujiunga na CHADEMA, Awale alikuwamo kwenye timu ya kampeni akiwa miongoni mwa viongozi waandamizi.

Pamoja na kuwemo kwenye timu ya kampeni, pia ni anachukuliwa kama miongoni mwa wasaidizi na washauri muhimu wa Lowassa.

Kukamatwa kwa Awale kunakuja baada ya hivi karibuni vijana wanane waliokuwa wakisaidia kazi ya kujumlisha kura za Lowassa kwenye kituo cha vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kujumlisha matokeo ya kura za urais katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka huu.

Chanzo:
Nipashe

Hata afande Temu alokamatwa kwa rushwa huko Tanga si ajabu familia yake ilikuwa na ushabiki kama wako wakiwa hawajui kama hata wao yanaweza kuwapata.tena bora huyo wa mabilioni kuliko wewe utakapokamatwa na hela ya dagaa..hamna msafi kwa sasa na kila mtu ana njaa ya hela so tusishabikie sana tukasahau kuwa na sisi tumo safarini
 
EL angekuwa rais, mafisadi wangefanyia sherehe sayari ya Mars. Pole pole mpaka atatiwa hatiani kubwa la maadui.

Kuna watu humu walijifanya wadukuzi na watetezi wa upuuzi... ngoja tuone wanaishia wapi

Hata afande temu huko tanga si ajabu familia yake ilikuwa na ushabiki kwa wako hawakujua kama wanaweza wakapatwa na jambo.Tanzania hii hamna msafi na kama ni msafi utabambikiziwa hata kesi.Tusishabikie sana maana bora wao wataenda kushtakiwa kwa hela kubwa maana wengine watakamwatwa kwa hela ya dagaa kama Afande huyu so tujitazame na sisi pia.
 
Labda Wananchi wa Kishumundu na Kibosho lkn WatanZania waliobakia wana Imani na Magufuli kwanza hata wale waliompigia kura fisadi Lowasa wameanza kujutia kura zao baada ya kuona kasi ya Raisi JPM!
Mkabila wewe, no doubt.
 
unaweza ukamwambia hivyo moja kwa moja kiwa ni mropokaji? au unaweza kumtumie ujumbe moja kwa moja aupate? kama unaweza poa ila kama huwezi nakishauri tu chuna maneno yako kwa mkuu wa nchi. wengine sisi tutukane tu hatuna shida. sio J.K yule wa kutukanwa na kuchekacheka. nakushauri ndugu yangu. fuata sheria. kosoa toa maoni lakini usimtukane

Nashukuru kwa ushauli ubarikiwe sana
 
Jaman campegne zmekwisha co mda Wa kurumbana ila nahamin kwa style hii inatufikisha mbali tukibaki na vinyongo
 
kama uchaguzi umekwisha tulipaswa kuganga yajayo. maghufuli aamrishe wale wote waliokamatwa wakati wa uchaguzi waachiwe huru ili tusonge mbele vinginevyo bado tutauguza vidonda vya uchaguzi kwa muda wote wa miaka mitano.
Vipi aamrishe wakati yeye sio hakimu, au unafikiri Magufuli anamawazo kama ya Lowassa ya kuingilia kazi za mahakama.
 
Back
Top Bottom