kikoozi
JF-Expert Member
- Jun 24, 2015
- 2,030
- 2,930
Habarini ndugu zangu wana JamiiForums, matumaini yangu mu wazima wa afya tele.
Nisiwachoshe niende kwenye mada moja kwa moja
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28, nimemaliza chuo kikuu mwaka jana. Tangu nimemaliza chuo, nimehangaika sana kupata kazi bila mafanikio. Mwaka huu mwezi uliopita nilibahatika kupata kazi ya kuandikisha wapiga kura kwenye uchaguzi huu wa Serikali za Mitaa.
Baba yangu alikataa kabisa nisijihusishe kwenye mambo yoyote yanayohusiana na siasa kwa hiyo hakupendezwa. Baada ya hilo zoezi la uandikishaji kuisha, juzi Ijumaa kuna mjumbe wa chama cha mapinduzi (CCM) aliniambia kuwa nimtafutie wanachama 20 tu kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi huu wa Serikali za Mitaa, na kuahidi atanipa pesa ya maji.
Pale home jumla tupo watu 7 pamoja na ndugu wengine, nilitaka kwanza kuanza na familia yangu, nilimfuata baba yangu na kumueleza kuwa na yeye awe mmoja wapo katika watu 20 nilioombwa na mjumbe
Ndugu zangu, baba alinitukana matusi mazito, siwezi kuyaandika hapa, mpaka kufikia kuniambia nitakuwa nimelaaniwa na dunia. Kaenda mbali zaidi ananimbia kama ntashilikiana na watu wa CCM na kumhusisha yeye, ataniondoa kwenye nyumba tunayoishi, ukizingatia hiyo nyumba ni ya babu yangu ambaye yeye ni baba yake.
Marehemu babu yangu kabla ya kufariki alisema kabisa na wazi kuwa nisinyanyasike kwenye ule mji. Wakuu, mpaka ninapoandika hapa, baba atoa vitu vyangu nje, anasema nikahamie kwa huyo mjumbe.
Naombeni ushauri wenu wakuu, nataka kuipigania haki yangu, maana babu alisema kile chumba nilichokuwa nakaa ni mali yangu halali.
Nipo katika wakati mkuu, nisaidieni niende polisi au nifanye nini wakuu?
Asanteni.
Nisiwachoshe niende kwenye mada moja kwa moja
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28, nimemaliza chuo kikuu mwaka jana. Tangu nimemaliza chuo, nimehangaika sana kupata kazi bila mafanikio. Mwaka huu mwezi uliopita nilibahatika kupata kazi ya kuandikisha wapiga kura kwenye uchaguzi huu wa Serikali za Mitaa.
Baba yangu alikataa kabisa nisijihusishe kwenye mambo yoyote yanayohusiana na siasa kwa hiyo hakupendezwa. Baada ya hilo zoezi la uandikishaji kuisha, juzi Ijumaa kuna mjumbe wa chama cha mapinduzi (CCM) aliniambia kuwa nimtafutie wanachama 20 tu kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi huu wa Serikali za Mitaa, na kuahidi atanipa pesa ya maji.
Pale home jumla tupo watu 7 pamoja na ndugu wengine, nilitaka kwanza kuanza na familia yangu, nilimfuata baba yangu na kumueleza kuwa na yeye awe mmoja wapo katika watu 20 nilioombwa na mjumbe
Ndugu zangu, baba alinitukana matusi mazito, siwezi kuyaandika hapa, mpaka kufikia kuniambia nitakuwa nimelaaniwa na dunia. Kaenda mbali zaidi ananimbia kama ntashilikiana na watu wa CCM na kumhusisha yeye, ataniondoa kwenye nyumba tunayoishi, ukizingatia hiyo nyumba ni ya babu yangu ambaye yeye ni baba yake.
Marehemu babu yangu kabla ya kufariki alisema kabisa na wazi kuwa nisinyanyasike kwenye ule mji. Wakuu, mpaka ninapoandika hapa, baba atoa vitu vyangu nje, anasema nikahamie kwa huyo mjumbe.
Naombeni ushauri wenu wakuu, nataka kuipigania haki yangu, maana babu alisema kile chumba nilichokuwa nakaa ni mali yangu halali.
Nipo katika wakati mkuu, nisaidieni niende polisi au nifanye nini wakuu?
Asanteni.