Frustration
JF-Expert Member
- Jan 30, 2018
- 3,151
- 4,141
Habari wanajf kwa ujumla. Naomba niende kwenye mada moja kwa moja kwa kuanza kutoa maelezo mafupi.
Mashamba ya familia yangu yapo kijiji jirani na mashamba hayo tuliyapata wakati huo tukiwa kijiji kimoja ila baada ya kujigawa ikawa mashamba yetu yapo kijiji kingine.
Kuna viashiria vya kutosha hadi sasa kwenye mashamba hayo kama vile miembe,mibolea na michungwa iliyopandwa na wazee wetu. Toka tuache kufanyia kazi maeneo yale panakaribia miaka 11 au 12 hadi sasa.
Hivi karibuni nimetembelea nimekuta kuna watu wanafanyia kazi i.e wamelima na nilivyofuatilia nimekuja kujua kuwa mmoja alipimiwa na serikali ya kijiji hekari 10 na wengine wanalima tu bila ya kupimiwa na serikali wala familia haijawapa maeneo hayo kulima.
Familia imewashitaki au kuwalalamikia watu wote waliokutwa katika maeneo hayo katika baraza la usuruhishi la kata kwa kosa la kulima katika maeneo yetu na kukataa kuondoka. Wao wanaeleza kuwa wanalima katika ardhi ya kijiji chao na hawawezi toka.
Mwenyekiti wao aliomba jambo liende kijijini kwakwe kwa usuruhishi zaidi na kata ikatoa siku 15 kusubiri majibu toka serikali ya kijiji jirani. Kuna siku tulialikwa kwenye kikao na tulishindwana kwakuwa wao kama serikali wanakilri kuwa eneo ni letu ila tuliyatelekeza mashamba hayo na hivyo kijiji yameyachukua kwa matumizi yake.
Pia walitushauri kama tunataka ardhi basi tuandike maombi ya kuomba ardhi kwa barua na kijiji kitatupatia kwa sharti la kupatiwa eneo lingine au palepale. Huu kama familia tumeona ni mtego ikiwa tutaandika maombi.
Naombeni ushauri wenu ikiwa serikali ya kijiji na watu wake wanadhamira mbaya na mashamba yetu, naomba muongozo wa kisheria juu ya mambo haya kwani tarehe 26 tunatakiwa tena shaurini.
Niwaombe msamaha kwa uandishi mbaya na mrefu AHSANTENI!
Mashamba ya familia yangu yapo kijiji jirani na mashamba hayo tuliyapata wakati huo tukiwa kijiji kimoja ila baada ya kujigawa ikawa mashamba yetu yapo kijiji kingine.
Kuna viashiria vya kutosha hadi sasa kwenye mashamba hayo kama vile miembe,mibolea na michungwa iliyopandwa na wazee wetu. Toka tuache kufanyia kazi maeneo yale panakaribia miaka 11 au 12 hadi sasa.
Hivi karibuni nimetembelea nimekuta kuna watu wanafanyia kazi i.e wamelima na nilivyofuatilia nimekuja kujua kuwa mmoja alipimiwa na serikali ya kijiji hekari 10 na wengine wanalima tu bila ya kupimiwa na serikali wala familia haijawapa maeneo hayo kulima.
Familia imewashitaki au kuwalalamikia watu wote waliokutwa katika maeneo hayo katika baraza la usuruhishi la kata kwa kosa la kulima katika maeneo yetu na kukataa kuondoka. Wao wanaeleza kuwa wanalima katika ardhi ya kijiji chao na hawawezi toka.
Mwenyekiti wao aliomba jambo liende kijijini kwakwe kwa usuruhishi zaidi na kata ikatoa siku 15 kusubiri majibu toka serikali ya kijiji jirani. Kuna siku tulialikwa kwenye kikao na tulishindwana kwakuwa wao kama serikali wanakilri kuwa eneo ni letu ila tuliyatelekeza mashamba hayo na hivyo kijiji yameyachukua kwa matumizi yake.
Pia walitushauri kama tunataka ardhi basi tuandike maombi ya kuomba ardhi kwa barua na kijiji kitatupatia kwa sharti la kupatiwa eneo lingine au palepale. Huu kama familia tumeona ni mtego ikiwa tutaandika maombi.
Naombeni ushauri wenu ikiwa serikali ya kijiji na watu wake wanadhamira mbaya na mashamba yetu, naomba muongozo wa kisheria juu ya mambo haya kwani tarehe 26 tunatakiwa tena shaurini.
Niwaombe msamaha kwa uandishi mbaya na mrefu AHSANTENI!