Msaada wa Kisheria unahitajika tafadhari

Jokia

Member
Feb 18, 2015
93
178
Habari zenu wakuu,

Mnamo tarehe 09/07/2023 nilifanya muamala kutoka simu yangu kwenda kwenye kampuni moja ya michezo ya kubahatisha 'kubet'.

Ni kampuni kubwa tu kwa hapa Tz. Hiyo fedha haikuingia kwenye akaunti yangu ambayo ipo kwenye hiyo kampuni. Nilifanya nao mawasiliano wakasema kuna tatizo la mfumo kwaiyo fedha itaingia ndani ya saa 48.

Tangu kipindi hicho hadi leo fedha haijaingia na wala haijarudi kwangu na tukiwasiliana majibu yao ni kwamba niwe mvumilivu tu wanashughulikia.

Sasa wakuu, naombeni msaada katika ni kipi nifanye ili nipate haki yangu. Fedha ni nyingi kiasi. Asante
 
Ukimaliza kuwasiliana na kampuni la simu, kama itashindikana au usiporidhika nenda TCRA, usiporidhika tena, utakata rufaa kwenye Fair Competition Tribunal (FCT).
 
Back
Top Bottom