covid 19
JF-Expert Member
- May 9, 2014
- 4,876
- 10,593
Wakuu ipo hivi,
kwetu tulizaliwa wawili tu mimi mkubwa na mdogo wangu wa kike, nipo naishi dodoma pamoja na familia yangu yaani naishi na mke wangu mama na mdogo wangu.
Mzee wangu alifariki miaka 3 iliyopita hivyo aliacha baadhi ya mali km nyumba 3 na mashamba, nyumba mbili zipo dodoma hizi hazina shida wala mashamba tunayamiliki bila shida yoyote balaa lipo kwenye nyumba moja ambayo ipo Dar es Salaam Sinza.
Hapo Sinza ilipo iyo nyumba ndio mzee wangu alipozaliwa kwao walikuwa wawili tu wote wakiume yeye mzee wangu akiwa ni kitinda mimba cha mama yk (bibi yangu). Upande wa ba mkubwa kaka yake mzee yeye anawatoto watatu wawili wa kiume mmja wakike..
sasa ipo hivi mnamo mwaka 2006 bamkubwa na mkewe warifariki kwenye ajali ya basi walikuwa wakiishi kilimanjaro watoto wao walikuwa wakubwa wakujitegemea..hivyo baada ya kufariki wazazi wao watoto waliuza mali moja baada ya nyingine za kwao hadi zikaisha licha ya kuonywa sana na kukalipiwa na mzee..
Sasa ikawa wamebaki mzee wangu na bibi mwaka 2009 mzee aliibomoa nyumba yote ya bibi maana ilikuwa ni zile nyumba za udongo zilizopo mjini alijenga nyumba mpya na kisasa kabisa pale kwa bibi (mama yk) kwa muda mfupi nakumbuka maana hapo nilikuwa nae mzee kipindi tunasimamia ujenzi. kwa kweli bibi na mzee wangu walifurahi sana, mwaka 2012 bibi nae akafariki hivyo mzee wangu akawa kabaki mwenyewe kwao.
Kwakuwa alijua tabia za watoto wa kaka yk za tamaa hakuwaruhusu wale watoto kukaa pale badala yk mzee aliweka wapangaji na kuacha viumba viwili kwa ajili ya kufikia endapo ndugu yyte ataenda dar basi maisha yameenda hivyo mwaka 2017 mzee nae alifariki sasa tumebaki watoto na mama..
Process za mirathi tulifanya na msimamizi wa mali hizo ni bi mkubwa pamoja na nyumba ya sinza ambapo kwenye mirathi imeandikishwa km mali ya mzee wangu, mwaka jana mtoto mmoja wa bamkubwa alihamia hapo sinza familia yk bila ya kuomba ruhusa kwa mama kwa kuwa ni ndugu hatukuwa na wasiwasi maana tuliambiwa alikuwa na hali ngumu kiuchumi..
Sasa ndugu hawa wanadai nyumba bora iuzwe maana wao hawana faida nayo ingawa wanaishi bure kodi za wapangaji hawapokei wao wakati eneo ni la bibi na baba yao anayo haki hapo.
Wakuu hili swala limetuvuruga hapa home.... kisheria tena za mirathi limekaaje hili kabla hatujafanya maamuzi magumu...
naombeni ushauri wenu maan mm ndio nategemewa nimpe mwongozo bi mkubwa nimestuck..
kwetu tulizaliwa wawili tu mimi mkubwa na mdogo wangu wa kike, nipo naishi dodoma pamoja na familia yangu yaani naishi na mke wangu mama na mdogo wangu.
Mzee wangu alifariki miaka 3 iliyopita hivyo aliacha baadhi ya mali km nyumba 3 na mashamba, nyumba mbili zipo dodoma hizi hazina shida wala mashamba tunayamiliki bila shida yoyote balaa lipo kwenye nyumba moja ambayo ipo Dar es Salaam Sinza.
Hapo Sinza ilipo iyo nyumba ndio mzee wangu alipozaliwa kwao walikuwa wawili tu wote wakiume yeye mzee wangu akiwa ni kitinda mimba cha mama yk (bibi yangu). Upande wa ba mkubwa kaka yake mzee yeye anawatoto watatu wawili wa kiume mmja wakike..
sasa ipo hivi mnamo mwaka 2006 bamkubwa na mkewe warifariki kwenye ajali ya basi walikuwa wakiishi kilimanjaro watoto wao walikuwa wakubwa wakujitegemea..hivyo baada ya kufariki wazazi wao watoto waliuza mali moja baada ya nyingine za kwao hadi zikaisha licha ya kuonywa sana na kukalipiwa na mzee..
Sasa ikawa wamebaki mzee wangu na bibi mwaka 2009 mzee aliibomoa nyumba yote ya bibi maana ilikuwa ni zile nyumba za udongo zilizopo mjini alijenga nyumba mpya na kisasa kabisa pale kwa bibi (mama yk) kwa muda mfupi nakumbuka maana hapo nilikuwa nae mzee kipindi tunasimamia ujenzi. kwa kweli bibi na mzee wangu walifurahi sana, mwaka 2012 bibi nae akafariki hivyo mzee wangu akawa kabaki mwenyewe kwao.
Kwakuwa alijua tabia za watoto wa kaka yk za tamaa hakuwaruhusu wale watoto kukaa pale badala yk mzee aliweka wapangaji na kuacha viumba viwili kwa ajili ya kufikia endapo ndugu yyte ataenda dar basi maisha yameenda hivyo mwaka 2017 mzee nae alifariki sasa tumebaki watoto na mama..
Process za mirathi tulifanya na msimamizi wa mali hizo ni bi mkubwa pamoja na nyumba ya sinza ambapo kwenye mirathi imeandikishwa km mali ya mzee wangu, mwaka jana mtoto mmoja wa bamkubwa alihamia hapo sinza familia yk bila ya kuomba ruhusa kwa mama kwa kuwa ni ndugu hatukuwa na wasiwasi maana tuliambiwa alikuwa na hali ngumu kiuchumi..
Sasa ndugu hawa wanadai nyumba bora iuzwe maana wao hawana faida nayo ingawa wanaishi bure kodi za wapangaji hawapokei wao wakati eneo ni la bibi na baba yao anayo haki hapo.
Wakuu hili swala limetuvuruga hapa home.... kisheria tena za mirathi limekaaje hili kabla hatujafanya maamuzi magumu...
naombeni ushauri wenu maan mm ndio nategemewa nimpe mwongozo bi mkubwa nimestuck..