Msaada tafadhali: Mama ni mchawi

Msaada tafadhali: Mama ni mchawi

Bujibuji Simba Nyamaume

Platinum Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,662
Reaction score
161,660
Amedondoka huko kwenye kanisa la kilokole akiwa mtupu na amekiri kuwa yeye ni kiongozi wa kundi lao.
Jambo hili limeniletea mfadhaiko na kuniathiri kisaikolojia.
 
Ungesema ni mwanga ungeeleweka zaidi tambua kuwa neno "mchawi" maana yake ni mtu mwenye roho mbaya
 
Mama ni mama kubaliana na hali yake alivyo yawezekana nawe kaisha kuambukiza
 
Pole sana! Ila kumbuka kuwa mama ni mama! Wapaswa kumheshimu na kumpenda ili uishi siku nyingi na heri duniani!
 
Maelekezo ya MUNGU kwa Musa "Usimwache mwanamke mchawi kuishi"

Timiza wajibu wako haraka.
 
jogi mbona unataka kumpoteza mwenzako.
 
Last edited by a moderator:
Kaa nae chini,mwambie kiunyenyekevu kabisa jins alivyoitia aibu familia yenu na wewe hapo,na mwisho muuluze ana mkakati gani wa kuacha uchawi,ingawa hawezi kukubali kwa urahisi,lakini mdogo mdogo anaweza kukuelewa,pole sana kiongozi,maalim MziziMkavu anaweza kukusaidia zaidi
 
Last edited by a moderator:
Wewe jamaa huna akili kabisa, sasa hata kama ni kweli unategemea msaada gani hapa jf
 
Mwambie aache lasivyo atarithisha mtoto wako wajukuu xake kama wewe umepona
 
Pole mkuu ila angalia isije ikawa mizimu imekuchagua ww kirithi mikoba, jisalimishe haraka kwa Mungu!
 
Kama amesha mpaka cheo, huko humtoi ila kaa mbali nae hakikisha ile biashara ya kupeleka wajukuu kwa bibi wakati wa likizo inakoma..
Kumbuka mpaka hapo alipofika kala wa wenzake sana na zamu yake ya kutoa nyama ikifika atatoa humo humo ndani ya familia ...
 
Usimuache mtu mchawi aishii....angekua wa ukoo wetu tungeshamchoma sindano ya sumu....
 
Mmmmh!!!!!!!!!! siamini hata kidogo, akulee toka unavaa nepi hadi ufikie kujitegemea ndio ujue ni mchawi, nina mashaka hata na hilo kanisa aliloangukia, siku hizi kuna watumishi niwachonganishi na wanaogofya watu kisaikolojia kiasi yeye akianza kuuliza mtu anabaki anajibu kila kitu ndio.

Kama kweli usemayo Utakumbuka maneno yangu siku moja, ila kama ni changamsha genge hujamtendea haki mama yako.
 
Dawa Yake Ww Mpokee Yesu Kuwa Bwana Na Mwokoz Wako, Maana Kuanzia Hapo Ndipo Hata Ukikemea Maneno Yako Yatakuwa Na Nguvu
 
Kama ni mkirsto anza maombi mungu atajibu sala zako.Pole Sana
 
Back
Top Bottom