Msaada Samsung galaxy s2 imezima ghafla

Msaada Samsung galaxy s2 imezima ghafla

koo

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2011
Posts
258
Reaction score
67
Heshima mbele

Naomba msaada sim yangu tajwa hapo juu niliiweka mfukon kutoa ikawa imezima kuiwasha haiwaki nimeweka kwenye umeme usiku kucha bado haiwaki naomba msaada nifanyeje haijawahi kuanguka wala kuingia kwenye maji nahisi ni virus lakin nashindwa nawezaje kuiscan kama haiwaki

naomba msaada jamani.
 
Haijaribu kabisa kuwaka, au inaishia njiani kabla ya kuload icons?
 
Toa betri kisha irudishie ndo uwashe au uchomeke charger..hata mi nna s2 na huwa inanitokeaga sometimes..
 
Toa betri kisha irudishie ndo uwashe au uchomeke charger..hata mi nna s2 na huwa inanitokeaga sometimes..

Nimetoa na kuweka hamna kitu mpaka naandika hapa iko kwenye umeme na haijigusi hata kutoa mwanga kwa mbali
 
kaka by any chance ulishawah kueka usb debuging on? kama hujui hata ni nini ipotezee.

umejaribu kuconect na pc inadetect?
 
Mkuu kwa ushauri wangu, Kuna uwezekano kwamba kuna app uliyoinstall ambayo inazuia simu kuwaka. Jaribu kuingia kwenye Recovery mode halafu uirestore factory settings. Hii imewahi kutokea kwenye android yangu.
 
Tumia computer charger cable ili uingie kwenye desktop mode. Uangalie kama itarespond.

Wakati mwingine nahisi gadgets zinachanganyikiwa shauri ya kuwa overworked. Itoe betri uiache usiku kucha then asubuhi uiwashe.
 
Ipeleke kwenye maduka ya samsung kama upo mjini dar es salaam wik nzima hii sumsung wanatoa huduma kwa wateja wao
 
kaka by any chance ulishawah kueka usb debuging on? kama hujui hata ni nini ipotezee.

umejaribu kuconect na pc inadetect?

Nimechomeka kwenye pc yani haijigusi hata chembe na kwenye pc haisomi kama kuna kitu kimeingia yan ninyeusii haina chochote inafanya nimejaribu kubonyeza kitufe chakuongezea sauti+home+chakuwashia hamna kitu
 
Ipeleke kwenye maduka ya samsung kama upo mjini dar es salaam wik nzima hii sumsung wanatoa huduma kwa wateja wao

Niko mkoa wa pembezoni sana kufika dar itanichukua zaidi ya wiki nikiwa bado njiani hasa kwa treni za sikuhizi hazina uhakika sawia
 
Tumia computer charger cable ili uingie kwenye desktop mode. Uangalie kama itarespond.

Wakati mwingine nahisi gadgets zinachanganyikiwa shauri ya kuwa overworked. Itoe betri uiache usiku kucha then asubuhi uiwashe.

Haisomi kwenye computer sijui hata nitaingiaje
 
Mkuu kwa ushauri wangu, Kuna uwezekano kwamba kuna app uliyoinstall ambayo inazuia simu kuwaka. Jaribu kuingia kwenye Recovery mode halafu uirestore factory settings. Hii imewahi kutokea kwenye android yangu.

Najaribu kubonyeja kitufe cha sauti+home+power haitikisiki labda kama kunanjia nyingine naomba unisaidie mkuu
 
Hata mimi SGS2 yangu ilikufa bila sababu. Nimeamua kununua simu nyingine na wala si Samsung tena!
 
Kuna jamaa alikua anatafuta simu humu, nikamshauri anunue simu yoyote kasoro sgs2 watu hawakunielewa. Tunavyoongea hapa ninazo sgs2 tatu zote zina tatizo hilo hilo! Peleka kwa fundi ndio the only solution.
 
Nimeunganisha yangu na pc na kubonyeza power+volume buttons....naiskia sauti tu kutoka kwenye pc kama vile kuna connection, lakini zaidi ya hapo hakuna kitu!
 
Nimeunganisha yangu na pc na kubonyeza power+volume buttons....naiskia sauti tu kutoka kwenye pc kama vile kuna connection, lakini zaidi ya hapo hakuna kitu!

jaribu kudownload odin kwenye pc ukiona inaonesha rangi ya blue na kuandika com kwenye odin ujue kuna mawasiliano kat ya pc na simu hivyo inaweza download firmware na kuflash simu
 
Najaribu kubonyeja kitufe cha sauti+home+power haitikisiki labda kama kunanjia nyingine naomba unisaidie mkuu
Ama kuna shock imetokea kwenye device yako, Tafuta fundi mtaalamu hapo eneo unaloishi akuchekie, Na maybe ni battery.
 
Back
Top Bottom