Msaada please. Nimeagiza Gari kutoka Singapore

Hello Gentleman and Ladies mmeshindaji wanandugu?
Naomba kuuliza Kwa anayejua ,Nimeagiza Gari aina ya suzuki escudo ya mwaka 2007 kutoka Singapore .Kwa bahati mbaya nchini Singapore hawana Wakala wa TBS Kwa ajili ya inspection. Na meli yenyewe inaingia Dar tarehe 28 mwezi huu.Je Kwa Tanzania nitafanyaje ili Gari iweze kufanyiwa inspection please. Na itakuwa vizuri zaidi kama Kuna mtaalamu ambaye anajua gharama za inspection please naomba msaada wenu Wana ndugu zangu .

Kiongozi...naomba uniangalizie land cruiser hardtop pick up macho ya panzi ama ya kawaida huko singapore ya 2000, 2005,2007 or 2010. Bei yake na iwe ktk hali nzuri sana isiwe imepata ajali wala kufunguliwa injini. Pls mkuu naomba unifanyie hiyo kazi tufanye biashara.
 
Singapore magari bei rahisi sana


Mkuu Bujibuji kwema baba!!! naomba uniangalizie land cruiser hardtop pick up macho ya panzi ama ya kawaida huko singapore nasikia rahisi mno babaa..ya 2000, 2005,2007 or 2010. Bei yake na iwe ktk hali nzuri sana isiwe imepata ajali wala kufunguliwa injini. Pls mkuu naomba unifanyie hiyo kazi tufanye biashara.
 
Haswaaa mimi nimenunua mark x Singapore mwezi wa 8 na inspection nimefanyia pale chuo cha usafirishaji ongea na agent wako ila utatakiwa kulipia km 344000tsh za ukaguzi TBS na kama gari yako itakutwa na kasoro flani utapewa mwezi mmoja kurekebisha halaf upeleke tena TBS... ila zingatia unapopeleka usibandike plate number
Asante sana broo
 
Mama yangu! Mkuu, kama gari haijafanyiwa inspection utatakiwa kulimwa fine ya 30% ya CIF ya gari. Cha kufanya pale gari itakapo ingia, ongea na agent wako aweze kupenyeza rupia (kuhonga) ili gari ipite bila inspection. Yani hapo andaa kati ya laki tano hadi saba hivi. Zamani tulikuwaga tunapenyeza (tunahonga) laki mbili na nusu ila serikali ilipozidisha ukali tukawa tunahonga hadi laki tano na zaidi. Niliwahi kuleta gari bila inspection nikatakiwa nihonge milioni moja, nikawabembeleza weee nikaishia kukata kama laki tano hivi...
Waswahili wanasema, kwenye udhia penyeza Rupia~ Samaia (ufunguzi wa Mloganzila)
Hoja yako hii kwa mimi nikiitizama kwa umakini sana naona imekaa kipelelezi hivi sijui lakin.
 
Haswaaa mimi nimenunua mark x Singapore mwezi wa 8 na inspection nimefanyia pale chuo cha usafirishaji ongea na agent wako ila utatakiwa kulipia km 344000tsh za ukaguzi TBS na kama gari yako itakutwa na kasoro flani utapewa mwezi mmoja kurekebisha halaf upeleke tena TBS... ila zingatia unapopeleka usibandike plate number
aisee mkuu ulitumia njia gani kuweka order ya hiyo gari
 
Back
Top Bottom