Msaada: Nini maana ya treasury bill (hati fungani)?

Msaada: Nini maana ya treasury bill (hati fungani)?

NImelisikia sana hili neno kwenye Tegeta-Escrow. Je, kwa kiingereza linaitwaje?
 
Hatifungani in english is known as BOND'bond is the face value certificate of loan to the government issued through discounted bills.sometimes the goverment may having a shortage of funds so it issue bonds to the public to raised fund to finance a concernd issue
 
sina hakika kama ni jukwaa sahihi,lakini kwa kuwa ni hoja mchanganyiko panaweza kufit hoja yangu,
hivi karibuni tu kuna msemo ambao umeanza kupata umaarufu hata bungeni unatumika,'hati fungani'hili neno limeniacha kidogo,japo linahusika na masuala ya kibenki,mwenye aidia nalo naomba msaada.
 
Bid bond/Bank Guarantee/Advance payment bond etc. ndio nadhani hio ndio hati fungani. Zinatumika zaidi kwenye contracts/Tenders etc.
 
Hati fungani au Bond(kwa kiingereza) ni utaratibu unaotumiwa na makampuni au serikali kukopa pesa kutoka kwa wananchi. Wale wanaonunua hizi hati wanakuwa wakopeshaji wa hiyo kampuni, kwa maana kwamba badala ya kampuni kukopa pesa benki, wanaweka utaratibu wa kuwawezesha wananchi kutoa pesa kwa makubaliano ya kuwarudishia hiyo pesa yao pamoja na riba kwa muda maalum.

Hati fungani inaweza ikatolewa na serikali kuu(Government bond), serikali za mitaa( Municipal bond), kampuni(corporate bond) au serikali ya nchi za nje(Euro bond).

Hati fungani utofautiana na hisa(share) kwa maana kwamba wenye hisa ndo wenye kampuni(debtors) kwa hiyo wao wanalipwa faida pale ambapo kampuni imepata faida na pesa yao hukatwa pale ambapo kampuni imepata hasara wakati wenye hati fungani ni wakopeshaji(creditors) kwa hiyo wao kulipwa faida haijalishi kampuni imepata hasara au la.
 
Hati fungani au Bond(kwa kiingereza) ni utaratibu unaotumiwa na makampuni au serikali kukopa pesa kutoka kwa wananchi. Wale wanaonunua hizi hati wanakuwa wakopeshaji wa hiyo kampuni, kwa maana kwamba badala ya kampuni kukopa pesa benki, wanaweka utaratibu wa kuwawezesha wananchi kutoa pesa kwa makubaliano ya kuwarudishia hiyo pesa yao pamoja na riba kwa muda maalum.

Hati fungani inaweza ikatolewa na serikali kuu(Government bond), serikali za mitaa( Municipal bond), kampuni(corporate bond) au serikali ya nchi za nje(Euro bond).

Hati fungani utofautiana na hisa(share) kwa maana kwamba wenye hisa ndo wenye kampuni(debtors) kwa hiyo wao wanalipwa faida pale ambapo kampuni imepata faida na pesa yao hukatwa pale ambapo kampuni imepata hasara wakati wenye hati fungani ni wakopeshaji(creditors) kwa hiyo wao kulipwa faida haijalishi kampuni imepata hasara au la.
asante sana mkuu.. barikiwa sana
 
Hatifungani in english is known as BOND'bond is the face value certificate of loan to the government issued through discounted bills.sometimes the goverment may having a shortage of funds so it issue bonds to the public to raised fund to finance a concernd issue
Mkuu ungeandika kiswahili tu....
 
Hii ni mikataba ya muda mfupi(Isiyozidi mwaka mmoja) kati ya pande mbili, mara nyingi huwa kati ya serikali na mtu binafsi au shirika ambapo serikali hupewa fedha kiasi fulani na kuahidi kukirudisha kiasi hicho pamoja na riba kiasi fulani katika kipindi maalum kisichozidi mwaka mmoja.

Kwa mfano serikali inaweza kuahidi kwamba itatoa shilingi mia moja na kumi katika kila shilingi mia moja iliyochukua kwa mtu binafsi au shirika fulani baada ya kipindi cha miezi mitatu, hapo ndiyo utamsikia mtu anasema hati fungani yangu imekaribia kuiva inapokaribia miezi mitatu kuisha.

NB: Urefu wa mikataba hii utegemea na miundo ya serikali yaweza kuwa miezi mitatu, miezi sita, miezi tisa au mwaka mmoja. However, mkataba zaidi ya mwaka huitwa Government Bond.
Upo vizuri mkuu maelezo yako.
Ila kwenye muda huwa inategemea na Serikali jinsi ilivyopanga muda wa kurudisha hizo pesa na ukubwa wa riba kulingana na muda wa kuiva kwa hati fungani.
 
Nimeona niifufue hii mada ili tujifunze zaidi, ili mtanzania wa kawaida anunue treasury bills au bonds anatakiwa kuwa na sh. Ngapi? Pia napenda kufahamu huwa zinatangazwa kuuzwa kupitia chombo gani cha habari?
 
Nini maana yake? Hapa naona umuhimu wa shule...
 
Kwa mwenye uelewa wa masuala ya kiuchumi na kiuhasibu, hivi hati fungani ni nini? Na inaivaje ivaje?
 
Pale hati fungani zilizoiva inapogeuka kuwa mapayo ya serikali
 
Hela inapokuwa nyingi katika uchumi/ mzunguko inapelekea mfumuko wa bei. Ili kuleta stability ktk macro economy kwa kupunguza mfumuko wa bei, serikali inatumia Monetary na Fiscal Instruments au policies.
Fiscal instrument 1wapo ni Treasury Bills ambapo Serikali ina issue treasury bills kwa public, public inanunua hzo bills na kwa kuspend hela kufanya manunuzi hayo, hela inapungua ktk mzunguko na kwa ushrkiano na sera nyingne za fedha na kodi mfumuko wa bei hatimaye unapungua, stability inakuwa restored ktk macro economy.
Kwa ufupi serikali inapo issue treasury bills ina borrow/ina kopa frm the public.

Wewe unaponunua Treasury Bill, unauziwa kwa bei pungufu (discounted price). Bdae iki mature (muda wa serikali kuinunua kutoka kwako ukifika) serikali inainunua kwa bei halisi ya treasury bill hyo (face/par value). Faida kwako inakuwa tofauti kati ya discounted price na par value ya treasury bill hyo.
Tuliosoma engineering hapa tunaona nyota tu, ngoja niende lunch nikirudi nitasoma tena
 
Hela inapokuwa nyingi katika uchumi/ mzunguko inapelekea mfumuko wa bei. Ili kuleta stability ktk macro economy kwa kupunguza mfumuko wa bei, serikali inatumia Monetary na Fiscal Instruments au policies.
Fiscal instrument 1wapo ni Treasury Bills ambapo Serikali ina issue treasury bills kwa public, public inanunua hzo bills na kwa kuspend hela kufanya manunuzi hayo, hela inapungua ktk mzunguko na kwa ushrkiano na sera nyingne za fedha na kodi mfumuko wa bei hatimaye unapungua, stability inakuwa restored ktk macro economy.
Kwa ufupi serikali inapo issue treasury bills ina borrow/ina kopa frm the public.

Wewe unaponunua Treasury Bill, unauziwa kwa bei pungufu (discounted price). Bdae iki mature (muda wa serikali kuinunua kutoka kwako ukifika) serikali inainunua kwa bei halisi ya treasury bill hyo (face/par value). Faida kwako inakuwa tofauti kati ya discounted price na par value ya treasury bill hyo.
Kwahiyo CAG Assad ni mbumbumbu kiasi cha kushindwa kutambua uwepo wa hati fungani zilizoiva..
 
Hela inapokuwa nyingi katika uchumi/ mzunguko inapelekea mfumuko wa bei. Ili kuleta stability ktk macro economy kwa kupunguza mfumuko wa bei, serikali inatumia Monetary na Fiscal Instruments au policies.
Fiscal instrument 1wapo ni Treasury Bills ambapo Serikali ina issue treasury bills kwa public, public inanunua hzo bills na kwa kuspend hela kufanya manunuzi hayo, hela inapungua ktk mzunguko na kwa ushrkiano na sera nyingne za fedha na kodi mfumuko wa bei hatimaye unapungua, stability inakuwa restored ktk macro economy.
Kwa ufupi serikali inapo issue treasury bills ina borrow/ina kopa frm the public.

Wewe unaponunua Treasury Bill, unauziwa kwa bei pungufu (discounted price). Bdae iki mature (muda wa serikali kuinunua kutoka kwako ukifika) serikali inainunua kwa bei halisi ya treasury bill hyo (face/par value). Faida kwako inakuwa tofauti kati ya discounted price na par value ya treasury bill hyo.
huwa mnada unafanyika wapi? huwa wanatangaza wapi hayo mauzo? Swali kwa niaba ya Saint Kayumba wote
 
Kwa ninavyojua mimi, hati fungani ni hati inayotolewa baada ya maharusi kumaliza fungate. Ndo wanapewa hiyo hati fungani na mkemia mkuu.... Ila sijui. Nimetoa tu maoni yangu jamani, aah
 
Back
Top Bottom