Msaada: Natafuta annointing water ya T.B Joshua

Msaada: Natafuta annointing water ya T.B Joshua

Ndugu Wana jf naomba kwa wanaoishi daslam mnielekeze wapi ntapata anointing water ya good morning, ya T. B Joshua anaejua hela ni pesa ngapi nisaidieni jamani nina shida na imaniyangu inaamini kupitia anointing water.
Huu nao ni aina ya ushirikina!
 
Nendajengo la Benjamin mkapa tower,posta mpya,ukiuliza hapo ghorofa za chini utampata wa kukuelekeza,mengine ya bei utayakuta huko huko,ni dsm
Sasa haya maji huwasaidia nini? Kwanini usichote yako ukaya swalia? Kuna mstari mwembamba sana kati yenu na washirikina maana wote mnaabudu wanadamu ..! Kwani nyie hamuwezi kuswalia maji au hamna imani? Wajinga ndio waliwao...biashara hiyo...
Nenda Benjamin Mkapa Tower pale Posta, uliza pale receiption first floor watakuonyesha ofisi yao ilipo . Mara ya mwisho bei ilikuwa ni $50. Jitahidi ufike kabla ya saa nne asubuhi kwani wana muda wao wa kazi
 
Ahaaahaaa babu jinga inama ufikiri mali yako inaliwa
 
Huyo T.B joshua mwenyewe ana kesi ya kujibu kafubguliwa Nigeria baada ya jengo lake kuanguka na kuua watu wengi wakiwa waafrica kusini. Sasa anashindwa kujua jengo lake litaanguka ila anajua ya watu. Au ndio mganga hajigangi? unamkuta mtu mzinifu, anavaa nusu uchi halafu anakwambia nakemea mapepo wakati yeye mwenyewe pepo
 
Sasa haya maji huwasaidia nini? Kwanini usichote yako ukaya swalia? Kuna mstari mwembamba sana kati yenu na washirikina maana wote mnaabudu wanadamu ..! Kwani nyie hamuwezi kuswalia maji au hamna imani? Wajinga ndio waliwao...biashara hiyo...

Mkuu, ukishangaa ya Musa utaona ya Firaun!

Gharama ya 'annointing water' ya TB Joshua hiyo ni cha mtoto. Hujasikia ya Mwingira wa Efatha? Kwenye kusanyiko mwaka huu kawauzia waumini wake kitabu chake kwa gharama zaidi ya sh. milioni moja, eti anayekinunua na kukisoma atafunguliwa shida zake zote!

Watu wanapigwa pesa kama hawana akili nzuri huku mtume na nabii akitajirika!

Nyie kondoo amkeni mnadunishwa kwa mafundisho feki. Someni Isaya 10:1-5!
 
Daaaaah hii hatareeee kwa hyo kama hauna ela unakufa na matatzo yako WATU WANGU WANAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA
 
Hakuna anointed water,yote biashara kaka,huyu t .b Joshua sijui kaipata wapi utume,anatumia majini tu kufanikisha kazi zake
 
Jaman shida nn? Mimi ndo ntayanunua na Kuya tumia nyinyi hamuwezi acheni vp Jaman
 
Mbeya yana patikana makunguru barabara iendayo ilemi darajani uliza kwa mtumishi
 
Lazima ulipie ivivu wako wa kumtafuta Mungu.
Wakristo ndo maana tunabezwa na waislam,,uvivu. Mtafuteni Bwana maadam anapatikana,mwiteni maadam yu karibu
 
Nimekupenda..vile vile kwa utafiti wangu mtu akiingia humo huneemeka kwa muda mwishowe atatoka akiwa masikini wa kutupwa na mapepo juuu
 
Asante kwa wote walio nielekeza kesho tu naenda kuyachukua kwa gharama yoyote.
 
Acheni kuwa na imani haba enyi wanadamu. Biblia inasema "Watu wangu wanaangamia kwa kukisa maarifa" lakini Pia amelaaniwa amtumainiaye mwanadamu...." Yaani unashindwa kuingia faragha ukamweleza Muumba wako shida zako! Wewe mkristo gani!!Aibu kweli...
 
Yaani bado mtu anaamini maji sijui ya ipako?

Interesting....!
 
Ndugu Wana jf naomba kwa wanaoishi daslam mnielekeze wapi ntapata anointing water ya good morning, ya T. B Joshua anaejua hela ni pesa ngapi nisaidieni jamani nina shida na imaniyangu inaamini kupitia anointing water.

Hili nalo n jipu linaitaji kutumbuliwa.
 
Sasa haya maji huwasaidia nini? Kwanini usichote yako ukaya swalia? Kuna mstari mwembamba sana kati yenu na washirikina maana wote mnaabudu wanadamu ..! Kwani nyie hamuwezi kuswalia maji au hamna imani? Wajinga ndio waliwao...biashara hiyo...

Tatizo ukishavuta hujifichi
 
Back
Top Bottom