Ushuhuda wa mke wangu kupona COVID19 baada ya kumuombea kwa kutumia medium ya new annointing water ya TB Joshua

Leslie Mbena

JF-Expert Member
Nov 24, 2019
207
677
USHUHUDA WA MKE WANGU KUPONA COVID 19 BAADA YA KUMUOMBEA KWA KUTUMIA MEDIUM YA NEW ANNOINTING WATER YA TB JOSHUA.

Leo 22:30hrs 20/01/2021

Bwana Yesu atukuzwe ndugu zangu,Namshukuru Mungu kwa sababu ya neema yake kuu juu yangu na Familia yangu,Jina langu ni Leslie Mbena,Mume na Baba wa watoto wawili,Mke wangu Elizabeth Benzege ni mjamzito tena wa mtoto wetu wa tatu,tukiwa katika mwezi huu wa mwisho kabla ya kujifungua,Mke wangu alianza kukohoa wiki moja iliyopita,wote tulifikiri ni kikohozi cha kawaida,hali ikaendelea kwa wiki nzima na ndipo alipoanza kukohoa hadi kuishiwa nguvu,tukaenda hospital wakampima mapafu na wakakuta tayari mapafu yake yameshaharibika na ndio inasababisha tatizo la upumuaji yaani Covid 19.

Nauweka Ushuhuda huu mtandaoni kama ulivyo ili uwasaidie watu waliokosa tumaini baada ya kuugua Covid 19,wajue kwamba lipo tumaini kwa Bwana Yesu kwa kila anayeamini na kuamua kumtii Mungu katika maisha yake yote.Tulilazwa katika wodi private floor ya tatu katika Hospital ya Bochi,nawashukuru manesi na madaktari kwa huduma yao nzuri pasipo unyanyapaa,kwani walitupokea wakamchoma sindano na dawa nyingi mchanganyiko sawa sawa na dalili zilizokuwa zinaonekana kwa mgonjwa,kila daktari aliyekuja alishika file la Mke Wangu akatoa ushauri,kuongeza au kupunguza dawa,ahsante kwa manesi ambao walipoona hali ya Mke wangu inazidi kuwa mbaya walileta maji ya moto na kumkanda mwili mzima,ahsante pia kwa wataalamu wa viungo waliotoa mazoezi kwa mgonjwa wakati wa oxygen hata baada ya kutolewa oxygen,hali ya upumuaji ilipozidi kuwa mbaya daktari alishauri mgonjwa awekewe oxygen,

Baada ya kulazwa tukauanza usiku ambao ulikuwa mbaya kwangu na kwa Mke wangu,mitungi miwili ya oxygen ikawekwa pembeni ya kitanda cha Mke wangu akawekewa oxygen puani,ikaletwa na mashine ambayo ilikuwa inasoma upumuaji katika mwili wa Mke Wangu,baadhi ya watu waliniambia kuna mawili mtu akiwekewa oxygen ni either apone au apumzike milele,hofu iliniingia,Mke Wangu ambae alikuwa bado anajitambua nae alianza kutoa machozi akiwa pale kitandani walipomuwekea oxygen,uwezo wetu wa kibinadamu uliishia hapo,na hapo uwezo wa Mungu kuingilia kati ndio ungemwokoa Mke Wangu,nilijua kabisa tayari roho wa umauti ameshaingia katika familia yangu,usiku wa kwanza ukapita,tukaamka siku ya pili.

Mashine ya kupima upumuaji katika mwili wa Mke Wangu ilikuwa inapanda na kushuka,wakati wote huo niliomba na kurudia ombi hilo hilo moja,Mungu mponye Mke Wangu,Mungu mponye Mke Wangu, ahsante kwa Mama yangu ambae alikesha akituombea,ahsante kwa Mama yangu mdogo,ndugu zangu wote,familia yangu yote na familia ya Mke wangu,jamaa na marafiki ambao wote walipiga simu kutuombea,usiku wa siku ya pili mashine ya kupima upumuaji ilishuka hadi 75,tukumbuke normal ya upumuaji kwa mwanadamu ni 90 hadi 100,mashine inaposhuka chini ya 80 alarm na taa nyekundu uanza kuwaka,manesi waliingia na kutoka na wakaja na dktari,wapo walioshauri tupewe referral kwenda hospital kubwa ya juu ya Mloganzika au Muhimbili,uko nilikataa maana tungeenda uko tungetelekezwa kwa sababu uko wagonjwa ni wengi,wakatuacha.

Siku ya tatu hali iliendelea kuwa mbaya,nikaanza kutafuta namba ya Emmanuel tv partners,niliwahi kusave kwenye simu yangu lakini sikuipata,nakumbuka wiki moja kabla hajaumwa Mke Wangu,nilimtuma aende posta,ghorofa la Benjamin Mkapa kuna ofisi ya Emmanuel tv partners akaombe New Annointing water wammiminie kwenye chupa ya maji,alikwenda kwa bahati mbaya alikuta wamehama,na wamehamia Kawe,hali ilivyozidi kuwa mbaya niligoogle prayer for viewers Tb Joshua ikaja sala ya Covid 19 Honduras,nikabonyeza na kuanza kuomba pamoja nayo,baadae akili ikanijia yupo Mwalimu wangu wa Masters pale Mzumbe University aliwahi kunipa Annointing Water,nikaanza kutafuta namba ya Dr Andrew Mushi (PhD) nikaipata nikamtumia sms, Daktari nina shida ya Annointing Water,Mke Wangu yupo kwenye critical condition due to Covid 19, Daktari alinipigia mara moja,nikajitambulisha, akaniambia yeye hana maana wamepewa watu wachache akaniahidi kuulizia,

Baadae Dr Mushi akanipigia akaniambia amepata kwa Mzee Bukozo ambae nae alipewa kidogo na Emmanuel tv partners, akaniambia niende kwake akanimiminie kidogo kwenye chupa ya maji safi ya Kilimanjaro,nikaenda hadi kwa Mzee Bukozo akanipokea akanihubiria, akaniambia nimweleze kidogo nilivyoijua Emmanuel tv na Tb Joshua,nilianza kueleza lakini nilimweleza Annointing water ilivyonisaidia hapo kabla hata sasa,kwa hakika nililia hadi sauti ikashindwa kutoka na Mzee Bukozo akaniambia nenda kaspray Annointing water ukimuombea,akaspray hewani akakemea,in the name of Jesus,you Covid 19 be washed away from this family,you spirit of death out in the name of Jesus, akaniambia nenda kijana,She is healed,nikasema Amen,huku nalia,kwa hakika ndugu msomaji kile kilio changu kilimaliza pale,na msiba wangu uliisha pale nilipoambiwa nenda kijana,She is healed in Jesus name.

She is healed in the Mighty Name of Jesus Christ of Nazareth.
Amen,Soma mistari ifuatayo katika Biblia.

1. Walawi 19: 1 - 2,
2. 1Petro 1: 14 - 16,
3. Yohana 14: 15,
4. Yakobo 2: 10 - 11,
5. 1Yohana 3: 22 - 24,
6. 1Yohana 4: 7 - 8,
7. 1Yohana 5: 18 - 19,
8. Wagalatia 5: 19 - 21 & 22 - 25,
9. Wafilipi 1: 20 - 21,
10. Marko 11: 23 - 25,
11. Matendo 19: 11 - 12,

Kumbuka, muujiza ni siri ya Mungu, Naye siri hiyo huwaonesha marafiki zake ambao ni watakatifu wanaotembea!

Ukiyiishi mistari hiyo hapo juu, wewe ni mtakatifu!Endelea kuomba na pia hata yeye mwenyewe umhubirie Neno la Mungu ili asipoteze uponyaji wake!

Brethren,ilikuwa mchana wa saa saba nilipopewa New Annointing water nikaenda moja kwa moja hospital,nilimkuta mdogo wangu wa kike aitwae Juliana, nikamwambia tumwombee Mke Wangu,Nikamgusa mgongoni Mke Wangu akiwa na oxygen nikamwambia tuombe,Masikio yake yalisikia japo alikuwa amelala,Mungu tunakija mbele zako kuomba uponyaji wa Mke Wangu Elizabeth,kama ulivyomponya Ezekiah na kumuongezea miaka,mponye tena Mke Wangu na ukamwongezee Miaka ili aje kuishi kulitukuza na kulisifu jina lako,kama ulivyomponya Batimayo,kama ulivyomfufua Lazaro,Mponye tena Mke Wangu katika jina la Yesu kristo wa Nazareth,nikammwagia New Annointing water,nilivyomspray New Annointing water upumuajia wake ukarudi asilimia mia moja akiwa kwenye oxygen,kumbuka upumuaji wake ulikuwa chini ya 85,tunaendelea kuomba na tukamaliza,Uwepo wa Mungu ukawa mahali pale,matendo makuu ya Mungu yakaanza kuonekana toka saa tisa jioni wakapunguza oxygen wakasema akiendelea hivi kesho wataangalia ili waitoe,baada ya saa moja upumuajia wake ukarudi chini wakaongeza tena kiwango Cha oxygen,nikaweka sala ya Tb Joshua aliyokuwa anawaombea wagonjwa kule Honduras kwenye isolation centers,

Neema na rehema ikawa upande Wangu na Mke Wangu,Mke wangu akapata nguvu akaanza kuongea,tukapata kibali machoni pa Bwawa Yesu, Madaktari wawili wakaingia kwenye chumba chetu,Mke Wangu akawaambia mtoto toka juzi achezi, Daktari mmoja akaenda kufuata utra sound na kuileta chumbani na kumpima,tumepima utra sound tumekuta ni mzima ana wiki 34,kilo 2.4 na bado wiki 5 ajifungue,Mungu akamtuma daktari mwingine kuja kuniambia ili mapafu yaweze kuja kupush mtoto mwezi ujao akaniandikia dawa nyingine nikanunue ili mapafu yapone haraka,haya yote kwangu ni muujiza,maana kwa hali ilivyokuwa sikuwaza hata kufika mwezi ujao,kama Nabii Isaya alivyotumwa kwa Hezekiah akamwambie,Mungu amekuongezea Miaka ya kuishi,Hii ndio maana ya breakthrough.
Because of Christ i command the total healing of the lungs of Elizabeth in Jesus' Name. Amen,Nikaendelea kumwombea kwa kutumia the medium of New Anointing Water,ili apone leo leo,1Wathesalonike 5: 16 - 18.siku ya tano,Mungu akaendelea kuonekana,mlango wetu wa chumba ikaondolewa mitungi yote ya Oxygen ikapelekwa kwenye milango mingine,uwa mitungi ya oxygen inawekwa standby kwenye chumba cha mgonjwa wa Covid19 ili unapoisha anabadilishiwa mwingine kwa haraka,hata mashine kupima kiwango cha upumuaji ikaondolewa chumbani kwetu,kwa maana Mke Wangu sasa alianza kuwa imara,Jina la Bwana Yesu libarikiwe,mgonjwa anakaa sasa na ameanza hata kujibu sms za watu kwenye simu yake,

Ninakosa maneno ya kumshukuru Mungu, nakosa sadaka nzuri yakumtolea Mungu wangu naomba niwe chumvi na mwanga kwa Walimwengu,palipo na giza nikawe nuru,palipo na dhiki nikawe faraja,Kama Mungu alivyombariki Mtume Paulo, Apron of Paul,ambae kitambaa chake alipokiachia kwa watu kila aliyeshika alipona ugonjwa wake na kuponya maelfu,Mungu ukambariki Tb Joshua na neema uliyomjalia ya kuombea maji na kila ataemwagiwa maji hayo akapokea uponyaji kama Mimi na Mke Wangu tulivyopokea, Nimalizie kwa kusema Bwana Yesu anaponya kwa walio tayari,ukijua kwamba Mungu anaweza yote basi hudhuria mikutano ya injili na Semina za Neno la Mungu utapona,wafuate wachungaji katika kanisa ambalo Mungu anaishi (A living Church) watakuombea na utapona,hudhuria ibada kila mara katika kanisa la kiroho utaombewa na kupona,Yesu kristo anaokoa,ukiamini leo hakika unaokoka,Yesu Kristo anaponya,ukiamini leo hakika utapona.

Nikiishia hapa, Mimi ni
Leslie Mbena,
Dar es Salaam.
Tanzania.
0755078854

-Bachelor of Business Administration in International Business.
-Master of Leadership and Management.

Recent Publication;
-Assessment on the Effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
 
Walawi 19: 1 - 2,
2. 1Petro 1: 14 - 16,
3. Yohana 14: 15,
4. Yakobo 2: 10 - 11,
5. 1Yohana 3: 22 - 24,
6. 1Yohana 4: 7 - 8,
7. 1Yohana 5: 18 - 19,
8. Wagalatia 5: 19 - 21 & 22 - 25,
9. Wafilipi 1: 20 - 21,
10. Marko 11: 23 - 25,
11. Matendo 19: 11 - 12,
 
Tayari umeshatupiga hapo mkuu.

Haujatwambia kama mke wako alipimwa na kukutwa na COVID19 bali walimpima na kumkuta na tatizo la upumuaji ambalo ndiyo husababisha COVID19. Hapo unatumia ubabe tu kutupiga, yaani unamaanisha COVID19 husababishwa na tatizo la upumuaji?
Siyo kwamba tatizo la upumuaji ndiyo husababishwa na COVID19?

Huko ni kumsingizia Mungu kwa viwango vilivyo pitiliza, Mungu hapendi kabisa hizo. Acheni sanaa zenu.

Mke wako atakua ali login JF kwa account yako akaona mambo unayoandika humu Majukwaani akaishia kupandisha pressure kiasi cha kushindwa kupumua, halafu wewe unaleta story zako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom