Kwanza pole sana. Pili kama hiyo picha hapo kwenye avatar inaendana na wewe (ya kwako) au umevutiwa na pozi la huyo kijana basi naomba uanze kubadilika hapahapa! Ujasiri hujengewi, ujasiri unajijengea mwenyewe. Anza kwanza kutoa hiyo picha weka picha zenye staha ya kiume. Kama unapenda pozi hizo jenga kwanza ujasiri wa kuachana nazo.
Lingine nimeona kuwa wewe hasa unatamani ushoga. Hiyo inatokana na hisia nyingi ulizojijengea juu ya jambo hilo. Najua hutaweza kusema ila pengine unaangalia video za aina hiyo. Acha hilo pia.... Baada ya hapo sali na jiamini...... Maumivu yakiendelea baada ya hapo basi muone daktari kwa kuwa utakuwa umeathiriwa na mfumo ila kwa sasa mimi naona umetekwa zaidi na hisia. Usiziendekeze, anza na hiyo avatar sasa!