Msaada-Nairobi fly kaniharibu ngozi shingoni

Msaada-Nairobi fly kaniharibu ngozi shingoni

Asante mkuu,sijui aliingiaje kwenye neti usiku!asubuhi naamka uso wote haufai!nimeshindwa hata kwenda kujenga taifa!anapenda sana usoni na shingoni sijui kwa nini!!?
Nenda pharmacy unaweza pata dawa. Kuna dawa niliwah tumia ya tube hakuna kovu lilibaki sema nmeisahau jina pole.
Ila hawa wadudu wanapenda sana uso sijui kwanini. Mimi nilivyo mweupe nikawa navaa nikabu nikitoka mpaka uso ulivyorudi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kumbe unafahamu ni Narrow bee fly.. Kwanini umeandika Nairobi?

Ni kwa sababu watu wengi wanamwita Nairobi fly, kwa hiyo akaona awaraisishie watu kwani angeliacha tu Narrow bee fly, watu wengi wasingejua na wasingeweza mpatia msaada
 
Wikipedia page
Screenshot_20200203_160629_com.android.chrome.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna huyu mdudu wa kuitwa Nairobi fly (narrow bee fly) kanitambaa uso wote haufai umejaa makovu kila pahala. Msaada kwa yeyote aliyewahi kukumbana nao alitumia dawa gani maana hali si hali, uso umeumuka.

Sent using Jamii Forums mobile app
Paka mafuta ya vaseline mengi kiasi hivi maeneo yaliyoathirika
Yale makovu yatatoka haraka ndani ya siku mbili bila kadhia yoyote
 
Duh pole sana, hao wadudu sio poa kabisa. Nakumbuka niliwahi kuwaona kpnd nipo advance, walitutambaa bweni zima. Sina ata hamu nao.
 
Mm pia narrow bee fly aliwahi kunitembelea usoni nilikuwa nanawa uso kwa sababu ya TETMOSOL Baada ya siku tatu NNE mambo yakawa shwari kabisaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu leo nimeamka nimekuta Shingoni Nimetembelewa na Huyo mdudu anaeitwa nairobi fly,maeneo ya shingoni kwa nyuma,

Nimeungua Aswaa Shida ni kwamba kunawasha sana,

Dawa yake ni nini wakuu.

Nb.
Wadudu hawa wapo wengi na Mvua hii sio usiombe kutembelewa nao.


Cc Zero iq

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jana asubuhi nimeamka na kukuta najisikia muwasho sehemu ya shingo. Nikajua ni kawaida ya matatizo madogomadogo ya mwili. Leo nimeangalia nimekuta kama michirizi shingoni inawasha kwa sababu ngozi yangu ni nyeupe inaonekana sana.

Nimewaonesha watu wenye experience wananambia ni mdudu anayeitwa nairobi fly kanipitia. Sasa wakuu naombeni msaada jamani dawa nayoweza kutumia kuzuia asiniharibu ngozi mwili mzima kwa sababu kwa mbali naona ishaanza kubabuka sehemu za shingoni.

Kama kunamtu ili tatizo lishawahi mkuta naomba anisaidie ushauri jamani sababu nimekosa raha kabisa.

Akhsanteni

Sio Nairobi fly mkuu, anaitwa Narrow bee fly. Siku nyingine usirudie kosa kama hili.


Happy dude [emoji67]‍[emoji538]
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom