Ushauri bora kabisaWala siyo kwamba wengine wanapendelewa ila kwa neema tu
1. Jiepushe kuwa na marafiki wa kupiga soga. Kuwa na marafiki wa kwenye kutafuta kazi, kuangalia fursa. Mnapigiana simu, kuna kazi fulani twende tukafanye
2. Penda kuchangamana na watu ila wenye malengo hasa angalia waliokuzidi umri au umri sawa ila malengo ya kutoboa
3. Usipende kubagua kazi. Mfano mm huwa sichagui kazi ili mradi iwe halali. Anza hata kukaanga chapati uza
Kadri unavyozidi kupambana ndiyo Mungu anakufungulia baraka
4. Siri ambayo ni ngumu na rahisi kutoboa. Kuishi mbali na ndugu, huko hakuna msaada wowote zaidi ya kujipigania. Lazima upambane utoboe
5. Kupunguza matumizi yasiyo ya msingi
6. Nyumba hizi tunazokaa huwa zina neema au mikosi. Unaweza kuwa kwenye lkn kila unachofanya hakifanikiwi ila nyumba nyingine ukafanikiwa
7. Usichoke kumuomba Mungu siku zote.