Msaada: Mdogo wangu ana stress za maisha

Msaada: Mdogo wangu ana stress za maisha

Muanzishie Biashara ya kuuza samaki akienda kutembeza wale samaki akirudi atajikuta kachoka hawazi tena.
Habari

Kuna mdogo wangu mhitimu wa chuo kikuu mwaka huu mwezi wa 7.

Baada ya kumaliza chuo nilimfwata nyumbani kwa mzee nikamchukua nakuishinae hapa nyumbani kwangu.

Lakini baada ya kukaanae nimegundua kuwa dogo anapresha ya maisha, yani anastress kutokana nakuwaza sana maisha.

Hali hiyo humfanya kutokuwa na furaha kabisa ilhali hakuna anachokosa hapa nyumbani maana anakula vizuri na kulala vizuri.

Sasa ndugu zangu naombeni ushauri nifanye nini hili nimsaidie dogo maana naona anakosa furaha muda mwingi asijekuathirika kisaikolojia
 
Mpe mtaji wa biashara, kama ni msichana mwache aolewe huyo mwenza wasaidiane kwenye kazi zake, yeye mwaka huu tu ana mawazo wapo wa 2014 hawajapata kazi
 
Aisee kipindi after chuo,kinatesa sana maana expectations vs reality ni tofauti, mi sikuhisi kama ningesota sana kitaa bila kazi,nilikua na stress mno nawaza hadi vocha niombe home[emoji30] acha tu, sambaza CVs kama mchele but no any call aisee.

Mshauri tu asijistress sana,ipo siku mambo yatakua poa, ajitahidi kusambaza CVs asichoke, pia kama unaweza mpa kimtaji ajishughulishe na vibiashara asikae idle,itamsaidia
 
Sio uzungu, kaka. All humans are the same no matter the race!

Wa Tanzania wengi hatuamini hiki kitu lakini kipo - Sonona ipo tena kwa asilimia zaidi ya mia! Kuna vijana wanaamua kujitoa duniani kwa sababu hizo na ni suala ambalo lingezuilika kwa maongezi tu - Yaani kubadilisha mtazamo wa muathirika kwa maongezi tu.

Kama ulinielewa nilianza na "talk to him" na uelewe anataka nini.. Ila kwa wewe haitakuwa accurate sana ukilinganisha na therapist ambae ataelewa moja kwa moja shida na namna ya kuisolve!!

But again! Is money more important than rescuing a human??
Acha maneno miiingiii, ampeleke halmashauri au manispaa or any institution akajitolee for free awe bize, ajichanganye na pia apate ujuzi na connection....
 
Ukiwa chuo unakuwa una dream za maisha yako yatakuwaje hapo baadae sasa ukija mtaani unaona kama umechelewa hivi uliwaacha wote wamekuzidi lazima uwaze.

Cha kufanya ongea nae nini anaweza fanya na kama uko vizuri muwezeshe kwenye ndoto zake.
 
Kama ni wa kiume lazima awe na stress hata umdekeze vipi, hawezi kufeel kuwa huru kutumia pesa asiyoitolea jasho.
Wewe mtafutie channels za mtaani aanze kujitegemea
 
jasema na huo Muzungu aliotumia kutetea hojayake[emoji23][emoji23][emoji23]
hivi tunaelekea wapi aisee? kwanini tuna uzungu sana siku hizi?

kijana ana stress za maisha na wewe ushauri wako wa kwanza ni zitumike gharama za kumlipa specialist ili amsikilize na kumpa ushauri? kabisa yani?

kweli social life is dead. inasikitisha.
 
Huo ni muda wa mpito tu na wengi wetu huwa tunalikuza tatizo kuliko uhalisia japo kwa kiasi flani hisia za kuwa Useless, kuishi chini ya rules za mtu mwingine (kufake ili usiharibu kwa bro ni feeling inayompa limits za uhuru aliouzoea), kushindwa kujisupport na kuwasupport watu tunaotaka kuwasaidia na ile kuona unachelewa kulinganisha na wenzio inaumiza kichwa mnooooo.

Ukitaka kumsaidia wala usiforce kumpa comfortability maana utaharibu zaidi. Cha msingi kuwa friendly na ujaribu kumdadisi via story za kawaida tu ili ujue kitu kinachomsumbua zaidi. Ukijua then ni step kubwa ya kulitatua. Pia hongera kwa kujali mkuu
 
Mpe mtaji.. kama tatizo kutokupata job,

Nadhani wengi tunachukulia hili suala very general. Mtu ambaye kupata kazi ni ngumu bhasi kuna njia za kumfanya awe competent zaidi katika field yake kama kuongeza soft skills kupitia course fupi hata za mtandaoni na pia kujitolea popote ili apate experience ya industry yake ambayo itasaidia kuboost CV yake na kumpa connections.

Mtu anayetaka ujasiriamali anaweza kufanya yote hayo pia bila kusahau njia za kufanya networking ili kumfanya awe katika cycle ya watu anayoihitaji..

Mwisho wa siku ni lazma atafute njia ya kumuelewa and from there ataweza kutoa msaada
 
Kawaida mtu akimaliza chuo anakuwa na presha ya maisha,hiyo ni hali ya kawaida, mimi pia nakumbuka baada ya kumaliza chuo nilikuwa katika hali kama hiyo kwa muda fulani, naona ni hali ya kawida na pia naona ni kitu kizuri sababu dogo anaonekana ana akili za maisha
 
Yani umeeleza kitu fulani chenye uhalisia,hii ilinikuta....ila na bado ina nikuta hii hali,licha ya kuwa na shughuli nyingi za kufanya ila bado sina furaha kabisa,maisha yangu namis vitu vingi sana asee!! Yani maisha yangu kwaasilimia kubwa ni kusononeka tu.
Hicho kipindi aisee ni kibaya sana,tena kwa mtoto wa kike nadhani ni kipindi kibaya zaidi tho' binadamu ni binadamu,.niliwahi kukieksipiriensi few years ago...lol[emoji23][emoji23][emoji23]nyumbani unakula vizuri tena wakati mwingine wewe ndio unapanga mle nini japo huna hata100 mbovu,unalala vizuri and you can hang out with friends sometimes lakini nilijihisi kabisa siko sawa i need something extra,nahitaji KUJITEGEMEA hata kama niko home nahitaji kuwa na "cha kwangu" yaani unakuwa na stress halafu sijui inakuwaje kipindi hiki nacho mahusiano hayanogi yaani hupati mtu yule unamuhitaji daaah[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]but all in all ni kipindi kifupi lakini kina mapito ambayo ukivuka salama hakika taji inakuhusu nilikuwa napenda kujiongelesha kwa sauti "Abba Father where are You" "are you listening" "why this" "please help me".....

Ndugu wa karibu pia mna mchango mkubwa wa kumpunguza hayo mawazo,kumpa moyo kwa mifano iliyo hai na kumuhusisha na mambo ya IMANI kama niwaamini..
 
Mleta uzi chukua ushauri huu,nna experience na hii hali.
mfungulie biashara ndogo hata M PESA aji keep bize, tena ikiwezekana mtafutie chumba hata cha bei nafuu awe huru, mlipie kodi ya mwaka mzima nakuhakikishia atarudisha furaha ndani ya muda mfupi, usimfuge hapo kwako huyo sio mbuzi ni binadamu
 
Aisee mimi nilisambaza CVs kama mchele ila bado nikatoka kapa,nikajaribu kujitolea miezi miwili tu nikaacha coz huku najitolea na mama mwenye nyumba nae alikua anatishia kunitolea vyombo nje,..ni wakati ambao kila ventures zangu ndogo ndogo zilipo dorola..ni wakati ambao nilijihisi kama sina msaada wowote dunia hii...yani kuna muda hata baadhi ya maboss ninaofahamiana nao nikaona kama wana nibania tu...kila nilofanya nikaona halifai,na kila alie nitizama nilihisi ana niona vile nawaza kichwani. Kuna muda nikahisi nilipoteza muda wangu kusoma chuo,hakika nilijutia sana! Nikahisi huenda nilipoteza muda...

Siku zilisonga bila mafanikio,matarajio yalimeza hata juhudi zangu za awali za utafutaji. Stress zilizonga maisha yangu,roho ya kukatia maisha tamaa ilikua ina ninyemelea but Tumaini lilikua kubwa kushinda roho hiyo. Mbaya zaidi sikua na mzazi au mlezi wa kunipa hata faraja tu kwa wakati huo.
Na nikipindi ambacho nilitamani hata nipate mtu nimweleze yake yanayo nisibu,..daaah sikumpata mtu huyo,na sidhani kama nitakuja kumpata...daah maisha ya upweke yasikie tu kwa jirani.
Ila yote yalipita,muda ulifika kila kitu kikawa mahala pake. Kazi sikupata kwa wakati huo,ila niliamua kubadili mtazamo na kusimama imara katika vijibihashara fulani vidogo vidogo,ubize ulipozidi na ile hali ikapungua kwa kiasi fulani,ingawa sonona ni sehemu ya maisha yangu.

So,huyo kijana namshauri atafutiwe kazi ya kufanya ili awe bize,pia mjenge kisaikolojia ili aondoe matumaini makubwa alojiwekea. Kula vizuri na kulala vizuri haiwezi kuwa chachu ya furaha yake, mpe uhuru kiasi. Namaanisha acha akapange na mpe kianzio cha bihashara au mtafutie pahala pa kujishikiza.
Aisee kipindi after chuo,kinatesa sana maana expectations vs reality ni tofauti, mi sikuhisi kama ningesota sana kitaa bila kazi,nilikua na stress mno nawaza hadi vocha niombe home[emoji30] acha tu, sambaza CVs kama mchele but no any call aisee.

Mshauri tu asijistress sana,ipo siku mambo yatakua poa, ajitahidi kusambaza CVs asichoke, pia kama unaweza mpa kimtaji ajishughulishe na vibiashara asikae idle,itamsaidia
 
Back
Top Bottom