Wakenya ni wajuaji sana,kuna dogo mkenya tunaishi nae amekuja kusoma sasa kawa MTU Wa makundi ya vijana Wa mtaani wavuta bangi, walevi na wacheza kamari,sasa wenyeji walimtahadharisha asiwe na marafiki wasioeleweka lakini hakusikia.
Sasa kilichomkuta anajuta alienda kuweka bond tablet ya Samsung kwa muhuni mmoja Wa mtaani ile muda Wa kurudisha pesa umefika akaja kuitwa anaambiwa wezi wamekata dirisha wameiba tablet,simu 2 na sh.laki2,mpango ulipangwa kifamilia mama Wa muhuni akawa anatetea wameibiwa kweli, ukicheki sehemu iliyokatwa ni ndogo ukilinganisha na ile tab,mkenya akawa ametapeliwa kihivyo.
Unakuta wakiwa wakenya wawili wanajifanya wajuaji kuliko wenyeji wao wanajipangia mambo yao wakishafikwa na matatizo ndio wanakuja kutia huruma kwa wenyeji wao, inabidi wabadilike kabisa la sivyo ndio yanakuja kutokea kama haya.
Pole sana mkenya na mshana jr.