Al-Watan
JF-Expert Member
- Apr 16, 2009
- 11,891
- 14,560
Wakubwa heshima zenu.
Mie kijana nimezichanga ughaibuni kwa kiasi (si kama Bligate hahaha), tatizo ilmu ya mambo ya fwedha haijakomaa.
Tatizo linakuja, nikitaka kuja kununua kitu cha gharama kubwa nyumbani, mfano kibanda cha kuotea Tanzania kwa pesa iliyoko benki ya Kimarekani, malipo nitafanyaje?
Maana ndugu zetu wengine huwezi kuwalipa kwa credit card, na Mmarekani haruhusu kutoa zaidi ya $ 10,000 bila maelezo marefu, Wamexico wanaotewa kila kukicha, kuna mmoja alifanya kazi kuosha vyombo miaka 10 na kuzichanga $ 60,000, wakamuotea na kumpukutisha $ 50,000. Isitoshe kutembea na mihela mingi ni ulimbukeni.
Sasa nikikutana na Mzee asiyejua hili wala lile, anauza nyumba kwa cash Dar, na mimi nina hela benki ya Kimarekani, nitafanyaje.
Natanguliza shukurani.
Mie kijana nimezichanga ughaibuni kwa kiasi (si kama Bligate hahaha), tatizo ilmu ya mambo ya fwedha haijakomaa.
Tatizo linakuja, nikitaka kuja kununua kitu cha gharama kubwa nyumbani, mfano kibanda cha kuotea Tanzania kwa pesa iliyoko benki ya Kimarekani, malipo nitafanyaje?
Maana ndugu zetu wengine huwezi kuwalipa kwa credit card, na Mmarekani haruhusu kutoa zaidi ya $ 10,000 bila maelezo marefu, Wamexico wanaotewa kila kukicha, kuna mmoja alifanya kazi kuosha vyombo miaka 10 na kuzichanga $ 60,000, wakamuotea na kumpukutisha $ 50,000. Isitoshe kutembea na mihela mingi ni ulimbukeni.
Sasa nikikutana na Mzee asiyejua hili wala lile, anauza nyumba kwa cash Dar, na mimi nina hela benki ya Kimarekani, nitafanyaje.
Natanguliza shukurani.