Msaada kuhusu sony home theatre system na RAM

Anko Elly

Member
Feb 22, 2017
69
70
Habari za asubuhi The Great Thinker wa jukwaa hili adhimu la Teknolojia. Matumaini yangu kuwa hamjambo na mnaendelea vizuri katika suala zima la upambanaji.

Kilichonileta leo kwenye hili jukwaa ni mambo mawili, Mosi ni kuhitaji msaada wa kueleweshwa kuhusiana na Sony Home Theatre System na kingine ni Ram ya Laptop yangu.

Nikianzia kwenye suala hili la HTS(Home Theatre System) za Sony nimejaribu kufanya Research kuona ni ipi yenye nguvu na bora zaidi.

Katika Research yangu ndogo nikagundua kuwa zipo za madaraja mbalimbali kuanzia 350, 650, 950 hapa nazungumzia nguvu ya mziki. Mfano hizi za 350 huwa na Speaker ndogo jumla 5 wakati hii ya 650 huwa ni zile speaker ndefu 4 na ndogo moja halikadhalika na 950.

Sasa swali langu ni kwamba nimetokea kuipenda hii yenye nguvu ya 950 sema zipo za aina mbili, moja ni ile yenye wireless speaker na nyingine Speaker zake unatumia wire kawaida.

Msaada naohitaji hapa kuweza kufahamishwa juu ya hizi Speaker za Wireless, kwa wale walioweza kutumia hasa katika ubora wake na Je, huwa zinakuwa na changamoto gani? Maana nimekaa nikaona kabla sijanunua nije huku kuomba msaada.

Mwisho kabisa nahitaji kujua bei ya RAM ya Dell Latitude E6410 8GB ni kiasi gani? au kama kuna mdau anauza ambayo ni mpya na sio Used anijuze hapa jukwaani kwa manufaa ya wengine na tukiafikiana bei tuweze kufanya biashara.

Nawasilisha wakuu
 
hio ni laptop ya kizamani 1st gen unaweza zipata hata laki 2 au 3 hazina issue sana, na usiangalie wingi wa ram sababu ram zinaongezeka kirahisi, mtu anaweza akatafuta laptop ya 150,000 akaspend kidogo akanunua ram ya 8GB kisha akakuuzia wewe kwa bei ghali.
 
kuhusu home theatre pia usiangalie nguvu tu ya speaker kuna vitu kama chanell ni muhimu mkuu, kuna 2.1, 5.1, 7.1 etc hizo ni idadi ya speaker na kila moja ina eneo lake linakaa kwenye chumba ama sebule, chagua kutokana na eneo lako unapopeleka hio home theatre.

pia sometime wireless sio nzuri hasa unapoplay vitu vyenye bandwidth kubwa, ni technology gani ya wireless inatumika? kama ni Wifi ni ipi?

CORAL
 
Sony nyingi huwa zinatumia Infrared, kunakuwa na ka transmitter na receicer ni zile speaker mbili, muhimu ni zinahitaji line of sight, yani kusiwe na obstacle kati ya transmitter na receiver ya hizo speaker.
Kuhusu Quality hamna tofauti ambayo utaisikia kwa kutumia aidha wire au hizo wireless, ila kama utaziweka sehemu ambayo watu wanapita pita ndio itakuwa usumbufu mana signal zitakuwa zinakata na kurejea pale mtu apitapo across the beam.
 
hio ni laptop ya kizamani 1st gen unaweza zipata hata laki 2 au 3 hazina issue sana, na usiangalie wingi wa ram sababu ram zinaongezeka kirahisi, mtu anaweza akatafuta laptop ya 150,000 akaspend kidogo akanunua ram ya 8GB kisha akakuuzia wewe kwa bei ghali.
Asante Sana Mkuu... Sasa unanishauri ninunue laptop gani ya kisasa ambazo bei zke ni nafuu
 
kwa mpya kuanzia around 700,000 hadi 800,000 ndio unapata laptop nzuri za i3 chini ya hapo utadanganywa tu mkuu.
Sasa hizi za core i3 si zitakuwa na uwezo mdogo mkuu ukilinganisha na hii yangu ya zamani yenye corei5? Nauliza lakini
 
Sasa hizi za core i3 si zitakuwa na uwezo mdogo mkuu ukilinganisha na hii yangu ya zamani yenye corei5? Nauliza lakini
i3 7th gen ni zaidi ya 50 percent faster kuliko i5 ya 1st gen, pia inatumia umeme kidogo sana na kwenye gpu ni zaidi ya 700 percent faster. yani utofauti wao ni mkubwa sana. na ukipata i5 7th gen ni nzuri zaidi.
 
i3 7th gen ni zaidi ya 50 percent faster kuliko i5 ya 1st gen, pia inatumia umeme kidogo sana na kwenye gpu ni zaidi ya 700 percent faster. yani utofauti wao ni mkubwa sana. na ukipata i5 7th gen ni nzuri zaidi.
Asante sana Mkuu kwa ufafanuzi huu na kunipa mwangaza katika hili. Kwaiyo nikienda kununua niwambie nataka core i3/core i5 ya 7th Generation sio watanielewa? Mwisho kabisa mfano nikienda kununua kwenye yale Maduka ya Used Laptop yaliyopo pale kariakoo Uhuru sio mbaya?
 
Asante sana Mkuu kwa ufafanuzi huu na kunipa mwangaza katika hili. Kwaiyo nikienda kununua niwambie nataka core i3/core i5 ya 7th Generation sio watanielewa? Mwisho kabisa mfano nikienda kununua kwenye yale Maduka ya Used Laptop yaliyopo pale kariakoo Uhuru sio mbaya?
yah 7th iwe priority ila ukikosa 6th pia ni nzuri.

uhuru tu uwe makini wana laptop refurbished zinakuwa sio mpya wanaweza kukubambikia,

hakikisha pia wanakupa warranty.
 
kuhusu home theatre pia usiangalie nguvu tu ya speaker kuna vitu kama chanell ni muhimu mkuu, kuna 2.1, 5.1, 7.1 etc hizo ni idadi ya speaker na kila moja ina eneo lake linakaa kwenye chumba ama sebule, chagua kutokana na eneo lako unapopeleka hio home theatre.

pia sometime wireless sio nzuri hasa unapoplay vitu vyenye bandwidth kubwa, ni technology gani ya wireless inatumika? kama ni Wifi ni ipi?

CORAL

2.1 sio hometheatre ...hiyo ni multmedia ya kawaida hapo kuna stereo na bass ..pia sio kila 5.1 na kuendelea ni hometheatre ..zipo seapiano za hvo ila zinamiss sifa ya kuwa na hizo effect hivo huwez ziita hometheatre

I got my own set up with 4channel za kawaida a center and a sub ...na sio hometheatre
 
2.1 sio hometheatre ...hiyo ni multmedia ya kawaida hapo kuna stereo na bass ..pia sio kila 5.1 na kuendelea ni hometheatre ..zipo seapiano za hvo ila zinamiss sifa ya kuwa na hizo effect hivo huwez ziita hometheatre

I got my own set up with 4channel za kawaida a center and a sub ...na sio hometheatre
kitu gani kinafanya 2.1 isiwe home theatre? speaker yoyote ile inayomimic sound kama theatre inastahili kuitwa home theatre.

zipo home theatre kibao toka kampuni kubwa kubwa ambazo ni 2.1 na zinatoa sound effect kama upo kwenye theatre

mfano Bose cinemate series
 
kitu gani kinafanya 2.1 isiwe home theatre? speaker yoyote ile inayomimic sound kama theatre inastahili kuitwa home theatre.

zipo home theatre kibao toka kampuni kubwa kubwa ambazo ni 2.1 na zinatoa sound effect kama upo kwenye theatre

mfano Bose cinemate series

Unawezaje gawa hizo effect kwenye channel mbili only left and right..where is surrounding ..kwenye hizo spika mbili ipi icheze hizo effect

Ziko hata hizi aboda za elf 90 nishawah ona moja imeandikwa hometheatre
 
Unawezaje gawa hizo effect kwenye channel mbili only left and right..where is surrounding ..kwenye hizo spika mbili ipi icheze hizo effect

Ziko hata hizi aboda za elf 90 nishawah ona moja imeandikwa hometheatre
swali hilo hilo jiulize unapataje sorrounding ya theatre kwenye speaker 5 ama 7? maana kumbi nyingi siku hizi zina speaker 20 kuendelea,

speaker ikishakua zaidi ya 1 tayari kuna sorround sound hata kama itakuwa ni left na right tayari ipo, ni kwa ubora ule ule? hapo ndipo unajikuna unapofikia.
 
swali hilo hilo jiulize unapataje sorrounding ya theatre kwenye speaker 5 ama 7? maana kumbi nyingi siku hizi zina speaker 20 kuendelea,

speaker ikishakua zaidi ya 1 tayari kuna sorround sound hata kama itakuwa ni left na right tayari ipo, ni kwa ubora ule ule? hapo ndipo unajikuna unapofikia.

Spika 20 zinarudia sound ile ile kulingana na ukubwa wa ukumbi ila sio kwamba kila moja itacheza effect yake big No

Hata nilipo kuna 5 channel na single super bass...sasa jiulize why nimeweka channel zote na mziki unatengenezwa na channel mbili tu

Jibu lake litakuwa ni sawa na huo ukumbi kuwa na speaker 20 ...lengo ni moja mimi kwangu kulingana na eneo channel hizo zimetosha
 
Subwoofer ya pioneer rms watts 600 kibongo bongo bei gani na zinapatikana wapi???
Spika 20 zinarudia sound ile ile kulingana na ukubwa wa ukumbi ila sio kwamba kila moja itacheza effect yake big No

Hata nilipo kuna 5 channel na single super bass...sasa jiulize why nimeweka channel zote na mziki unatengenezwa na channel mbili tu

Jibu lake litakuwa ni sawa na huo ukumbi kuwa na speaker 20 ...lengo ni moja mimi kwangu kulingana na eneo channel hizo zimetosha
 
Spika 20 zinarudia sound ile ile kulingana na ukubwa wa ukumbi ila sio kwamba kila moja itacheza effect yake big No

Hata nilipo kuna 5 channel na single super bass...sasa jiulize why nimeweka channel zote na mziki unatengenezwa na channel mbili tu

Jibu lake litakuwa ni sawa na huo ukumbi kuwa na speaker 20 ...lengo ni moja mimi kwangu kulingana na eneo channel hizo zimetosha
Si kweli mkuu speaker za theatre zina effect zaidi na sio kwamba zinarudia yale yale.

5.1 ni sorround sound tu kwa maana kulia, kushoto mbele nyuma etc.

Speaker za Cinema ni 3d hazimalizi kulia na kushoto tu bali zinaenda hadi juu na chini,

Mfano kuna sauti ya tetemeko speaker za chini zitahusika, kuna sauti ya Ndege kupaa speaker za juu zitahusika, kuna Sauti ya Kiumbe kipo angani kitaongea juu kulia basi speaker ya juu kulia itaongea.

Jaribu kwenda kumbi za Cinema kuthibitisha ninayokwambia.
 
Back
Top Bottom