Msaada kuhusu kupima DNA

Msaada kuhusu kupima DNA

Wewe ukimuangalia huyo mtoto unaona kuna kipi unachofanana nae? Kama hakuna hiyo ni redflag namba 1.

Kapime DNA bila kujali gharama ni kheri ujue kwamba si damu yako bado mapema, maana unaweza kujikita ktk matunzo na kubania uzazi mwingine kutokana na majukumu uliyonayo muda ukaenda bila mtoto wako wa damu..

Ukishajua kuwa SI wako, usikatishe huduma bali upunguze huduma..

Dunia haiko fair wale wanaokupa moyo wa uvumilivu wa kulea mtoto si wako ndio hao hao watakaokucheka kuwa ni bwege. Hakikisha mapema kbs kama ni damu yako.

NB:Mtoto wa kulea ambae unajua si wako ni tofaut na yule ambae unajua ni wako alaf unakuja kuambiwa si wako.
Umesema kwel
 
Kwakifupi ni kwamba hakuna hasira za muda mrefu namna hiyo. Yaani mtoto awe wako harafu mama yake awe anaimba kila siku kuwa mtoto si wako!!!!!!. Kwakifupi acha hata kupima we amua tu kama unahudumia kama msaada ama unaangalia ustaarabu mwingine. Hapa wameshakuja na kukuambia eti baraka zako ziko kwa huyo mtoto. Hebu waulize kama wameshasaidia hata katoto kamoja ka kwenye mazingira magumu kama wameweza kupata hizo baraka
Nashukuru kwa wazo zur
 
Umesema unampenda sasa nini kujitia stress ,ikiwa wako au isiwe wako wewe ni kungangana tu aikiwa mkubwa atakuja kukufaa huyo ,mtafutie wadogo wake at list wawe wa halali yaani owa .
 
Mkuu hilo mbn simple tu we,piga kimya alafu maji,na,mafuta vitajitenga apo,baadae,ni,swala la,mda,tu na,damu ni,nzito kuliko maziwa mkuu na,kama,ni,wako wala hauna haja yakutumia nguvu kuuuubwa we relax mambo yataji,set yenyewe maana,mtu nitofauti na,kitu,mkuu. na,usiumie,kichwa kwa,jambo,hilo mambo mengine unaacha,tu,asili ifanye kazi yake na,hapo ndipo unapoonekanaga uzito wa,damu. na,usionyeshe sura yakugombania mtu we endelea na,mishe zako,tu.
Nashukuru
 
Duuh pole.

Ila Kamwe kama wewe NI Mwanaume using'ang'anie Mtoto na Mwanamke aliyemzaa Mtoto huyo.

Kama amesema siô wake Mpe.

Hata kama angesema ni wako alafu anataka Mtoto wake amlee mwenyewe. Mpe Mtoto wake. Huyo ni Mamaake. Yeye ndiye anazaa siô wewe.

Sijui Kwa nini Watu Wanaona shida katika Jambo hili.

Tafuta Mwanamke Mwingine uzae Mtoto Mwingine Lea. Akizingua naye mpe Mtoto wake. Tafuta Mwingine. Hivyohivyo

Yaani Mwanaume unaumizwa na ishu ndogo kama hiyo kana kwamba hauna uzazi.

Suala la Huduma hiyo inategemea na wéwe mwenyewe.
Kama amesema Mtoto siô wako Huna haja ya kumhudumia Mtoto àmbaye siô WAKO.

Hakunaga Baraka za namna hiyo.
Mtoto kama siô wako ujue siô WAKO.

Kama ishu ni adaptation. Tafuta Mtoto Mwingine àmbaye hamkuwa na uhûsiano wowote ule Wala huwajui ndugu Zake Kisha mfanyie adaptation

Hao wanaokuambia utabarikiwa hawaelewi chochote kuhusu Baraka
 
Gharama ya DNA ni Wastani wa 150,000.....!

All in all kila kinachotokea Kwa Binadamu kina sababu.
Ipo sababu Kwa Nini umeachana na huyo Mwanamke.....!
Pia ipo sababu Kwa Nini umeletewa huyo Mtoto na Mungu ili Umtunze...!
Mkuu kama gharama ni 150k naweza kupambna kidogo kidogo nkaipata niko Moro mjini inamana wanapima hospital za kawaida au kuna hospital maalum nsaidie kwa hilo kama unajua pia.
 
Duuh pole.

Ila Kamwe kama wewe NI Mwanaume using'ang'anie Mtoto na Mwanamke aliyemzaa Mtoto huyo.

Kama amesema siô wake Mpe.

Hata kama angesema ni wako alafu anataka Mtoto wake amlee mwenyewe. Mpe Mtoto wake. Huyo ni Mamaake. Yeye ndiye anazaa siô wewe.

Sijui Kwa nini Watu Wanaona shida katika Jambo hili.

Tafuta Mwanamke Mwingine uzae Mtoto Mwingine Lea. Akizingua naye mpe Mtoto wake. Tafuta Mwingine. Hivyohivyo

Yaani Mwanaume unaumizwa na ishu ndogo kama hiyo kana kwamba hauna uzazi.

Suala la Huduma hiyo inategemea na wéwe mwenyewe.
Kama amesema Mtoto siô wako Huna haja ya kumhudumia Mtoto àmbaye siô WAKO.

Hakunaga Baraka za namna hiyo.
Mtoto kama siô wako ujue siô WAKO.

Kama ishu ni adaptation. Tafuta Mtoto Mwingine àmbaye hamkuwa na uhûsiano wowote ule Wala huwajui ndugu Zake Kisha mfanyie adaptation

Hao wanaokuambia utabarikiwa hawaelewi chochote kuhusu Baraka
Asante mkuu
 
Hupaswi kuamini chochote kutoka kwa mwanamke aliyemtelekeza mwanae akiwa mchanga.

Kama umeweza kumlea mtoto angali mchanga endelea kufanya hivyo, huenda riziki yako inatoka kwenye baraka za huyo mtoto.

Kama ukifanikiwa kupima na kugundua mtoto sio wako, usimtelekeze. Endelea kumpa huduma hadi atakapokua, Mungu anajua zaidi kwanini alimuweka huyo mtoto katika mikono yako.
Ili akue akamtafute baba yake?

Kuna wanawake wapuuzi kweli. Huyo akikua mama yake lazima ampe sumu against baba alomlea

Mtoa mada usifanyie DNA tz, kafanye kenya, mara 3 kisha chk majibu
 
Wanawake saa nyingine ni wapuuzi. Mimi almanusura nibambikiwe watoto! Nina mtoto mmoja wa kwanza ni copy na mimi, babu yangu, baba yangu kuanzia tembea, ongea, cheka, kila kitu, meno... Ila kuna huyo wa pili niliona mbona simsikii Moyoni sio ule upendo wa mtoto wa kwanza..katoto kaanza kukua bhana bhana sijui yule mtoto kachukua kwa nani kana komwe e.t.c hayupo kabisa ila kafanana na jamaa mmoja hivi ambae nilishawahi kukuta chati zao mara kadhaa..

haya kuna mwanamke mwingine akataka kunibambikia mtoto wa kike, mtoto kuzaliwa kukua hakuna kabisa alikochukua ni tofauti hakuna tulichofanana hata kidogo..
Wanawake wapuuzi kabisa.
Hakuna baraka za kulea mtoto ambae amezaliwa ndani ya nyumba ambae sio wako hasa hawa wanawake wa kizazi hiki wasiokua na adabu. Baraka utazipata kwa mtoto ambaye ni Yatima hana baba hana mama huyo Mlee hiyo ni baraka kubwa sana.

Ukiachana na jembe langu la kiume hao wengine niliwahudumia mpaka wanazaliwa ila nilikua siwasikii Moyoni walipozaliwa kumbe Ulimwengu wa roho ulianza kunipa Dalili, sasa walivokua wanakua ndo kila kitu kikawa wazi ndugu Mwana Uzi kwangu mimi hakukua na haja na DNA maana kila kitu wazi hata ndugu zangu walisema unapigwa na wenyewe walikuja kujua nimegundua.! Na nilikua natuma pesa kama kichaaa na nahisi nililogwa nisijue chochote na kweli nililogwa baada ya kufatilia Kiroho.

Kwa scenario hizo Lazima mtu alogwe..! Wapuuzi sana hawa wanawake. Sasa baada ya kugundua nilikata mlija wa matumizi miaka 5 sasa na sitaki kuja kuwasikia tena kwenye maisha yangu.! Na deal na yule mtoto wa kwangu tu mmoja

NB; INAUMA SANA KUBAMBIKIWA MTOTO/WATOTO NA BAADAE KUJA KUJUA SIO WAKO..VERY PAINFUL

NI BORA ULEE MTOTO UKIJUA UMEMKUTA HUKO HANA BABA HANA MAMA UKAMCHUKUA AU SINGLE MAMA UMEMKUTA NA MTOTO HAPO UNAJUA KABISA NALEA KWA UPENDO USIO WA KINAFIKI.
 
Ivi embu jiulize utakapopima ukaambiwa sio wako utafanyaje?

Mimi sioni hata haja kupima, maana umemkubali na kumlea toka uchanga wake kwa Imani kuwa mwanao na Damu Yako. Huyo mwanamke asikutoe endelea tu na jukumu Hilo jema ulilolianzisha. Ikibidi Fanya kama uliyemuokota jalalani.

La msingi wamleee, ikifika wakati muafaka, chukua mtoto wako.
Hapana hii italeta mtafaruku mkubwa mbeleni..Vipi huyo jamaa anayetajwa ni baba wa mtoto akaja kumchukua mtoto wake na wewe umegharamia kila kitu.
Ni bora kuziba ufa mapema kuliko kuendelea kuumia na maumivu maana huyo mwanamke atamletea maumivu yasiyokoma.
Wanawake wapo wengi atampata atakayemfaa atamzalia. Wanawake wapuuzi sana.

NB; HAKUNA MWANAUME ANAYEPENDA DAMU YAKE ITESEKE, ILA WANAWAKE NDIO SABABISHI WANAUME KUONDOKA NA KUWAACHA.
 
Huwa naskia kuwa DNA inapimwa kwa amri ya mahakama..... Yani mnakubaliana mama na baba then mnaenda mahakamani hakimu anatoa vielelezo ambavyo dktr ndo anapata ruhusa ya kupima DNA ili kuondoa mgogoro apo hospitalin... Niliskiag Huu utaratb ila Sina hakika nao sana....

Nakushauri mkuu.. kam wanadai mtoto sio wako basi we kausha miaka miwili hesab kam umetoa sadaka tu, sitisha Huduma zote kaa tuliza akili tafuta mwanamk mwngine ila asiwe kutoka mjini ndo wale wale watakuumiza kichwa. Mi ni muhanga wa ishu kam yako ingawa ni tofaut kidg khus mtoto.
 
Habari,

Nina mtoto nimemlea kwa takriban miaka miwili hivi, nampenda sana uyu mtoto na ndo mtoto pekee nilienae kwa sasa ila njia ya mama yake na yangu zimeenda tofauti na kila mtu na maisha yake.

Kwa muda mrefu kidogo mtoto nlimpeleka kulelewa na bibi mzaa mama yake tena akiwa ananyonya baada ya mama yake kunitelekezea mtoto.

Nlimpa yule mama huduma zote za mtoto ikiwo bill ya maziwa na mahitaj mengine. Mtoto akaanza kusimama na kutembea akiwa kwa bibi nami nilimhudumia vizur tu.

Mama yake akaanza maneno kuwa mtoto sio wangu, akarudia na kurudia na kila nlipowashirikisha wazaz wake waliniambia nimblock kwakuwa ni hasira za kuwa mbali na mtoto kwakuwa japo alikutelekezea ila alipojua umemleta hapa nyumbani alimtaka mtoto ila tukamkatalia kwakuwa tumeshamwachisha nyonyo na kwamba mtoto aliletwa kwa maandishi kutoka serikal ya mtaa kwahiyo hawezi kutoka tena atakaa pale.

Basi nlipoambia ni hasira nkapuuza na kupuuza na kupuuza kila aliponitamkia hayo maneno.

Uvumilivu una kikomo, na ulikoma pale aliponitajia baba wa mtoto kwa jina kabisa na ni mwanaume ambae alishakuwa nae kimahusiano. Nikaacha kuhudumia vikaanza vikao visivyo na mwisho na visivyoeleweka na visivyo na suluhu. Nimesitisha huduma tangu mwez wa tisa.

Najiskia vibaya kutokumhudumia uyu mtoto hasa ikiwa ni wangu, ila ntajiskia vibaya kama ntahudumia mtoto sio wangu.

Naomba kwa anaejua gharama na taratibu za kupima DNA anijulishe mana hili swala ni gumu sana kwangu. Ikiwa gharama ni rafiki basi nikapime.

Asante
kama hamjaoana kidinoi, mlikuwa mahawara tiu. Mtoto siyo wako. Wewe lea tu ukiweza, kama huwezi wacha wenzako walee.

Unampima DNA ili iweje?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom