Habari zenu wakuu.
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu, nina mdogo wangu wa kike anahitaji kwenda jeshini ili aje kuwa mwanajeshi officer yaani mwenye nyota, na elimu yake ni bachelor degree.
Kwa anayefahamu, ninaomba kujua jeshini inahitajika elimu gani ili mtu aweze kuwa officer yaani kuwa na nyota? Pia ningependa kujua na mishahara ya kila cheo kama ikiwezekana.
Na je, course za officers huwa zinachukua muda gani kuhitimu hadi apewe hicho cheo? Yaani kuanzia JKT hadi TMA jumla ni muda gani na je kama anataka kuwa officer ni lazima apitie kwanza JKT au anaweza hata kwenda TMA moja kwa moja?
Kwa anayejua chochote kuhusiana na haya mambo msaada tafadhali.