Msaada: Kila nikipata pesa linafata tatizo

Msaada: Kila nikipata pesa linafata tatizo

washeby

Member
Joined
May 28, 2015
Posts
32
Reaction score
4
Nina bahati ya kupata hela,kila nikizipata linafata tatizo sijawahi fanya kitu cha maana.

Msaada tafadhali

 
nenda kwa walokole ukaombewe tatizo litaisha, hiyo ni roho ya ufukara inakufuatilia.
 
Pole nkuu! nenda kwenye makanisa ya kilokole ukaombewe roho ya ufukara inakunyemelea!
 
Hiyo ni inshu ndogo inawezekana kuna roho ya kifungo inakufatilia pia roho ya kutokustawi,ushauri wangu ni kwmba kama hujaokoka tafuta kanisa la kiroho lililokaribu ukaongozwe sala ya toba uokoke na baada ya hapo ukishafunguliwa kila ukipata hela kwnye mapato yako katoe fungu la kumi (10%) ya mapato yako yote unayopataga,hiyo itasaidia pia kufungua baraka zako nyingi na pia kuiwekea ulinzi fedha yako iliyobakia na matatizo hayatakupata mara kwa mara
N.B usipookoka hata uwe unalala kanisani au unaombewa kila siku kamwe matatzo hayataisha kukuandama.
 
Nami pia nina ibirisi hilo, mpaka msemo wa "ng'ombe wa masikini azai" unaanza kunitawala.
 
Hiyo ni inshu ndogo inawezekana kuna roho ya kifungo inakufatilia pia roho ya kutokustawi,ushauri wangu ni kwmba kama hujaokoka tafuta kanisa la kiroho lililokaribu ukaongozwe sala ya toba uokoke na baada ya hapo ukishafunguliwa kila ukipata hela kwnye mapato yako katoe fungu la kumi (10%) ya mapato yako yote unayopataga,hiyo itasaidia pia kufungua baraka zako nyingi na pia kuiwekea ulinzi fedha yako iliyobakia na matatizo hayatakupata mara kwa mara
N.B usipookoka hata uwe unalala kanisani au unaombewa kila siku kamwe matatzo hayataisha kukuandama.

Na mwislam afanyeje?
 
Hiyo ni inshu ndogo inawezekana kuna roho ya kifungo inakufatilia pia roho ya kutokustawi,ushauri wangu ni kwmba kama hujaokoka tafuta kanisa la kiroho lililokaribu ukaongozwe sala ya toba uokoke na baada ya hapo ukishafunguliwa kila ukipata hela kwnye mapato yako katoe fungu la kumi (10%) ya mapato yako yote unayopataga,hiyo itasaidia pia kufungua baraka zako nyingi na pia kuiwekea ulinzi fedha yako iliyobakia na matatizo hayatakupata mara kwa mara
N.B usipookoka hata uwe unalala kanisani au unaombewa kila siku kamwe matatzo hayataisha kukuandama.

Stunna acha kudanganya watu!,hivi unataka kuniambia Majaribu km haya huwakuta wasiookoka tu??,Kumbuka kuwa Mkristu aliyekamilika ni lazima ajaribiwe ili aweze kuthibitisha Imani yake,Na unaposema kuwa kuna Makanisa ya Kiroho,Je ni yepi hayo??,na je Makanisa ya Kimwili ni yepi??.Makanisa ya Kiroho maana yake ni nini???.
 
ukienda kwa walokole mwisho wa siku utaambiwa utoe fungu la kumi .Siku hizi wachungaji wengi ni makanjanja wako kupiga pesa.

Wewe omba unavyojua wewe na kuamini kwa Mungu kila jambo litaenda poa pia inaonyesha unakuwa hauna plan .

yani mpaka unapata pesa haujui ufanye nini ndio maana unatumia yote,ukae ukijua matatizo hayaishi duniani bali ni lazima uwe na vipaumbele vyako ambapo ukipata pesa inaenda uko
 
Makanisa ya kwenda ni Roman Catholic church au Anglican church (CPT) au KKKT, ya kiroho ni ya wahuni walioasi kwenye makanisa halali. Yaani usiende kwenye kanisa ambalo kiongozi wake ni mtu wa kawaida tu aliyemjasiriamali wa kupiga hela za watu na wake zao. Utakuta mchungaji/nabii/mtume hajasomea mahali popote ila atakuambia anafufua watu wakati hata kuku hajawahi kufufua.

Kwa imani yako mwenyewe muombe MUNGU kwani hata wewe anakusikia tena vizuri tu ukiwa chumbani kwako. Ila jumapili hudhuria kwenye ibada kwenye makanisa tajwa hapo juu.
 
Naomba kupingana na wote waliotoa ushauri kuwa aendw kwenye makanisa ya kilokole/kiroho.

1. Issue ya kiimani inahitaji imani hasa, iwapo akienda na hana imani ni kazi bure.

2. Kwa imani yake aliyonayo kwa Mungu iwe ni Mkristo au Mwislam, kwanza aanze kujitathimini mwenyewe je ana uhusiano mzuri na Mungu wake? Mf. Je anatoa sehemu ya kumi ya mapato yake katika dhehebu lake? (nina imani wakristo na waislamu huwa tuna hii ibada) iwapo hatoa basi asali na kuomba msamaha kwa kutotoa hiyo sadaka /zaka.

3. Kama kuna matendo mabaya aliwahi kuwafanyia watu kama vile kudhulumu au njia anayotumia kupata hizo pesa sio halali hakika hazitadumu ndio sababu zinaondoka kupitia matatizo.

4. Kama ulikuwa huwasaidii wahitaji anza leo, ila angalia kuna matapeli wengi katika hili

Mwisho sali/omba Mungu akuondolee hilo pepo la matatizo baada ya kujitathimini. Usiamini katika kwenda kuombewa kwani huko wanatoza fedha kwa ajili ya kufunguliwa n.k.

Ni mtazamo wangu CL...
 
Una pepo la umasikini, dawa ni kutambua kiini cha tatizo then deal nalo hadi kieleweke, wapo watu wengi wanateswa na hili, na wengine wamepata msaada na wanakula mema ya nchi
 
Mkuu si kila tatizo ni jaribu. Pia ni vema utambue tofauti ya jaribu na tatizo, jaribu huwapata watu wenye msimamo thabiti wa kiroho na lengo ni kuwatenga na Mungu eg Yesu mlimani, Ayubu nk. Lakini matatizo matukio mabaya na yasiyoeleweka chanzo yenye kusononesha moyo nk
 
Stunna acha kudanganya watu!,hivi unataka kuniambia Majaribu km haya huwakuta wasiookoka tu??,Kumbuka kuwa Mkristu aliyekamilika ni lazima ajaribiwe ili aweze kuthibitisha Imani yake,Na unaposema kuwa kuna Makanisa ya Kiroho,Je ni yepi hayo??,na je Makanisa ya Kimwili ni yepi??.Makanisa ya Kiroho maana yake ni nini???.

Upo sawa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom