Msaada: Kila nikipata pesa linafata tatizo

Msaada: Kila nikipata pesa linafata tatizo

Nina bahati ya kupata hela,kila nikizipata linafata tatizo sijawahi fanya kitu cha maana.

Msaada tafadhali

mkuu labda kila tatizo unalitatua kwa pesa ndo maana kila siku unaona azitoshi anyway katika kila shida kuna fursa ukiweza kugundua na kizitumia vizuri utafanikiwa pia
 
Tatizo hilo sio lako tu, hata mimi pia.
Kila nikipata hela za madini wanawake wananipapatikia nao ujue wanakuja na matatizo yao ya kufunguliwa salon, maduka ya nguo na Tigo pesa, pesa ikikatika wanapotea kidogo.
Nikizipata tena wananipapatikia tena warembo zaidi, kwa kweli nimewakanyaga sana ila hata kiwanja sina, sijui ni mkosi gani niliokua nao.
Najitahidi sana hata wakati mwingine kuweka hela benki lakini wanawake wa mjini wanajua jinsi ya kunilainisha, mpaka nakwenda kutoa. Pale Mwenge kuna salon tano zimetokea mikononi mwangu na sasa hivi tumebaki kusalimiana tu, sana sana naishia ofa ya konyagi.
Safari hii nikizifuma tu naoa na kununua kiwanja Mabwepande labda huko hakuna wanawake wenye ushawishi kama Sinza.

Baba huruma
 
Ni kwa sababu huna masimamo na kile ulichokiwsha panga kukifanya. Kama umepanga kufanya jambi fulani, ukapata pesa na ghfla tatizo likajitokeza, acha hilo tatizo lingoje kwanza fanya ulichopanga. Kufikia mafanikio siyo kitu rahisi, ndiyo maana waliofanikiwa wanaonekana ni watu wenye dharau, waliosahahu walipotoka, ukimplekea shida hakusaidii kwa wakati.
 
Unatakiwa kushukuru kwani fedha zinakuja tatizo linapokaribia kutokea fikiria ukipata tatizo na
hela hakuna
 
Pole nkuu! nenda kwenye makanisa ya kilokole ukaombewe roho ya ufukara inakunyemelea!
Huko ndo atazimaliza kabisa kwa njia ya 'mtolee mungu' huku matatizo yake kuongezeka maradufu. Mwisho wake ni frustrations.
 
Pesa hazikupendi mkuu, hivyo kaa mbali na pesa kuepuka matatizo.
Pia, usije ukawaza kwenda kukanyaga mafuta ya upako.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
washeby kwani pesa unatafuta za nini, si ni pamoja na kutatua hayo matatizo. acha pesa ifanye kazi yake.

inawezekana pia hutoi zaka na sadaka. "BLESSED ARE HANDS THAT GIVE"
Hajui kazi ya pesa huyo. Yeye anataka azitunze tu awe anazionaona.
 
Tatizo ni wewe mwenyewe. Umewekeza zaidi katika mawazo ya kuwa kila ukipata fedha unapata tatizo. Sasa hapo tatizo la kwanza ni tatizo la kuhisi kila kinachofuata ni tatizo. Ada za shule umezifanya kama tatizo, kulipa bila za maji na umeme unauotumia umetafsili kama tatizo , Kodi ya nyumba uliopanga unaona nalo ni tatizo, kujitibia mwenyewe afya yako na watoto unaona pia ni tatizo, sasa kila kitu umefananisha na tatizo. Punguza kabisa hisia hizo na kuamini kila kitu ni tatizo mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chukua kitambaa Cheupe, weka chumvi ya mawe na unga wa pilipili nyekundu fungia kwenye kitambaa cheupe uwe unaweka mfukoni na ukilala weka chini ya mto, pia kama ni nuksi ndogo ogea maji ya chumvi kwa siku 14.

Usisahau kuomba
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom